Hatimaye na Mimi yamenikuta

Hatimaye na Mimi yamenikuta

Tafuta hela kijana hakuna haja ya kulilia mapenzi!

Kuchapiwa ? Kuna shida mahali,,,aidha humfikishi huyo mkeo ama huna hela kwa hio humtimizii mahitaji yake ,,, tatizo lipo Kwako !!!

Asilimia kubwa ya wanawake walioko kwenye ndoa wanachepuka kwa sbb zifuatazo;
Kutoridhishwa
Uchumi
Gubu/kutukujali n.k (hii sababu Ni Minor)

Wa kuiweka ndoa yako kwenye mstari ni wewe!
Wacha kulia lia hapa
Hujawahi kusikia mtoto wa tajiri ni mwizi?
 
Mbona hivo mnatukatisha tamaa sisi ambao hatujaoa, sometime muwe mnatupa mambo mazuri yanayopatikana kwenye ndoa na sio story ya kukatishana tamaa,
Mkuu ndoa ni tamu Sana. Ila Uvumilivu, maarifa na busara inatakiwa sababu changamoto ni nyingi. Hapa tunaelimishana na kupeana uzoefu. Na changamoto kubwa ya ndoa nyingi Kwa sasa ni michepuko. Hivyo Kama umeamua kuingia kwenye ndoa changa karata zako vizuri.
 
Uligunduaje anachepuka?? Kimsingi wanandoa wengi inaaminika wanachepuka wote wake kwa waume isipokuwa tu wanafanya kwa siri ila watu wapembeni wanajua ila hawakwambii na yeye pia hawamwambii. Hivyo ni kuomba tu usijue ukishajua uamue uendelee nae au utafute mwingine.

Nadhani huko majuu ndio maana kina will smith na mkewe wameruhusiana kila mmoja kutoka na mtu mwingine anaemtaka. Ni hulka ya binadamu kupenda kitu kipya na cha tofauti.

Kwa hali ya dunia inapoeleka ya utandawazi huko baadae ndoa zitakuwa chache sana au za mkataba.

Wewe tafuta mwingine maisha yaendelee wako zaidi ya bilioni 3.
Kupitia mawasiliano yake ( texts na voice calls) Mkuu sadly I was too late
 
Nawasalimu wote.
Nyie wanandoa aisee hebu heshimuni ndoa zenu.
Nimeoa miaka 5 Sasa juzi nimegundua wife anachepuka na Jamaa. Tena kirahisi rahisi tu. Huyu mwanamke nilikuwa Nampenda aisee, Ila kaniona Fala. Kinachoniuma zaidi sijawahi kuchepuka pamoja na vishawishi vyote navyokutana navyo Ila niliheshimu ndoa kinyama.

Daaah aiseee, Jamaa anaetembea nae nimemfahamu nae pia Kaoa, Sasa hapa nawaza sijui nikalale na mke wake halafu nifanye nae ujinga wote halafu nimtumie uchafu niliofanya na mke wake.

Kweli kuna watu hawana Akili Sasa unachepuka vipi na mke au mume wa MTU halafu na wewe ni mwanandoa? Halafu ukisikia mwenzako anachepuka unalalamika wakati wewe umelala au kulalwa na Mtu ambae analala au kulalwa na mwingine???

Hili Jambo limebadilisha kabisa mtazamo wangu Kwa wanawake na kitu inaitwa ndoa.

Mnaotaka kuoa hebu tafakarini mara mbili mbili Kwanza, Kama hamuwezi vumilia zinaa na mna roho ngumu oeni. Ila Kwa wale wanaoweza vumilia zinaa na hawana sababu za msingi za kuoa msijaribu hata Kidogo, narudia tena msijaribu.

Asilimia kubwa ya wanawake wanataka kuolewa ili kupata Ile heshima na title kwamba ni mke wa Mtu Ila deep down hawaelewi nini maana ya ndoa na ni nini Wana sacrifice wanapoingia katika ndoa.

Ila maamuzi niliyochukua ni kutengana na wife ninayempenda Ila ndio hivyo mapenzi hayalazimishwi pia umri wangu bado ni rika la 20's hivyo still bado takuwa na Mambo mengi ya kufanya.

Wife nishamsamehe na huyo jamaa waliefanyana nae shamsamehe nimemwachia Mungu sababu Kisasi ni cha Mungu na hata Yule mke wake nitamwonea tu.

Kuna Muda nasema Sasa wanawake watanikoma ni chapa ilale ha ha ha, daaah Ila deep down naona tawaonea tu kwa makosa ya Mtu mwingine.

Wenye ndoa ambazo hazina wachepukaji mshukuruni Sana Mungu Siku zote bila Kuchoka sababu msiba usikie tu Kwa jirani yako.

Huu mwaka nimeumaliza vibaya Ila naamini ni mwanzo mpya wenye nguvu na mwanga zaidi.

