Hatimaye JK akabidhiwa ripoti ya madini

Hatimaye JK akabidhiwa ripoti ya madini

So, JF members are not interested in this, are they? Some mining outfit plays police in an otherwise peaceful village in Tanzania, and that does not attract the attention of JF members?

Where are you Mwafrika wa Kike? It’s your thread, remember? There was plenty of activity around here when it was rumored that Mzee Mwanakijiji had developed some soft spot towards you. Is this thing of trigger happy guards arresting villagers, for “trespassing” on the villagers’ own land, not a whole lot more interesting to you, and even to Mzee Mwanakijiji?

Come on guys, your silence on this is deafening!

Mwalimu Moshi,

Samahani sana kwa kutoiona hii on time maana kila ijumaa jioni mimi huchukua off (kwenda kwenye faculty day ya ikibinda nkoi pale mwenge...lol) na kurudi jumatatu.

Niliahidiwa kuwa hii report itatoka mwisho wa mwezi na kwa vile leo ni mwisho wa mwezi wa tatu (mwaka 2008 to be specific) basi tutegemee kuona kina Zitto wamefanya nini katika hili.

Sio kwamba nimepuuzia hiyo story yako, nilijaribu kusubiri kidogo (na hata nilisema hapa) ili niweze kuwa na basis ya kutoa opinion yangu.

Kwa sasa nadhani kila kitu kiko mezani na hii habari yako ya majambazi na uporaji wao sasa itakuwa ajenda namba moja kwenye hii story!

Samahani na asante kwa kunikumbusha hili.

Asante!
 
Kamati ya Madini ilipewa muda gani naona time is up longtime kama alivyosema bi mdogo hapa. Sasa, tuambiane yameishia wapi..
 
Kamati ya Madini ilipewa muda gani naona time is up longtime kama alivyosema bi mdogo hapa. Sasa, tuambiane yameishia wapi..

Muda waliopewa wali ulishamalizika, lakini kwa kuwa walikuwa hawajamaliza kazi, wakaomba kuongezewa muda na JK akawapa hadi kati kati ya Aprili. Kwa taarifa nilizonazo, ripoti inakaribia kukamilika na mipango iliyopo ni ikabidhiwe kwa rais kabla ya Aprili 10.
Time is almost up, sijui tutaona usanii mwingine?
 
sasa sijui wataiweka hadharani au hadi Rais aamue kwanza..?

Hii ni tume/kamati/mkutano wa watu/weka jina lolote utakalo/wrver ya raisi kwa hiyo itafanya kazi kwa ridhaa yake. Na so far yeye ndiye ataamua nini kifanyike kwenye report hii (as far as I know).
 
Muda waliopewa wali ulishamalizika, lakini kwa kuwa walikuwa hawajamaliza kazi, wakaomba kuongezewa muda na JK akawapa hadi kati kati ya Aprili. Kwa taarifa nilizonazo, ripoti inakaribia kukamilika na mipango iliyopo ni ikabidhiwe kwa rais kabla ya Aprili 10.
Time is almost up, sijui tutaona usanii mwingine?

Mbona haya ya kuongezewa muda yafanyike chini kwa chini? au ndiyo yaleyale ya kusaini mkataba wa Buzwagi hotelini?
 
Ni kwamba kamati ikishatoa taarifa yake kwa Rais, basi Rais ataunda kamati nyingine ya kuaangalia hiyo taarifa na kumwambia inasema nini na afanye nini. Ndio mtindo walio nao hawa "wenzetu".

Wakati haya yote yakiendelea, walafi wanachimba madini kwa kasi kubwa. Kwa nini Rais hawaambii wasitishe uchimbaji kwanza mpaka kieleweke?

Kwa sasa, Kamishina wa Madini anatakiwa atoe tamko la kusitisha uchimbaji mpaka akague usalama wa migodi yote kwanza. Hawapashwi kuendelea kuchimba tu wakati hakuna hata uhakika kwamba wameweka vizuio vya maji ya mvua. Fikiria Watanzania wako kwenye mashimo ardhini wakati hata kitu kidogo cha kuzuia maji ya mvua yanayotiririka yasiingie hakipo!

Nasema wasitishe mpaka kieleweke kwanza!
 
Augustine Moshi ,

Lakini mambo yote haya si yalifanywa na Mkapa . Kiongozi ambaye ulishawahi kusema ya kuwa alikuwa rais wa bora wa Tanzania tangu tupate uhuru .
 
