Hatimaye Kikwete amsamehe Deus Mallya...

Hatimaye Kikwete amsamehe Deus Mallya...

Sajenti

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2008
Posts
3,651
Reaction score
414
Katika kuadhimisha miaka 46 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alitoa msamaha kwa wafungwa 3,101. Katika msamaha huo yumo kijana Deus Mallya aliyeshitakiwa kwa kosa la kuendesha gari kwa uzembe na bila ya kuwa na leseni na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha aliyekuwa Makamu mwenyekiti wa CHADEMA marehemu Chacha Wangwe. Ajali hiyo ilitokea katika eneo la panda mbili katika mkoa wa Dodoma........
 
Huenda yaliyosemwa yalikuwa ya kweli, prof. Lipumba aliwahi kunukuliwa akisema Deus mallya ni shu shu shu na alipata mafunzo yake Libya. Kwa hiyo huenda alitumika kutekeleza kazi maalumu ya serikali.
 
Huenda yaliyosemwa yalikuwa ya kweli, prof. Lipumba aliwahi kunukuliwa akisema Deus mallya ni shu shu shu na alipata mafunzo yake Libya. Kwa hiyo huenda alitumika kutekeleza kazi maalumu ya serikali.

Ukisema hivi inamaanisha kifo cha Chacha Wangwe kilipangwa ???
 
Na yeye siku yake ya kukufa si ipo jamani. hataishi milele
 
Msamaha kwa mtu aliyesababisha ajali na kuua public figure anasamehewa kirahisirahisi tu?...Imekwendakwendaje hii?..Mbona walisema msamaha unawahusu Wagonjwa wa Ukimwi na TB, na vitu vya namna hiyo?
 
Na yeye siku yake ya kukufa si ipo jamani. hataishi milele
cha kuchekesha kipo hapa je ni kikwete anayependekeza majina ya wasamehewa au nani.. mbona hizi link huwa zinakera je kosa la kuendesha gari na kusababisha ajali iliyoua si kosa dogo tu la traffic? Mbona tunasema tu bila kujua hasa hizi sheria zinasemaje na nani hasa anahusika na mipangilio. Hili huwa linatyupa sana watanzania. kwa kawaida wanaosamehewa ni wale wenye makosa ya kipuuzi na wagonjwa je kosa la trafic si la kipuuzi na kama shushushu kafanya kazi yake ilikuwaje wahangaike vile?: Serikali huua ndio lakini wako very niti katika hili na kama unabisha soma falsafa za mauaji na conspiracy zake
 
nilikuwa nje ya mtandao duh haya mabadiliko yako very unfriendly. sipendi JF huo ndio ukweli inanisumbua haya marangirangi yenu mfumo ahh yaani ulijiondoa hewani kufix vitu au ulijiondoa hewa kunikera. mhh nilikuwa nafikiri tu.
 
nilikuwa nje ya mtandao duh haya mabadiliko yako very unfriendly. sipendi JF huo ndio ukweli inanisumbua haya marangirangi yenu mfumo ahh yaani ulijiondoa hewani kufix vitu au ulijiondoa hewa kunikera. mhh nilikuwa nafikiri tu.

Mkuu mbona umetoka nje ya mada?
Au umepotea njia!!
 
cha kuchekesha kipo hapa je ni kikwete anayependekeza majina ya wasamehewa au nani.. mbona hizi link huwa zinakera je kosa la kuendesha gari na kusababisha ajali iliyoua si kosa dogo tu la traffic? Mbona tunasema tu bila kujua hasa hizi sheria zinasemaje na nani hasa anahusika na mipangilio. Hili huwa linatyupa sana watanzania. kwa kawaida wanaosamehewa ni wale wenye makosa ya kipuuzi na wagonjwa je kosa la trafic si la kipuuzi na kama shushushu kafanya kazi yake ilikuwaje wahangaike vile?: Serikali huua ndio lakini wako very niti katika hili na kama unabisha soma falsafa za mauaji na conspiracy zake

Mkuu utakuwa umetumwa??

nilikuwa nje ya mtandao duh haya mabadiliko yako very unfriendly. sipendi JF huo ndio ukweli inanisumbua haya marangirangi yenu mfumo ahh yaani ulijiondoa hewani kufix vitu au ulijiondoa hewa kunikera. mhh nilikuwa nafikiri tu.

Sasa wewe ndo unatukera bora upotee kabisaaaaa.....nitamshutua mode akubani
 
tatizo nchi hii ina mambo mengi sana..yaliyomo na yasiyokuwemo ....mbona kina nanihii hawajasamehewa basi??
 
Msamaha kwa mtu aliyesababisha ajali na kuua public figure anasamehewa kirahisirahisi tu?...Imekwendakwendaje hii?..Mbona walisema msamaha unawahusu Wagonjwa wa Ukimwi na TB, na vitu vya namna hiyo?
...Mkuu si unajua hii ni bongo kila kitu kinawezekana. Kwni kuna tabu gani kama hao walioko kwenye parol board wakiambiwa watengeneze mazingira kuwa Deus ni mgonjwa wa TB au muathirika wa HIV ili atoke?? Sishangai sana....Haya ni mambo ya chekundu cheusi ukiokota cheupe umeliwa bana...!!
 
Hii ni skendo, wala si jambo dogo. Wanajua wanachokifanya.
 
Upuuzi mtupu, kama ni shushu kweli walishindwa kumtafutia LESENI???? Acheni uzushi nyie ndio mnaipausha JF mpaka kinaonekana ni KIJIWE cha waliokosa kazi, JK kawasamehe wafungwa kwa tatratibu zilizopo na sio kwa majina, ebooooo
 
cha kuchekesha kipo hapa je ni kikwete anayependekeza majina ya wasamehewa au nani.. mbona hizi link huwa zinakera je kosa la kuendesha gari na kusababisha ajali iliyoua si kosa dogo tu la traffic? Mbona tunasema tu bila kujua hasa hizi sheria zinasemaje na nani hasa anahusika na mipangilio. Hili huwa linatyupa sana watanzania. kwa kawaida wanaosamehewa ni wale wenye makosa ya kipuuzi na wagonjwa je kosa la trafic si la kipuuzi na kama shushushu kafanya kazi yake ilikuwaje wahangaike vile?: Serikali huua ndio lakini wako very niti katika hili na kama unabisha soma falsafa za mauaji na conspiracy zake

Mkuu vipi ya Gen. Imrani Kombe kwani ilikuwaje?
 
Upuuzi mtupu, kama ni shushu kweli walishindwa kumtafutia LESENI???? Acheni uzushi nyie ndio mnaipausha JF mpaka kinaonekana ni KIJIWE cha waliokosa kazi, JK kawasamehe wafungwa kwa tatratibu zilizopo na sio kwa majina, ebooooo

Mkuu hayaja kukuta lakini kama ungeisha ondokewa na mpendwa wako ktk mazingira ya kutatanisha yanayo acha maswali basi usingelisema hayo unayosema sasa. Omba Mungu tu akuepushe na mkono wa dola, huwa ni mrefu sana na mgumu huwezi kuukata hata kwa gesi.
 
Back
Top Bottom