Hawa panya wa kisasa mbona balaa

Hawa panya wa kisasa mbona balaa

Umuofia kwenu, kwa takribani miezi minne sasa nilishuhudia mbegu mpya kabisa ya panya nyumbani kwangu.
Mkuu,
Upo mkoa gani?
Na kupita kabisa, mbaya kuliko wanazaliana kama utitiri yani
Duh
Wakuu kama kuna mtu anafahamu ile gundi maalum ipo kwenye tube kama ya baiskeli naomba aniambie
Wauzaji karibu wote wa sumu na mitego ya panya wanakuwa na hiyo gundi..

Em tupia picha tuwaone hao panya wa kibabe basi
 
Umuofia kwenu, kwa takribani miezi minne sasa nilishuhudia mbegu mpya kabisa ya panya nyumbani kwangu.

Panya hao wana muonekano tofauti na hawa wetu na cha ajabu kabisa wanawawinda panya wale wa asili na kuwaua kabisa.

Mdomo wao ni mrefu kama nguruwe hivi,
Na ajabu yao pia hawa panya hata paka hawali, ukiwategea sumu hawali ,
Wana mwili ambao una mijongeo ya ajabu ,nasemea hili kwa sababu panya hawa hata pawe na tundu dogo kiasi gani atajiminya

Na kupita kabisa, mbaya kuliko wanazaliana kama utitiri yani

Nimetumia Indocid yani naona kama ilikua cow bell kwao ,nikatumia masumu ya mitaani mpaka madukani bila bila,

Nikajitahidi kuzidisha usafi na kutokuacha uchafu kwa namna yoyote hapo wakaanza kula gypsum sasa ,

Wakuu kama kuna mtu anafahamu ile gundi maalum ipo kwenye tube kama ya baiskeli naomba aniambie

Ntaipata wapi mana najua ile kidogo ni suluhisho nje ya hapo sijui na panya hawa sijafanikiwa kupata picha ila usiombee🥹🥹🥹
watu mliozaliwa mijini mnakosa mengi sana. sisi wengine tuliishi na mapanya nyumbani mnafukuzana nayo balaa, mengi tu kwasababu kwa bibi nyumba ni hiyo hiyo na sehemu ya kuwekea mazao ni hiyohiyo mumo kwa mumo.

kuna panya hawa wa kawaida, halafu kuna aina fulani ya panya wembamba wana midomo mirefu na vimacho vidogo sana, hawa huwa hawali nyasi, chakula chao ni panya, na huwa wanawinda panya. wana nusa sana kuliko kuona, na wakianza kumfukuza panya hadi wanamkamata, hawana shida na mazao yako wala chochote, wao ni carnibals wa panya. kama haujui mbio za panya ni pale huyu akiingia kwenye nyumba yako huwa wanakimbia kabisa. nadhani utakuwa unaongelea hao. kwa bibi yangu mzaa mama Iringa huwa wanaita "vinyunga" kama kuna mhehe hapa afafanue.
 
Na wanaangua kicheko kama binadamu! Hiyo ni mizimu imekuja kwa sura ya panya! Sasa kuna vindege vidogo vya kijani na vyekundu navyo ni shida
huyo ni panya wa kawaida kabisa, kwa walioishi vijijini wanamjua, na chakula chake huwa ananyonya damu ya panya wenzake. ukimpiga au akihisi hofu huwa analia chwiii chwiii, halii kama panya wa kawaida, ni aina yake na ni kiumbe cha Mungu cha kawaida kabisa, tumeisho tukiviona mno.
 
huyo ni panya wa kawaida kabisa, kwa walioishi vijijini wanamjua, na chakula chake huwa ananyonya damu ya panya wenzake. ukimpiga au akihisi hofu huwa analia chwiii chwiii, halii kama panya wa kawaida, ni aina yake na ni kiumbe cha Mungu cha kawaida kabisa, tumeisho tukiviona mno.
Si ndo hiyo sijui wanacheka au wanalia? Panya gani hao!! Ni laana! Walikujaga kwangu nikawa mawavizia wakiingia kwenye pazia la dirisha wakidhani wamejificha nikambonda mmoja kwa kiatu na kumuua! Walikimbia wote ni zaidi ya mwaka sijawahi kuwaona tena! Hao panya huwezi kuwatega kwa mbinu zozote za binadamu! Ni mashetani
 
Si ndo hiyo sijui wanacheka au wanalia? Panya gani hao!! Ni laana!
ni panya ambao wapo sana mashambani huko, chakula chake ni panya wenzake na huwa wananuka, wanatoa harufu mbaya hao. wala sio mashetani wala chochote, mashambani wakati tunalima huwa tunawaona, nilivyoishi kijijini nawafahamu ni panya wa kawaida. shida ninyi wa mjini mnaona kitu cha ajabu.


18835.jpg
75753979_gwts1-ruth-carden-ucd.jpg--_75753979_gwts1_ruth_carden_ucd.jpg
 
Back
Top Bottom