Mfurahie sikukuu hii ya Christmas.
Unaona wife wako kama umemuonea kumpuga kwa uzinzi, hata mimi ninakiri umemuonea.

Ndiyo maana umemuacha kishingo upande huku unajilaumu, roho inakusuta.

Ujue wengi wanaingia kwenye ndoa kwa madhumuni zaidi ya upendo ama ngono pekee.

Manufaa ya ndoa ni pamoja na kusaidiana mambo makubwa na madogo ya kimaisha, kupanuana akili na kushauriana, pamoja na kulindana nk nk.

Sasa mmoja wenu akikengeuka jambo flani mojawapo katika muunganiko wenu, yakupasa kurudi nyuma na kukaa naye chini kurekebisha dosari hiyo.

Mke ama mume haachwi kwa kosa moja, kama niivyo pasingekuwepo na ndoa za watu hadi kuzeeshana sasa!

Tayari hapo ulishauvaa uhakimu, umemuhukumu mwenzako saazingine kwa makosa yale yale unayopenda wewe kuyafanya.

Fikiria mara mbilimbili mrudie mkeo, kwa misukusuko ulompatia bila shaka atajirekebisha.
 
Nimekaa kwenye ndoa muda sasa nilichojifunza ni kuwa mke hukinaisha, na mume huchokwa, au kwa ufupi binadamu tunakinai.

Watoto, Busara, hofu ya MUNGU, hofu ya taswira yako katika jamii, upendo uliopo sababu ya kuzoeana baada ya kuishi miaka mingi pamoja na ukomavu wa akili ndio hushikilia ndoa.

Haya mambo ni nadra sana kuyapata kwa binadamu mwenye age ya 20's ndio maana haishauriwi kuwahi kuoa.
 
Unaona wife wako kama umemuonea kumpuga kwa uzinzi, hata mimi ninakiri umemuonea.

Ndiyo maana umemuacha kishingo upande huku unajilaumu, roho inakusuta.

Ujue wengi wanaingia kwenye ndoa kwa madhumuni zaidi ya upendo ama ngono pekee.

Manufaa ya ndoa ni pamoja na kusaidiana mambo makubwa na madogo ya kimaisha, kupanuana akili na kushauriana, pamoja na kulindana nk nk.

Sasa mmoja wenu akikengeuka jambo flani mojawapo katika muunganiko wenu, yakupasa kurudi nyuma na kukaa naye chini kurekebisha dosari hiyo.

Mke ama mume haachwi kwa kosa moja, kama niivyo pasingekuwepo na ndoa za watu hadi kuzeeshana sasa!

Tayari hapo ulishauvaa uhakimu, umemuhukumu mwenzako saazingine kwa makosa yale yale unayopenda wewe kuyafanya.

Fikiria mara mbilimbili mrudie mkeo, kwa misukusuko ulompatia bila shaka atajirekebisha.
Mwanamke akishazini ukathibitisha hafai tena kuwa mke. HUYU HAFAI TENA, HAKUNA NDOA HAPO HATA AKIMSAMEHE.

Wanawake waliopitia mafunzo kutoka kwa mabibi na mashangazi wanaelewa akili ya mwanaume linapokuja suala la fumanizi na ndio maana hata akichepuka hawezi ruhusu ijulikane kizembe.

Mwanamke yoyote mwenye akili na mkomavu wa nyonga na fikra, aliyepitia mafunzo ya matunzo ya mume hawezi kamatwa akizini.

Ikitokea akakamatwa kwenye hayo mazingira yanayopelekea kuhisi labda amezini huwezi thibitisha alikuwa akizini hata ww uliyelala naye huwezi thibitisha kirahisi kuwa umemlala.

Huyo ndo mwanamke aliyekuzwa akijua kuilinda ndoa yake na kulinda heshima ya mume wake, wana akili kubwa sana ya kupanga kuchepuka. Mazingira yote anaandaa yeye na huwezi mshika kizembe.

Hawa wa siku hizi hawakai na shangazi zao wanajifunza kwenye matv tu ndio maana wanafumaniwa fumaniwa tu. Siku hizi kutembea na mke wa mtu ukafumaniwa imekuwa rahisi sana.
 
Tafuta hela kijana hakuna haja ya kulilia mapenzi!

Kuchapiwa ? Kuna shida mahali,,,aidha humfikishi huyo mkeo ama huna hela kwa hio humtimizii mahitaji yake ,,, tatizo lipo Kwako !!!

Asilimia kubwa ya wanawake walioko kwenye ndoa wanachepuka kwa sbb zifuatazo;
Kutoridhishwa
Uchumi
Gubu/kutukujali n.k (hii sababu Ni Minor)

Wa kuiweka ndoa yako kwenye mstari ni wewe!
Wacha kulia lia hapa
Aliokwambia hela ni kama Solex kwenye chupi ya mkeo ni nani? Ukitaka usichapiwe tengeneza selo umfungie mkeo asitoke nje mpaka unaporudi toka mihangaikoni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom