Hatimaye ndugu yetu Pascal Mayala amehitimu UDSM

Kama kweli ni Paschal Mayalla tunayemfahamu mkumbuke alipata ajali mbaya sana ya pikipiki. Na hii ajali ilitokea kipindi akiwa ameshaanza shule yake hiyo. Hivyo ni lazima ATAKUWA aliahirisha Masomo. Nimpongeze kama ameweza kusoma tena baada ya ile ajali mbaya. Ni juhudi kubwa sana hii anahitaji kupongezwa na kila mwenye nia njema. Keep it up Paschal.
 
Wew una viwanda vingapi hadi sasa?
 
vyoyote itakavyokuwa, ila mimi kwa upande wangu watu wanaopenda sana kupoteza mda mwingi vyuoni kujiendeleza kielimu huwa nawachukulia kama wana matatizo fulani ya kisaikolojia. hawapo sawa wale. we wachunguze vizuri utabaini kitu.
Wazito kinyama afu wanavaa suruali pana za kitambaa na sendo zenye soli nene
 
Mtoto wa kiume kupigana mikwara na girl ni ushamba wa hali ya juu.
Mwanamke anabembelezwa au anakaushiwa,sio mikwara mikwara...Shubaaamit
Sasa mkuu unakuja kusema sema huku nyuma si ukwende hapo mbele hapo kwenye replay yake umwambie?
 
Embu nipe stori ya kilaza mmoja nimuonee huruma.
Kuna jamaa mmoja namfahamu mpaka anamaliza kidato cha nne hakuwahi kujua zile hesabu za decimals yan yeye kila akifundishwa anaulizia tu ile point au nukta ya kati inayotenga namba namba inafuata nini pale kwanini isitolewe na bado alikuwa kidogo zimo zimo kichwani vilaza Wengine nitakuelezea siku nyingine
 
Kongoletulation Mwanasheria Msomi Ndg. Pascal Mayalla kwa kuhitimu Shahada yako ( yawezekana Watu wanazungumza hapa bila kufahamu Vizingiti ulivyopita binafsi nimejaribu kuvaa Viatu vyako naona bado vimenibana kidogo sana ila "Kuzaliwa Familia Masikini ni Shida sana tena ni Mateso sana" . Pole kwa uliyopitia, Hongera kwa kuwa Ndoto yako imétimia.
 
Hongera sana Dkt.Pasko.

Nilidhani umesomea uandishi wa khabari kumbe wewe ni mwanasheria msomi
 
Ila nnavojua mimi hua kuna kikomo cha mda wa kuendelea na masomo baada ya kuahirisha au kurudia mitihani kwa ngazi ya bachelor degree au master degree ila kwa huo mda wa tangia 2003 na kumaliza mwaka huu hmm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…