palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,463
Leo wakili P.Kibatala amewakilisha rasmi barua jeshi la polisi kutaka ufafanuzi juu ya zile nyaraka muhimu
ambazo Gwajima anapaswa kuzipeleka wiki ijao. Jeshi la polisi limetakiwa kutoa kifungu cha sheria
kilichopelekea mteja wao aombwe nyaraka husika pamoja na tuhuma za matusi. Baaada ya kupata nyaraka
muhimu kutoka jeshi la polisi Gwajima anatarajia kuchukua hatua za kisheria.
ambazo Gwajima anapaswa kuzipeleka wiki ijao. Jeshi la polisi limetakiwa kutoa kifungu cha sheria
kilichopelekea mteja wao aombwe nyaraka husika pamoja na tuhuma za matusi. Baaada ya kupata nyaraka
muhimu kutoka jeshi la polisi Gwajima anatarajia kuchukua hatua za kisheria.
- Peter Kibatala : Bro Roma Roma Masu;wao watujibu kama tulivyoomba, na mengine yatafuata. Hatukuwaandikia kama mapambo. Tuna mpango mkakati utakaojumuisha kufungua cases za kikatiba week ijayo. Watujibu tu kama vile sisi ni wajinga, kisha tukutane nao High Court. Sisi tunataka barua/warrant/sijui nini rasmi inayotaja vifungu husika.
Peter Kibatala : WATUJIBU. Hilo tu. Me safari yangu ni High Court, the rest ni njia tu. Waniandikie na kuniambia 'Kibatala,wewe mzembe sana! ina maana hujui ni kifungu fulani na fulani cha sheria fulani kinatupa mamlaka hayo?'. Nanyi pia Mawakili wenzangu mnaruhusiwa kunitajia kifungu husika kinachowapa nguvu Police kumuhoji mtu kwa kosa la kutumia lugha ya matusi na kudai receipts za ununuzi na umiliki wa helicopter. Sheria ni ubunifu na si conformity
Kibatala: section 38 CPA inazungumzia searches. Hawa jamaa hawajam-search, wamemuamuru awasilishe nyaraka. Ni kifungu kipi kinawapa mamlaka hayo?
Kwa kifupi, Askofu Gwajima anaweza kukataa kuwapa vielelezo vyote au baadhi (kama anavyojisikia mwenyewe) kwa jeshi la polisi pale anapoona na ama kuhisi kuwa haki zake za kimsingi na ama za kikatiba zinaingiliwa ama kutetereshwa bila ya sababu ya msingi.
Mfano halisi: ni kuwa wito wa mahojiano ulikuwa juu ya kesi ya kumtukana au kumtolea maneno ya kashfa Askofu Pengo. Sasa tazama hii list ya vitu 10 inahusiana na nini? kama si uonevu wa wazi na ufinyangaji wa haki za raia. (which is absolutely irrelevant)
Binafsi nilianza kuwa na wasiwasi mkubwa kuona jinsi Wakili John Mallya alivyokuwa ana handle hii kesi, kwani katika uwanja wa sheria unapokuwa unamwakilisha mteja wako katika mahojiano ambayo ni sensintive kama ya Gwajima (ambayo yanaweza kuzaa kesi ya jinai mbaya kabisa), Wakili unapooona ama kuhisi mtiririko wa mahojiano yanaelekea nje ya tuhuma anayokabiliwa mteja wako (yaani to exploit your client constitutional rights) una haki ya kumwambia/shauri mteja wako asilijibu swali hilo tatanishi. Na ndio sababu kuu ya kuwa pale kwenye mahojiano. Na polisi kama wanaona wana haki wanachoweza kufanya ni kukupeleka mahakamani ambako sheria itapima kila mtu kwa usawa.
Hitimisho ni kuwa Gwajima ana haki ya kutopeleka hati yeyote ile ambayo anahisi hazihusiana na wito wa majhojiano juu ya tuhuma zilizojengwa mbele yake. Mwisho namshauri Gwajima kuwa imefika mahali sasa ajenge wigo mzito wa timu nzito ya Wanasheria, John Mallya naona kama hii kesi ni kama inamzidi kimo. Nafarijika kuona Mwanasheria mahiri na makini Peter Kibatala ameongezea nguvu na ameanzia na 'strategy' makini tu ya kuhoji uhalali. Na polisi wakileta ubabe unafungua shauri la kikatiba kuhoji mamlaka ya polisi juu ya kuitisha documents zote hizo katika tuhuma ya kumtukana mtu na tuone mahakama itatamka vipi.