Et mtu umheshimu kisa ana mafanikio ko asipokuwa na mafanikio unayotaka basi hastahili heshima , mtoa mada ni ndezi Sana , na ndo chanzo cha kutengeneza machawa , hii nchi vijana wamekuwa machawa na walamba miguu ya watu
Tuende poke, kwa upwndo, kwa kujengana, kwa kuelewa kuwa kuna wengi wanajifunza mambo, wanajifunza maisha.
Kitu kimoja nilichojifunza JF ni kwamba, hapa kuna watu wa kila aina, kila rila, kila uzoefu.
Kwa hivyo, unaweza kukuta watu wawili tofauti sana wanajibizana, na wasipojua kupeana nafasi ya kujibizana vizuri, kitakachofuata ni matusi.
Mtoa mada ya msingi sijui umri wala elimu rasni yake, wala upeo wake, ika nimependa sana alivyoandika.
Kitu kikubwa anafundisha au kukumbusha jamii ni kuheshimiana, kutochukuliana poa tu.
Hili ni somo zuri sana ambalo wengi tunaweza kulitumia, hata mimi.
Kitu kingine anachotufundisha ni juwa maendeleo yanahitajika, yanatuheshimisha, ni jambo ambalo linatupasa wote tulilenge.
Hapo sina cha kumpinga. Yumkini ukiwa na rafiki ambaye hana maendeleo, halafu ukakutana naye baada ya miaka michache ana maendeleo, hayo maendeleo aliyoyapata ni kitu kizuri, ni kitu cha kupigiwa mfano, si kitu cha kubezwa. Hapo sijampinga hata tone. Mimi pia hupenda kujifunza kwa watu, sio tu walioendelea zaidi yangu, bali hata wale waliojiendel3za kutoka walipokuwa mara ya mwisho mpaka walipo sasa ambao hawajaendelea kama mimi labda. Kitu muhimu ni kujua wamepigaje hatua. Maana dunia inabadilika kila simu, na pengine hata mimi ninayeweza kujiona niko zaidi yao, nikawa sijajua kupiga hatua kwa haraka na ufanisi zaixi katika dunia ya leo, nikajifun,a kitu kutoka kwao. Hapo sina tatizo.
Kwa hivyo, kimsingi, mtoa mada namuelewa sana na mambo aliyoandika ni ya msingi sana.
Nilitaka kukumbushia tu point moja ya msingi kwamba, watu wote wanastahili heshima. Waliofanikiwa na wasiofanikiwa.
Kwa sababu, kwanza, si watu wote wanaostahili heshima wanafanikiwa.
Watu wengine huwa wanaacha mambo yanayoweza kuwapa heshima katika jamii fulani - hususan kupata pesa na positions za uongozi- kwa sababu zenye kuweza kuwapa heshima ya juu zaixi ya habari za pesa na uongozi.
Kwa hivyo, unapokutana na, kwa mfano, mtu ambaye alipata nafasi ya kuibia wananchi na kuwa tajiri mkubwa sana, lakini hakufanya hivyo, akijua kuwa cheo ni dhamana, akafanya kazi kwa uadikifu, akastaafu vizuri bila kupita njia za rushwa, kwa mtazamo fulani akawa masikini, huyu ni mtu wa kuheshimiwa, si mtu wa kubezwa kwa sababu hakuiba mali za umma kama jamii yetu ilivyotarajia.
Kwa hiyo, heshima ipimwe kwa mambo mengi yenye kina, kuzidi mafanikio ya juu juu tu ya nani ana kazi gani, ana hela ngapi.
Tuangalie mchango mkubwa zaidi kwa jamii.