Rufiji, naona unanitoa nje ya Dar es Salaam kidogo. Inaelekea Mkapa alikuwa na ulafi sana wa mali, lakini alijenga uchumi zaidi ya waliomtangulia na waliomfuatia. Kuna viongozi corrupt (eg Suharto wa Indonesia) ambao pamoja na mapungufu yao, wanajenga sana uchumi. Mkapa ni wa aina hiyo.

Mkapa alipokea uchumi wenye kasi ya mfumuko wa bei ya 30%. Miaka kumi baadaye alikabidhi uchumi ambao kasi yake ya mfumuko wa bei ilishashuka hadi 4.5% kwa mwaka!

Mkapa alifanikiwa kuondoa deficits kwenye bajeti yetu. Mkapa alileta mapinduzi makuu kwenye civil service, alijenga madaraja na mabarabara, alianzisha mapinduzi makubwa kwenye Elimu, alianza ukarabati wa hospitali zote za serikali, etc. etc.

Lazima niongezee kwamba Mkapa alikuta jeshi (JWTZ) linalovaa viraka akawanunulia nguo na magari. Wote tuliona.

Mkapa hakuwa malaika. Alizalisha sana mali lakini akachota hapo kidogo vile vile. Sina shaka kwamba kama Mkapa angekuwa bado Rais, barabara ya Mtwara hadi Mwanza ingeshamalizika, kasi ya mfumko wa bei kwa sasa ingekuwa kwenye 2.5%, etc. etc.

Baada ya kukurudishia, anomba turudi kwenye mada.
 
Modes hii thread kwanini isiunganishwe na ile ya countdown kamati ya madini ya m.wa kike?
 
Nilianzisha thread iliyokuwa ikiuliza kama Zitto atasimamia yale aliyokuwa akiyapigania kule bungeni ambapo walimsuspend lakini Kikwete kwa kufuta makosa ya CCM ambayo inaliendesha bunge akampa pole na sasa tunataka matokeo ya pole hiyo!
 
Rufiji, naona unanitoa nje ya Dar es Salaam kidogo. Inaelekea Mkapa alikuwa na ulafi sana wa mali, lakini alijenga uchumi zaidi ya waliomtangulia na waliomfuatia. Kuna viongozi corrupt (eg Suharto wa Indonesia) ambao pamoja na mapungufu yao, wanajenga sana uchumi. Mkapa ni wa aina hiyo.

Mkapa alipokea uchumi wenye kasi ya mfumuko wa bei ya 30%. Miaka kumi baadaye alikabidhi uchumi ambao kasi yake ya mfumuko wa bei ilishashuka hadi 4.5% kwa mwaka!

Mkapa alifanikiwa kuondoa deficits kwenye bajeti yetu. Mkapa alileta mapinduzi makuu kwenye civil service, alijenga madaraja na mabarabara, alianzisha mapinduzi makubwa kwenye Elimu, alianza ukarabati wa hospitali zote za serikali, etc. etc.

Lazima niongezee kwamba Mkapa alikuta jeshi (JWTZ) linalovaa viraka akawanunulia nguo na magari. Wote tuliona.

Mkapa hakuwa malaika. Alizalisha sana mali lakini akachota hapo kidogo vile vile. Sina shaka kwamba kama Mkapa angekuwa bado Rais, barabara ya Mtwara hadi Mwanza ingeshamalizika, kasi ya mfumko wa bei kwa sasa ingekuwa kwenye 2.5%, etc. etc.

Baada ya kukurudishia, anomba turudi kwenye mada.

Vema sana kuturidisha nyuma na kuonyesha mazuri yaliyofanywa na kutabiri angefanya nini kama angeendelea kuwa kiongozi wa nchi.
Lakini ndugu yangu, unachofanya haoa ni kuionyesha mazuri ya Mkapa ay udhaifu wa serikali iliyopo madarakani? Kwani katika maneno yako, kwa ulinganifu, unaonyesha jinsi ambavyo serikali ya sasa ilivyoshindwa kufikia 'rekodi' za Mkapa
 
Augustine Moshi , ni kweli kwamba Mkapa alifanya baadhi ya mambo mazuri ila kama mtu ukifanya comparison ya mazuri na mbaya na long term effect ya vitendo vyake basi utaona ya kuwa mabaya yake ni mengi kuliko mazuri . Ni lazima tutambue ya kuwa kama mikataba ya migodi yetu ingekuwa imetengenezwa kwa lengo la kuboresha maisha ya mtanzania na sio matumbo ya Mkapa na Yona hela zile zingetsosha kabisa kujenga hata barabara kumi unazozingumzia.

