Hawa ndiyo wabunge wa viti Maalum CHADEMA, CCM na CUF

Kama mfumo wa kupata watakaochaguliwa kuwa wabunge wa viti maalum utakuwa ni ule uliotangazwa na Kitila Kitumbo basi CHADEMA itakuwa imekosea sana.

Kwa maoni yangu viti maalum visitumike kama asante kwa watu bali kama ni mkakati wa kukiongezea chama mawanda yake na kukijengea umaarufu zaidi kwa jamii.

Kwa mfano kuna haja gani kwa mkoa wenye wabunge wengi wa CHADEMA kupewa tena wabunge wa vii maalum. Na kwenye tayari mbunge wa kuchaguliwa jee kuna haja ya kuteua tena mbunge wa kiti maalum ili afanye nini?

Ingekuwa bora kama CHADEMA ingechagua wabunge wa viti maalum (wanaofaa lakini) kutoka kwenye ile mikoa na majimbo ambayo hayana wabunge wa kuchaguliwa. lengo ni kutumia wabunge hao wa kuteuliwa kama changamoto kwa wabunge wa kuchaguliwa wa CCM (WATCH DOG).

Kilimanjaro ina haja gani tena ya kuwa na mbunge wa viti maalum kuliko Mtwara, au Mbeya mjini kuliko jimbo la Rungwe?


Mi nafikiri la muhimu kwanza ni kumpata mwenye moyo wa kukijenga chama kutegemea na uwezo wake wa kujenga hoja na kutoa muda wake kukisaidia chama. Huu ni wakati wa mapambano. Hata Jeshini huwezi kumweka kamanda legelege kwa sababu ati anatoka mkoa fulani. Ujasiri, umakini, na moyo wa kukitumikia chama wakati wa shida na wakkati wa raha ni muhimu zaidi.

Kama wapo wanaotoka mikoa ambayo haikupata wabunge ambao ni majasiri na wanajua kujenga hoja ni vizuri zaidi wakachukuliwa hao. Kama hawapo si vizuri ukamuokota mtu ukamwambia nenda bungeni wakati haoni kuna tatizo.
 
CHADEMA inautaratibu wa jinsi ya kupata wateule wake na unazingatia athari na faida za kutapanya jitihada. Pia CHADEMA inaamini katika kujenga himaya imara kabla ya kuanza kusplip efforts ambazo baadae huenda zisizae matunda na kuelekea kupoteza hata kile ulichokua nacho. Tumeona manufaa ya Dr Kufocus lake na Southern Highlands baada ya strong hold ya Nothern. Ingekua equal effort ingewekwa kwa Kigoma na kuondokana na kwamba sasa twende kwingine maana kigoma tunanguvu na tumekuwepo mda mrefu, basi leo tusingeshuhudia NCCR kikiwa na nguvu za kutisha Kigoma zaidi ya CHADEMA

Itikadi iwe ni kulinda kwa nguvu zote kile tulichonacho na wakati huo huo tukitafuta njia ya kuingia maeneo mapya. After all sidhani kama ni party decision juu ya ni wapi mbunge wa viti maalumu atoke maana nadhani inategemea na idadi ya kura za mbuge wa kuchaguliwa na raisi katika mkoa na majimbo husika
 
Ni kweli kuangalia hali ya mtandao wa wabunge waliochaguliwa majimboni ,ni muhimu katika kuamua wbunge wa kuteuliwa CHADEMA tafakarini hili!
 
sasa majina yamekwisha pelekwa tume ya uchaguzi tangu 30/09, haiwezekani....kinachoangaliwa ni chama kinapewa wabuge 10 inamaana waanangalia kumi bora kwenye orodha iliyopelekwa na chama
 
Mbunge wa kiti maalum hana jimbo, utamuhusishaje na mkoa? Au kwa ukabila?

Naona CCM wanahusisha na mkoa maana kila mkoa unatoa wagombea wawili. Huenda hiyo ni njia bora zaidi kuliko hii ya kuteua makao makuu.
 
Kwa mahesabu ya haraka haraka, wafuatao wataenda bungeni kupitia CHADEMA viti maalum.

1.Lucy Owenya
2.Eather matiko
3. Mhonga Ruhwanya
4.Anna Mallac
5. Paulina Gekul
6. Conjesta Rwamlaza
7.Susan Kiwanga
8.Grace Kiwelu
9. Susan Lyimo
10. Regia Mtema
11.Christowaja Mtinda
12.Anna Komu
13.Mwanamrisho Abama
14.Joyce Mukya
15. Naomi Kaihula
16. Chiku Abwao
17. Rose Kamil Sukum
18. Christina Lissu Mughiwa
19. Raya Hamisi
20. Philipa Mturano

Namba inaweza kupungua kidogo au kuongezeka kidogo lakini mpaka sasa kwa mahesabu yangu nahisi hao hapo juu watafanikiwa kuingia Mjengoni.

