Siku ya kwanza ya mahojiano magazeti yalireport mawakili watatu wa Gwajima akiwepo Kibatala na Neema kama sijakosea, kwahiyo kibatala hajaibuka tu, alikuwepo!! Nilimsikia Gwajima akisema wanaurafiki wa karibu na Dr Slaa, hii inaweza kuwa ndio sababu ya kutumia mawakili wa Chadema, maana nasikia Mallya naye ni wakili hatari sana anayechipukia ndani ya Chadema!!
Kwa mwenendo huu polisi wasilogwe kupeleka hii kesi mahakamani maana Tundu Lissu anaweza kuingia ndani na Mabere Marando hii kitu itafanya watanzania wote kwa ujumla wao wafungue macho na masikio yao kwenye hili sakata!!