Kwa kifupi, Askofu Gwajima anaweza kukataa kutoa vielelezo vyote polisi walivyovitaka pale anapoona na kuhisi haki zake za kimsingi na zile za kikatiba zinaingiliwa ama kutetereshwa bila ya sababu ya msingi.
Mfano halisi ni kuwa wito wa mahojiano yalikuwa juu ya kesi ya kumtukana au kumtolea maneno ya kashfa Askofu Pengo Vs.(dhidi) Rejea list ya vitu 10 (which is absolutely irrelevant) ambao ni uonevu wa wazi na ufinyangaji wa haki za raia.
Binafsi nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa kuona jinsi Wakili John Mallya alivyokuwa ana handle hii kesi, kwani katika uwanja wa sheria unapokuwa unamwakilisha mteja wako katika mahojiano ambayo ni sensintive kama ya Gwajima (ambayo yanaweza kuzaa kesi ya jinai), Wakili unapooona ama kuhisi mtiririko wa maswali yanaelekea nje ya tuhuma anayokabiliwa mteja wako (yaani to exploit your client constitutional rights) una haki ya kumwambia mteja wako asilijibu swali hilo. Na polisi kama wanaona wana haki wanachoweza kufanya ni kukupeleka mahakamani ambako sheria itapima kila mtu kwa usawa.
Hitimisho ni kuwa Gwajima ana haki ya kutopeleka hati yeyote ile ambayo anahisi hazihusiana na wito wa majhojiano juu ya tuhuma zilizojengwa mbele yake. Mwisho namshauri Gwajima kuwa imefika mahali sasa ajenge wigo mzito wa timu nzito ya Wanasheria, John Mallya naona kama hii kesi ni kama inamzidi kimo. Nafarijika kuona Mwanasheria mahiri na makini Peter Kibatala ameongezea nguvu na ameanzia na 'strategy' makini tu ya kuhoji uhalali. Na polisi wakileta ubabe unafungua shauri la kikatiba kuhoji mamlaka ya polisi juu ya kuitisha documents zote hizo katika tuhuma ya kumtukana mtu na tuone mahakama itatamka vipi.