Mleta mada yote uliyosema kuhusu Mbowe hakuna anayeyapinga, lakini ukweli uko wazi kiongozi akiongoza zaidi ya miaka 10 anakuwa hana jipya, sana sana atatumia madaraka yake kusalia hapo madarakani na sio kwa ridhaa ya wanachama/wananchi wake. Mifano ya kwamba sasa Mbowe kafikia mwisho ni kitendo cha kumpokea Lowassa aliyefuata madaraka tu, na kisha kayakosa karudi kule kule alikotoka. Kama yuko kama kiongozi anapaswa kukabidhi kijiti kwa mwingine, lakini kama yuko hapo kama ajira basi muambie amechemsha.