Mie nadhani mburura nyie mnaopinga mleta mada hamnazo. Huyo Lowsa anaposema elimu bure ipi? Ya shule binafsi za watu na mashirika ya umma au ipi? Mbona hamjiulizi angalau maswali mepesi haya. Kabla ya mikopo vyuo vikuu tulikuwa tunapata kitu kinaitwa Bursary au financial support kwa mfano sie tuliotoka Bukoba tulipata hiyo financial support toka Chama Kikuu cha Ushirika Bukoba na baadaye wazee wetu wanalipa kidogo kidogo kwa kukatwa kwenye mauzo ya kahawa. Sijui kama ilikuwa bure. Lakini anaposema bure, je ni pamoja na hela ya matumizi kwenda disco nk? Au unakwenda shuleni na chuoni utajiju...Sasa hivi wanaopata mkopo wengi ni kama wanasoma bure, wengi wote ninaowafahamu hakuna hata mmoja aliyelipa mkono na wengi wanafanya kazi. Sasa nyie msioelewa kama unachagua kusomeshwa bure na kupewa mikopo chagua mikopo maana utajua namna ya kutumia hela yako na usumbuhi, na ndio maana sasa hivi wanafunzi wanapata hela yao safi na huwezi kuona wanapiga kelele. Kwa ufupi dunia nzima hakuna elimu ya bure.
EL anamnukuu Tony Blair kuhusu vipaumbele vyake kwamba ni elimu, elimu, elimu, ni kweli Tony alisema hivyo kwenye kampeini na alipoenda kwenye mdahalo anulizwa swali wewe umesema vipaumbele vyako, lakini mbona hapa Uingereza elimu ni bora, vijana wanasoma na mikopo wanapata kwa wakati na hatujawahi sikia malalamiko; akasema hamkunielewa, nilisema hivyo nikiwa na maana ya kufundisha wanasayansi zaidi ili na sisi tuvmbue vyombo vya kwenda kuvumbua sayari kama waMarekani na si kwenda mwezini kama Marekani tuvumbue sayari au twende sayari zingine kwa sababu kama ni elimu ytayari ipo sawa tunahitaji elimu mpya. Sasa ndugu yangu EL tunataka naye atueleze vizuri tu kwamba anapozungumza elimu ni elimu ipi. N anyie jiulizeni anayahisi ayasemayo? Au ni ule msemo wa Mwl. Nyerere (alazwe mahali pema peponi) kwamba ''Mtu akikwambia kitu cha KIPUMBAVU na akajua amekwambia kitu cha KIPUMBAVU ukakubaliana nacho ANAKUDHARAU'' Atakuwa anakirudia na wewe unamshangilia hata kwa kuzungusha mikono kama ZOMBI. Msiwe MAZOMBI. Anayetaka kuwa kuendelea kuwa ZOMBI kwa kuzungusha mikono anyoshe mkono.