Hawa watu sasa wamekubali kuwa Corona imeisha?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,227
113,583
Toka mwanzo na mpaka sasa, msimamo wangu kuhusu hii Corona ni sawasawa na ule wa Rais Magufuli.

Si ajabu pia, kuwa, msimamo wangu waweza kuwa ni mkali zaidi kushinda hata huo wa Rais Magufuli.

Yaani, COVID-19 si hatari kama tulivyoaminishwa. Tumelishwa matango pori.

Jana nilimwona Bernard Membe akienda kuchukua fomu za kugombea urais.

Alipofika hapo ofisini, akasalimiana na mtu kwa kushikana mikono. Sikuona watu wakiwa wamevaa upuuzi wa barakoa. Sikuona watu wakiwa wamekaa mbalimbali.

Wakina mama waliokuwepo walikuwa wakiimba. Inasemekana katika kuimba, vichembe chembe vya mate huwa vinaruka na hivyo kuwezesha kiurahisi maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

Kipindi Corona inabamba, hawa watu wa kambi ya upinzani ndo walikuwa mstari wa mbele kumnanga Rais Magufuli kuhusu msimamo wake wa hivyo virusi.

Sasa hebu tazama video hii! Imekuwaje? Hao wapinzani sasa wamekubali kuwa Corona si hatari kivile?

Mpende au umchukie, kiukweli Magufuli kwa misimamo yake lazima umheshimu tu.

 
Daktari mmoja wa WHO alisema haafiki kutokutoa taarifa za maambukizi ila anamsifu JPM kwa kuwa na msimamo. Akasema lockdown kwa nchi zetu haiwezi leta tija.

Akamalizia yeye anapenda sana mtu anayesimamia maamuzi yake na kutokuyumbishwa, akaenda mbali zaidi kwamba hata kama anachosimamia hakipo sahihi ila kwake ni ule msimamo wa mtu ana uheshim sana kuliko mtu anaebadilikabadilika.
 
Daktari mmoja wa WHO alisema haafiki kutokutoa taarifa za maambukizi ila anamsifu JPM kwa kuwa na msimamo. Akasema lockdown kwa nchi zetu haiwezi leta tija.

Akamalizia yeye anapenda sana mtu anayesimamia maamuzi yake na kutokuyumbishwa, akaenda mbali zaidi kwamba hata kama anachosimamia hakipo sahihi ila kwake ni ule msimamo wa mtu ana uheshim sana kuliko mtu anaebadilikabadilika.

Sina uhakika sana, ila ngoja niulize.

Je, nchini Tanzania watu wanakufa kama nzi waliopuliziwa dawa ya kuua wadudu?

Maana kwa hivi sasa sioni tahadhari zozote zile zilizopendekezwa zikichukuliwa na watu nchini Tanzania....
 
Japokuwa watu wamepuuzia kiasi flani ila ukweli ni kwamba covid19 ipo bado, tunaishi nayo na most likely ilikuwepo TZ tangu 2018. Kuvaa barakoa pekee might not be the most effective way ya kuizuia
Kama ipo tokea 2018 basi si hatari kivile tulivyoaminishwa.

La sivyo, ingekuwa ni hatari kama tulivyoaminishwa, wengi wetu tungekuwa tushakufa.
 
Sina uhakika sana, ila ngoja niulize.

Je, nchini Tanzania watu wanakufa kama nzi waliopuliziwa dawa ya kuua wadudu?

Maana kwa hivi sasa sioni tahadhari zozote zile zilizopendekezwa zikichukuliwa na watu nchini Tanzania....


Yule mzee nae alikua anatetea kibarua chake, nikamuuliza kuna umuhimu gani kutolea taarifa maambukizi ambayo hata mtu akigundulika ana Corona hapatiwi matibabu zaidi yakutengwa? Na kwakua vipimo havifanyiki nchi nzima kwa mkupuo hauoni kwamba inaleta usumbufu usio na tija kuhangaisha watu bila sababu ukizingatia kwetu vifo sio kama huko nchi za watu?

Akaendelea kupiga fundo la kilevi nikajua hata wenyewe hawana muongozo wa kueleweka kuhusu namna bora ya kukabiliana na Corona achilia mbali kuielewa Covid 19 yenyewe.
 
Membe kajipaka vitakasa mikono pia alinawa mikono baada ya kutoka pale na kwenda kutafuna tangawizi kunywa maji ya limau Asprin kwa wingi, corona ipo nyingi hapo jijini Dsm lakini kwa kuwa watu wameamua kufanya siri hawataki kusema ndugu zao wamekufa kwa covid 19 bali husingizia ni magonjwa mengine ya kawaida tu, wengi hawataki ijulikane wana mgonjwa wa corona kwao wakihofia kutengwa na jamii zilizowazunguka, hilo jiji la Dsm lina watu zaidi ya milion 5 na wengi huishi uswahilini kwenye misongamano mkubwa ambapo hufa wengi lakini wanafanya siri huku wewe na CCM mkiendelea kuwahadaa watanzania kuwa corona imekwisha Tanzania.
 
Jasusi mbobezi aliwahi kusema Tanzania itatengwa na jumuiya za kimataifa kwa vile tu imechukua hatua tofauti na jumuiya za mataifa mengine katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona
Mashirika ya Ndege ya kimataifa bado yanaitenga Tanzania ni Ndege chache za kimataifa zinakuja hapo Dsm, nyinyi mnasema corona haipo lakini ofisi za Balozi wana taarifa za kwenye jamii kote wanajua corona ipo kwa wingi.
 
Kama ipo tokea 2018 basi si hatari kivile tulivyoaminishwa.
Kweli. Ninawafahamu angalau watu 11 walioipata na kupona baada ya kujidunga mixer za tangawizi, kitunguu swaumu, kitunguu maji, pilipili kichaa na limao. Hii kitu imetuspare waafrica. Wazungu hata flu tu huwaua sana
 
Corona ipo kwa wingi hapo jijini Dsm, Dodoma, Arusha na Mwanza, Moshi, Mbeya kidogo lakini corona ipo Tanzania haijakwisha inaendelea kuua watu kwa siri na wengi hawasemi kuwa ni corona hupakazia magonjwa mengi kuepuka kutengwa na jamii.
 
We vipi
Corona kutokuwepo sasa haimaanishi kipindi kile haikuwepo..
Halafu acheni kufanya kama Afrika nzima Magufuli peke ake hakuweka lockdown..
Nitajie nchi nyingine zaidi ya Kenya,Uganda,Rwanda,South Africa na Nigeria zilizokuwa na lockdown.
Unamaanisha nje na nchi ulizozitaja hakuna nyingine iliyoweka lockdown....

Straighten hoja yako usaidiwe majibu?
 
Back
Top Bottom