Hatoi matumizi ya mtoto, kaomba nimkopeshe pesa

Najua unayo Jay ila umenifanyia makusudi

Kumbuka kua ni Mbegu yangu na yai lako ndivo vimetupatia binti mrembo sana.

Maisha yanabadilika na vitu vinabadilika, mpaka imefikia wakati wa kukuomba unikopeshe utambue yakwamba nmekwama.

Mimi sio kwamba nilikua namktaa mtoto, ila kosa nipale mazingira yako ulonionyesha yakaniondolea amani,mpaka tunapima ndipo nikawa na Uhakika wa Mwanangu.


Sio kwamba sitak kuhudumia, wewe wajua kipato chang na majukum yangu nandio maana kidogo nilichopata nilikitoa, na zaidi ya yote nmekua kila siku nakuombea Wewe na Mwanangu ili muwe na maisha yenye afya njema

Nataman kuona mwanangu namsomesha naanapata huduma bora, ivo nikiwa kama mwanadam mkosaj, tambua tu ninampenda sana Mwanangu, na ninakupenda wewe nakukuheshim kwa kunizalia mtoto mzuri.


Jay, Hata ivo Adhabu yoyote utakayoamua kunipa kama hukum nitaipokea ila kumbua kua NINAKUPENDA WEWE NA MWANANGU.
Makubwa!!!
 
Thank you
lady Jay sasa nimejua ni binti. Maskini huyo mwanaume bado hajielewi! Mtoto wa Kike ndiye mkombozi wa mwanaume uzeeni. Ni kosa kubwa kwa mwanaume kumtupa mtoto wa Kike. Unapoinvest kwa mtoto wa kike unajiwekea security, hata akiwa na shilling mbili lazima atakupa moja abakie na moja. Mtoto wa kiume akikua atahangaika na mama yake na girlfriend wake. Wewe hata kukupigia simu inakuwa ni mtihani.

Jitahidi mama kuhakikisha baba yake anawajibika maana sie tumeyaona, baba hakumtunza mtoto ila akikua lazima ahangaike na baba yake. Mtoto wa Kike kwa baba ni Chanda na pete. Watoto wa kiume tunawazalia mama zao tu.

kwa upande wangu kila wakati najitahidi mtoto wa Kike afike mbali kielimu. Wakiume including me tunaboa kwa kusahau baba zetu
Asante mkuu. Ila huwezi mlazimisha mtu mzima kufanya majukumu yake.Mwenyewe babangu alikua na blabla kibao wakati wa kutoa matumizi na sijui anaendeleaje huko. Ila nikipata chochote siwezi msahau mamangu.

Watoto wanakua na wanaona. Huo muda wa kukimbizana nae Bora nikae nisimamie biashara. Ila nitamkomesha tu ,nitamkomeshaga tu.
 
Asante mkuu. Ila huwezi mlazimisha mtu mzima kufanya majukumu yake.Mwenyewe babangu alikua na blabla kibao wakati wa kutoa matumizi na sijui anaendeleaje huko. Ila nikipata chochote siwezi msahau mamangu.

Watoto wanakua na wanaona. Huo muda wa kukimbizana nae Bora nikae nisimamie biashara. Ila nitamkomesha tu ,nitamkomeshaga tu.
Si rahisi mtoto wa Kike kwa baba. Unless aendelee kuwa mpuuzi baada ya mtoto kuvunja ungo. Nakueleza akiwa baba yake ni mjanja kama sie kwa watoto, humbandui kwa baba. Akiwa wa kiume hapo sawa. Nina mifano lukuki
 
Habari za weekend wapendwa,

I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.

Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.

Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.

Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.

So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.

Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.

Wanaume, nimewainulia mikono.

NB:Alitumia namba ngeni so nimemblock tena.Sitaki mazoea na mtu asiyejielewa.

Jumapili njema wapenzi.
Pole mkuu, kila jaribu huwa na mlango wa kuingia na kutokea. Hilo nalo litapita, just concentrate na mwanao huku ukisimamia ndoto zako.
 
Habari za weekend wapendwa,

I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.

Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.

Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.

Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.

So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.

Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.

Wanaume, nimewainulia mikono.

NB:Alitumia namba ngeni so nimemblock tena.Sitaki mazoea na mtu asiyejielewa.

Jumapili njema wapenzi.
Hii mada ilivyoanza nilifikiri naongelewa mimi!
 
Ushauri wangu

Fanya vyoyote utakavyofanya uhakikishe huyo baba anatoa matunzo yote ya mtoto hata ikibidi kumpeleka ustawi wa jamii au mahakamani mpeleke! Mathalan imethibitika mtoto ni wake, hana budi kumlea tena na hiyo miezi ambayo hajalipa andika kama deni na lazima alipe!

Kwanini nasema hivi?

Wewe na jamaa inawezekana mmegombana, lakini mtoto na baba yake hawajagombana. Utapambana mwenyewe apo kujidai kumlea mtoto, baadae mtoto akiwa mkubwa atakusumbua sana umpeleke kwa baba yake! Usipompeleka utajenga uhasama mkubwa na mtoto ambae umemtesekea wewe mwenyewe na atakuona mbaya! Ukija kumpeleka kwa baba yake baadae, na akagundua baba ana hela, atakulaumu sana kwa kumkosesha fursa katika maisha!! And trust me, huwezi kumtenganisha mtoto wa kike na baba yake, bora ata angekua wa kiume.

Ishu kama hii ilimtokea dada yangu, kapambana na mtoto saizi yuko chuo. Mtoto kamtafuta baba yake mpaka kampata na sasa hivi mtoto na baba lao moja, mama ndio anaonekana kituko!
Ndio maa a wengine huwaambia watoto wait baba walishakufa kuepuka masumbufu kama hayo,.
 
Mungu baba awabariki sana kina mama wote wanaolea watoto wao bila usaidizi wa baba zao..!!
Ni ushauri wangu kuwa suala la kuanzisha familia liwe mmekubaliana, vinginevyo hutokea misuguano kama hii hasa mwanaume asiyejua thamani ya ubinadamu na asiyethubutu kuvaa kiatu cha mzazi mwenzie.
 
Huwaga napata wakati mgumu kuhukumu story za upande mmoja......kila mmoja ana play victim......tunataka tusikie na upande wa pili......

Niliwahi kuletewa kesi kama hii na binti mmoja na nikawa mkali mpaka nikampeleka yule kijana police na ustawi wa jamii.....mpaka siku nilipooneshwa picha na video chafu za huyo mwanamke akifanya mapenzi na kijana mwingine.......tangu hapo nikawa makini na vilio vya wakina mama mpaka nisikie upande wa pili.......

NB;
Panapo fuka moshi, kuna moto chini.......
 
Ila huyo jamaa ni mjinga sana asee. Hata kama angekuwa hajaajiriwa mtoto wake anashindwa jichanga hata vi buku tano tano vya hapa na pale yani anapita neutral karibu miaka miwili?


Huyo kama hatumii bange basi yake ina loose connection, maana angekuwa timamu kwanza ujasiri wa kupiga simu na kuomba hela asingekuwa nao.
 
Back
Top Bottom