Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Mwenyekiti wa chadema ameshaachiwa na sasa watu wamembeba juu juu Arusha

Haya mambo yanayofanywa na serikali pamoja na kutumia vyombo vyake vya usalama ni mambo ya aibu sanaa kwa nchi inayojigamba kuwa imekuwa katika mambo ya demokrasia!!! hizi ndiyo kero ambazo hata wakimpotezea Lowasa, Rostam na Chenge bado ni suala la kutwanga maji kwenye kinu maana watanzania waliowengi huichukia serikali kwa kero kama hizi.
 
Nakubaliana na wewe Mkuu, CCM hawasomi alama za nyakati, wanatumia vyombo vya dola wakidhani wanammaliza kisiasa CDM kumbe wanapandisha chati........Peoples'........!!!
 
Your analysis is short-sighted focusing on two days personal discomfort and lack long term strategic vision chances are your FISADI. THINK TWICE B4 YOU PRESENT your BS!!!!
 
waswahili tunasema utabaki na labda. CDM kuiona ikulu bado ni ndogo ya zuzu.

Asiyejua kwamba Watanzania walio wengi wameichoka CCM ndio yuko kwenye usingizi wa pono. Suala ni je CCM wataweza kuiba hela za umma kuwawezesha kuchakachua tena 2015 na je CDM wataweza kujipanga kulinda kura zao? Na jinsi mambo yanavyoenda CDM wako na advantage.
 
Wanadanganywa, wanadanganyika. ndio maana mara mgogoro uvccm na imara wanatumiwa na cdm kuvuruga amani.
kwani kabila kubwa la wakazi wa Arusha ni wafugaji.

Inabidi nawe ujiunge nao maana kichwa umejaza kamasi!
 


Mkuu hapa ni home of great thinkers , mie nilitegemea uje na takwimu useme hivi sasa CCM wana wanachama kadhaa, na cdm kadhaa, CUF kadhaa, sasa kusema wengi , wanaweza kuwa hata 1000 ni wengi pia. Ila fanya uchunguzi utakuta usemacho kwenye hali halisi sicho. Maneno yakujifariji hayo !
 
wakimaliza miaka mitano watakuwa hawana tena hamu ya kuongoza tz, sasa hivi wanaona aibu kuachia ila moyoni wanatamani sana kuachia ngazi
 
Ccm wamempiga teke chura wakifikiri wanamkomoa!.Wananchi wanazidi kupata mwanga zaidi kuwa nani yupo upande wao.
 

Napenda unijibu haya yafuatayo kwa ufasaha :
1. Kura zinaibwaje ?
2. Kura zinachakachuliwaje ?
3. Kura zinalindwaje ?
 
HIVI NGOJA NIULIZE, mbona Slaa alipoitwa mahakamani alienda bila tatizo? Kwa nini Mbowe hakwenda as required? Na kama alikuwa na jambo muhimu la kufanya,kwa nini mwanasheria wake hakutoa taarifa mapema?
 
Yapo kila Wilaya , na maji yake yanawasha balaa, ukimwagiwa yale maji hakuna la zaidi ya kukimbia tu. Na sio maji tu, jamaa wana silaha za kijeshi pia full masinonda kwa lolote. Hiyo ndio dola sasa
Dola inayotamka Bungeni (through PM) kuwa mafisadi wakiguswa nchi itasambaratika? hiyo sio dola hata kidogo ila kundi la matapeli.
 
wakimaliza miaka mitano watakuwa hawana tena hamu ya kuongoza tz, sasa hivi wanaona aibu kuachia ila moyoni wanatamani sana kuachia ngazi

Kumbe mna hamu na Ikulu, hilo sasa watanzania bado hawajawaruhusu, subirini labda 2050
 
wee unapimaje umaarufu,mbona alikua rumande sasa amepiganiaje hiyo haki,na kama ni hivyo kuwekwa rumande ndio umaarufu basi mch. mtikila ndie jembe zaidi kuliko yoyote tanzani.

Elewa topic kwanza mkuu...
Sijamfananisha na Mtikila, wala sijasema yeye ni maarufu kuliko mtu yeyote Tanzania
Unaelewa maana ya umaarufu?
Kuna watanzania wangapi leo wako rumande? au wanasafirishwa kwenda mahakamani? au wamesomewa mashitaka?
Naomba utumia kamusi yako kuangalia maana ya neno 'umaarufu'...
 
ili kodi inayokusanywa na ccm iende wapi? kama mmeshindwa kuongoza nchi si mkae pembeni we ndunya
 
huyu hakimu naomba nipate detail zake maana nina mtu nilisoma naye Kahunda sekondari (senegerema) mwaka 1996 the same name Charles Magessa kama ni huyo najua ana misimamo ya ajabu sana sijui kama ni yeye au la. pleaseeeeeeeeee kama kunamtu anamfahamu naomba anijulishe hapa.
 

Wengine tuko kwenye vita ya kuikomboa nchi yetu. Kulala sakafuni ni jambo la kawaida sana, tunalitegemea na tumeshalizoea. Ukishavaa kombat huwezi ogopa kulala sakafuni. Heshima unaipata kwa watu wanaokuheshimu. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kukojolewa na kichaa na kukojolewa na mtu mwenye akili timamu analujua analolifanya. Na kwa taarifa yako CCM inahusika sana na hili jambo kwa kuingilia kazi za mahakama. Order ya kukamatwa Mbowe imetoka Lumumba.
 
wee unapimaje umaarufu,mbona alikua rumande sasa amepiganiaje hiyo haki,na kama ni hivyo kuwekwa rumande ndio umaarufu basi mch. mtikila ndie jembe zaidi kuliko yoyote tanzani.

:help::help:
 
waswahili tunasema utabaki na labda. CDM kuiona ikulu bado ni ndogo ya zuzu.

Nafikiri ni ndoto ya zuzu kwa CCM kushinda uchaguzi, na ni ndoto ya zuzu kwa CDM kutangazwa washindi. Ila mwisho wa CCM kung'ang'ania madaraka kwa mtutu wa bunduki haupo mbali. Ni nani aliamini Mubarak na chama chake leo hii wangekuwa powerless baada ya kujitangazia ushindi wa bunge kwa 90%?. Sooner or later mabadiliko makubwa ya uongozi yatafanyika Tanzania kwani mamlaka hutoka kwa wananchi na si kwenye umiliki wa maghala ya silaha.

Ni mwendawazimu pekee kuwa na mawazo kuwa upinzani Tanzania hauwezi kuongoza nchi. CCM inaweza kuzifanya ndoto hizi za upinzani kushindwa kuwa za kweli kwa kuhakikisha kuwa 90% ya vijana wana ajira zinazowaingizia kipato cha kukidhi mahitaji ya siku 30 kwa mwezi na ziada ya siku 15. Kuhakikisha rushwa imeisha Tanzania, kuhakikisha uchumi umekua, kujenga miundombinu, kuhakikisha usalama wa raia ni priority, kuondoa uonevu wa vyombo vya dola dhidi ya raia, kupatikana katiba mpya iliyotokana na wananchi. Haya yote yakifanyika siyo tu CCM inabaki madarakani bali itakuwa pia ni oneway ticket out of power. Watanzania wanahitaji kitu kipya na hilo halikwepeki. Ni nature tu, tena kitu kizuri ni kwamba hizi nguvu za ziada za dola zinazotumika sasa dhidi ya raia ni kama training ya uvumilivu na kuongeza ujasiri, the more they do the more people's fear will disappear.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…