Naona mzee Ndesamburo atakuwa yeye baba, mtoto na mkwe wake. Itabidi mtoto na mkwe wajiheshimu huko bungeni maana baba atakuwa anawaangalia.
 
Kwa mahesabu ya haraka haraka hawa hapa chini watakuwa wamepeta kwenye viti maalumu kupitia CCM. Namba inaweza kuongezeka kidogo ila nafikiri hawa 50 wana uhakika wa kuingia mjengoni.

Hii ya Rita Mlaki kukimbia jimbo lake na kisha kupewa nafasi kupitia NGO naona halifai kabisa. Wangetoa nafasi hiyo kwa watu wapya.

(i) Viongozi Wakuu wa UWT
1.Ndg Sophia Mnyambi Simba (Mwenyekiti)

2.Ndg Amina Nassoro Makilagi (Katibu Mkuu)

(ii) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya kwanza)
Mara
3.Ndg. Gaudentia Mugosi Kabaka
Tanga
4.Ndg. Ummi Ally Mwalimu
Mtwara
5.Ndg. Agness Elias Hokororo
Manyara
6.Ndg. Martha Jachi Umbulla
Shinyanga
7.Ndg. Lucy Thomas Mayenga
Kusini Pemba
8.Ndg. Faida Mohamed Bakari
Dodoma
9.Ndg. Felista Alois Bura
Kaskazini Unguja
10. Ndg. Kidawa Hamid Saleh
Ruvuma
11. Ndg. Stella Martine Manyanya
Mwanza
12. Ndg. Maria Ibeshi Hewa
Mbeya
13. Ndg. Hilda Cynthia Ngoye
Kigoma
14. Ndg. Josephine Johnson Genzabuke
Simiyu
15. Ndg. Esther Lukago Midimu
Kaskazini pemba
16. Ndg. Maida Hamad Abdalla
Kusini Unguja
17. Ndg. Asha Mshimba Jecha
Dar es Salaam
18. Ndg. Zarina Shamte Madabida
Arusha
19. Ndg. Namalok Edward Sokoinei
Tabora
20. Ndg. Munde Tambwe Abdallah
Kagera
21. Ndg. Benardetha Kasabago Mushashu
Geita
22. Ndg. Vick P. Kamata
Njombe
23. Ndg. Pindi Hazara Chana
Lindi
24. Ndg. Fatuma Abdallah Mikidadi
Morogoro
25. Ndg. Getrude Rwakatare
Kilimanjaro
26. Ndg. Betty E. Machangu
Singida
27. Ndg. Diana Mkumbo Chilolo
Mjini Magharibi
28. Ndg. Fakharia Shomari Khamis
Pwani
29. Ndg. Zaynabu Matitu Vulu
Rukwa
30. Ndg. Abia Muhama Nyabakari
Katavi
31. Ndg. Pudenciana Kikwembe
Iringa
32. Ndg. Lediana Mafuru Mng'ong'o


(iii) Kundi la Vijana T/Bara (nafasi tatu)
33. Ndg. Sarah Msafiri Ally
34. Ndg. Catherine V. Magige
35. Ndg. Ester Amos Bulaya
36. Ndg. Neema Mgaya Hamid

(iv) Kundi la Vijana T/Zanzibar (nafasi 2)
37. Ndg. Tauhida Galos Cassian
38. Ndg. Asha Mohamed Omari

(v) Kundi la NGO's (nafasi 2)
39. Ndg. Rita Louis Mlaki
40. Ndg. Anna Margreth Abdallah

(vi) Kundi la Vyuo Vikuu (nafasi 2)
41. Dkt. Fenella E. Mukangara
42. Ndg. Terezya Lwoga Huvisa

(vii) Wanawake wenye Ulemavu (nafasi 2)
3. Ndg. Al-Shaymaa Kwegir
44.Ndg. Margreth Mkanga

(viii) Kundi la Wafanyakazi (nafasi 2)
45. Ndg. Angellah Jasmin Kairuki
46.Ndg. Zainab Rashid Kawawa

(ix) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya pili)
Kusini Pemba
47.Ndg. Mwanakhamis Kassim Said
Lindi
48.Ndg. Riziki Said Lulida
Ruvuma
49.Ndg. Devotha Mkuwa Likokola
Morogoro
50.Ndg. Christina Ishengoma
 
We should focus on value addition rather than equity, hasa ukizingatia kuwa bunge lijalo vihio ni wengi, rather than equity in allocation, i would like to focus on analytical capacities, capacity to influence and manage dialogue. Remember tanzanian people will judge us based on the quality of our contribution and the dynamism we will create in the parliament.
mkuu tupe formula ya kupata number ya viti maalum, nasikia inategemea na number ya kura za urais na viti vya ubunge, jee formula yake itakuwaje kama chadema itapata wabunge 30, na kura mil4-mil5 za urais, kwa mfano.
 
Mkuu Kiranga,

Kitu alichokuwa anakizungumzia ndugu yetu pale juu ni kuwa mikoa ambayo imepata wabunge basi ipewe nafasi ndogo kwenye viti maalum, ili viti maalumu ving viende mikoa ambayo haina wabunge bungeni, let say its better kuwa na mbunge wa viti maalum Mtwara na Lindi than in Arusha,Moshi, Manyara, Mwanza or Dar es salaam, hii itasaidia kuwatandaza wabunge all over Tanzania, na hivyo kuongeza umaarufu mikoa ambayo bado vugu vugu liko chini.

Mazee, sijauliza mnapeleka wapi viti maalum, hilo unalolisema limeelezwa na nimeelewa, ila halijibu swali langu.

Mimi nauliza "nitafikaje Muhimbili" wewe unanijibu "Muhimbili ni hospitali nzuri, ina wodi za Sewa Haji Mwaisela na nini sijui, imejipanga hivi na hivi" ndiyo ndiyo ndiyo, nitafikaje huko ?

Hujajibu swali la msingi hapo juu. Utamhusishaje mtu na mkoa wakati mbunge wa kiti maalum hana jimbo analogombea? Utaangalia kabila lake, makazi yake, alipooa, anapofanya kazi, sehemu alipojenga au vipi? Utaweka link gani kati ya mtu na mkoa katika situation ambapo mtu hafanyi kampeni kushinda jimbo fulani? Na mathalani ukitumia makazi ya mtu, ukishampa ubunge ataruhusiwa kuhama au hataruhusiwa, kama ataruhusiwa whats the point of using makazi?

Mnahusishaje mkoa na ubunge wa viti maalum? Kwa ukabila ?
 
Viti maalumu hutokana na uiano wa kura. kwa hiyo ccm mwaka huu wamelimia nyani,watavuna mabua. idadi yao itashuka sana.
 
Mbunge wa kiti maalum hana jimbo, utamuhusishaje na mkoa? Au kwa ukabila?
Hakuna mahali nilipotaja ukabila kwenye thread au Post yangu. Hoja hapa kuna haja gani kwa mikoa yenye wabunge tayari au majimbo yenye wabunge kuwa tena kwenye Orodha ya wabunge wa Viti maalum. kwa nini wale wanawake waliojaza fomu za kuomba kuteuliwa kuwa kwenye orodha wa wabunge wa viti maalum kutoka kwenye majimbo au mikoa isiyo na wabunge wa CHADEMA wasifikiriwe kwanza?
 
We should focus on value addition rather than equity, hasa ukizingatia kuwa bunge lijalo vihio ni wengi, rather than equity in allocation, i would like to focus on analytical capacities, capacity to influence and manage dialogue. Remember tanzanian people will judge us based on the quality of our contribution and the dynamism we will create in the parliament.
Nani kakakwambia kwamba kule ambako hakuna wabunge wa CHADEMA wale walioomba hawana capacity to influence.. Kuchagua kutoka kwenye mikoa isiyo na wabunge wa kuchaguliwa wa CHADEMA haimaanishi kuokota hovyo hovyo kila aliyeoomba.
 
Kwa nini mk ulima unaitakia mabaya ccm, inaonesha kwa jinsi ulivyo na roho mbaya ya kutompenda jirani yako kwa wivu wa maendeleo.
Naomba upange na viti vya Chadema, Cuf, Nccr mageuzi, Tlp na kadhalika manake wewe ni mtaalamu wa kuchakachua orodha ya watu
wasokuhusu. nashukuru kwa kuzipata orodha hizo na unambie ni kigezo gani ulichotumia kupata 50 na wengine watapata kwa uwiano gani.
 
Hujajibu swali la msingi hapo juu. Utamhusishaje mtu na mkoa wakati mbunge wa kiti maalum hana jimbo analogombea? Utaangalia kabila lake, makazi yake, alipooa, anapofanya kazi, sehemu alipojenga...
inaonyesha ndugu yangu hujui kabisa kinachoendelea kwenye hili jambo. Walioomba kuteuliwa viti maalum CHADEMA walipitishia maombi yao kwenye majimbo na ngazi ya taifa. Na wastani wagombea kwenye kila mkoa walikuwa wawe watatu watatu. kwa maana hiyo Yupo aliyeomba kupitia jimbo la Nyamagana na yupo mwingine wa Lindi mjini.

