lady Jay
JF-Expert Member
- May 29, 2016
- 526
- 646
Habari za weekend wapendwa,
I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.
Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.
Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.
Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.
So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.
Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.
Wanaume, nimewainulia mikono.
NB:Alitumia namba ngeni so nimemblock tena.Sitaki mazoea na mtu asiyejielewa.
Jumapili njema wapenzi.
I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.
Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.
Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.
Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.
So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.
Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.
Wanaume, nimewainulia mikono.
NB:Alitumia namba ngeni so nimemblock tena.Sitaki mazoea na mtu asiyejielewa.
Jumapili njema wapenzi.