Sasa Nyamagana wamepata Mbunge wa kuchaguliwa wa CHADEMA. Kwa nini yule aliyeomba kupitia Lindi mjini asiteuliwe (Kama ana uwezo Lakini) badala ya kumteua wa Nyamagana ambaye jimbo lake tayari lina mbnge wa kuchaguliwa kupitia CHADEMA?
 
idadi ya wabunge wa viti maalum ni sawa na asilimia 30 ya viti vyote vya ubunge chama hicho ilichoshinda au?

utaratibu ni kuwa chama kinapeleka list ya watu wake kwa mujibu wa preference ikimaanisha kuwa wakipata nafasi 10 basi watangazwe wale kumi wa mwanzo.

zoezi la kupeleka orodha ya wabunge limeshafanyika zama nyingi sana na sasa ni kazi ya tume ya uchaguzi kuwatangaza tu.
 
idadi ya wabunge wa viti maalum ni sawa na asilimia 30 ya viti vyote vya ubunge chama hicho ilichoshinda au?

utaratibu ni kuwa chama kinapeleka list ya watu wake kwa mujibu wa preference ikimaanisha kuwa wakipata nafasi 10 basi watangazwe wale kumi wa mwanzo.

zoezi la kupeleka orodha ya wabunge limeshafanyika zama nyingi sana na sasa ni kazi ya tume ya uchaguzi kuwatangaza tu.
Inaonyesha kwamba mfumo wa kuiachia Tume kuteua wabunge kwa kufuata namba kwenye orodha ni mbaya. Kuiachia tume kuteua wabunge kutoka kwenye orodha waliyopelekewa ni kuviza demokrasia na kuondoa vipaumbele vya chama.

Kwa Mfano katikati ya kampeni chama kinagundua mmoja kati ya waliopeleka majina yao tume ni msaliti, lakini hakuna ushahidi wa kumfukuza chama, huyo naye kwa sababu yuko kwenye namba moja ya Orodha basi na yeye ateuliwe!!??
 
Inaonyesha kwamba mfumo wa kuiachia Tume kuteua wabunge kwa kufuata namba kwenye orodha ni mbaya. Kuiachia tume kuteua wabunge kutoka kwenye orodha waliyopelekewa ni kuviza demokrasia na kuondoa vipaumbele vya chama.

Kwa Mfano katikati ya kampeni chama kinagundua mmoja kati ya waliopeleka majina yao tume ni msaliti, lakini hakuna ushahidi wa kumfukuza chama, huyo naye kwa sababu yuko kwenye namba moja ya Orodha basi na yeye ateuliwe!!??

ndio eee ......lakini haya majina yanapelekwa just before kampeni rasmi kuanza. kwa hiyo nadhani ni sahihi kwa tume kufikiri kuwa chama hakitaka kufanya mabadiliko.
 
mi ningependa pia kuwe na wanaume wa kuteuliwa.
pia izingatiwe maeneo ya kutiliwa mkazo kama, elimu atoke mwakilishi mwenye uelewa wa mambo ya elimu, atoke mtu mwenye uelewa wa mambo ya afya an alie tayari kuyatetea kila anapoamka na kila hoja inapozuka, kilimo, viwanda, wanawake, watoto,
yani kila aina ya vita chadema inayopigania, atoke mtu mmoja, hodari, mweledi, na jasiri kuisimamia na kuipigania.
mimi sidhani kama vita muhimu Tanzania ni usawa wanawake tu,
kuna agenda nyingi sana zinahitaji wapiganaji pale bungeni.
ni kweli wanawake wanasaidia sana kusukuma agenda nyingi za maendeleo, lakini kuna nyingine zina weledi zaidi ambao si wanawake.
 
Haika

kama chama kinataka mtaalamu wa kwenda kupigania Elimu, basi na kiteuwe Mwanamke mwenye kuweza kazi hiyo. Kama chama kinataka kupigania Afya kitafute mwanamke wa kupigania hiyo, haijakatazwa.

viti maalum ni maalum kwa wanawake ili kuongeza mchango wa wanawake bungeni, na sio kwa lengo la kuongeza wapiganaji bungeni.

suala la wapiganaji chama inachotaka ama kitafute mgombea mwanamme na kihakikishe anashinda, au kitafute mwanamke mwenyew weledi huo wanaotaka.
 
Back
Top Bottom