Mkapa alifanya mambo mengi mazuri alipoingia madarakani na wataalamu wengi wa mambo watakubali ya kuwa aliyefanya haya mambo behind the scenes alikuwa Nyerere. Wakati Nyerere alipokuwa hai serikali ya Mkapa ilikuwa effective kweli kweli lakini mara baada ya huyu mzee kufariki mambo yalibadilika...kwa hiyo mimi nadhani mtu wa kupewa credit ni Nyerere na sio Mkapa na serikali yake.
 
Yaani Rufiji unanishangaza. Unataka kusema Mwalimu aliaacha kujenga daraja lako miaka 24 yote aliyokuwa madarakani akisubiri alijenge wakati wa Mkapa? Na mbona hakulijenga wakati wa Mwinyi?

Kwa taarifa yako, Mwalimu hakujali kabisa usafiri wa Kusini. Na aliona Kusini ni kama jela, ndio maana alimsukumiza Kasanga Tumbo huko kwa miaka kumi, kama adhabu.

Unataka kusema Mwalimu aliacha tukose hata sabuni ya kuogea, akisubiri ajenge supermarkets wakati wa Mkapa? Mtu aliyesema kukosekana vitu madukani ni matokeo ya maendeleo unathubutu kumlinganisha na Mkapa? Unamkosea sana haki Mkapa.

Mwalimu alikataza watu wa Sumbawanga kuuza mahindi yao nje. Wakati huo huo akawanyima barabara ya kuyaleta Dar, yakabaki yanawaozea tu. Mkapa alikwenda huko akawaruhusu kuyauza kwa yoyote yule. Wewe utasema ni Mwalimu aliwakomboa? Usidanganye.

Mwalimu alipokea nchi iliyokuwa inatumia 20% ya bajeti kwenye Elimu. Alianza kubomoa Elimu kwa matendo, na kwa kuinyima fedha, na kufikia wakati anaondoka madarakani, alishashusha bajeti ya Elimu hadi kufikia asilimia 4.9 tu ya bajeti yote.

Mwalimu aliua shule nzuri kama St. Francis (Pugu), St. Andrew's (Minaki), Miriam College (Kilakala), Assumption College (Weru Weru), etc. Baya zaidi ni kwamba alikataza kabisa kuanzishwa kwa shule nyingine kama hizo.

Mwalimu huyo huyo ndiye aliwafundisha akina Malecela, na CCM kwa ujumla, namna ya kuiba kura. Hilo bado linatutesa.

Labda Mwalimu alikuwa na nia nzuri, lakini ukweli ni kwamba aliturudisha nyuma sana. Si haki useme kazi nzuri za Mkapa ni kazi za Mwalimu.
 
Inapokuja swala la Mkapa, Augustine Moshi is the worst person to discuss anything with.
Sina hakika kama huwa ni yeye mwenyewe, ndugu yake au ni kitu gani. Lakini jamaa ana aina ya upofu unaomfanya anaona Mkapa kama malaika fulani hivi. Hata kama angefanya ukichaa wa ajabu namna gani, Moshi atakwambia he's the best. Ni ngumu sana kumjadili Mkapa na huyu Bwana tangu zamani Moshi ni Mkap, Mkapa, Mkapa no matter what's the agenda. Kwa kweli sio siri inafika point inaboa. Inahitaji kuwa na kichaa fulani kushindwa kuelewa ubaradhuri alioufanya Mkapa kwenye nchi hii.
 
Jim ,

Nakubalina na wewe kabisa , Augustine Moshi ameonyesha na anazidi kudhihirisha ubias wake inapokuja kwenye ishu ya Mkapa. Aingii akilini kwa mtu kusema ya kuwa Mkapa ameleta maendeleo ya ajabu wakati ukweli ni kuwa Mkapa ametumbukiza nchi yetu kwenye umasikini wa ajabu. Hivi kweli tunaweza kukaa hapa na kusema inflation ilishuka kwa kiasi fulani wakati hata hatujui ni vigezo walivyotumia kupata hiyo figure ?

Vile vile ni lazima tutambue ya kuwa hizo figure zinakuwa cooked na BOT , Jee tutawezaje kutathmini ukweli wa hizo figure ambazo zinatolewa na kina Balali ? Pili huwezi ukasema ya kuwa Nyerere akuhusika na success ya awamu ya kwanza ya Mkapa, ni lazima tutambue ya kuwa kama isingekuwa Nyerere ...mkapa singekuwa rais wa Tanzania . Kwa hiyo JK ndiye aliyemshika mkono na kumpa strategy za jinsi ya kurevamp masuala ya uchumi. Mimi napinga argument ya kusema kwa kuwa simply mtu alifanya makosa fulani hawezi kuyarectify in future.

Mwisho , ni lazima tutambue ya kuwa kama ile mikataba ingeweka manufaa ya mtanzania mbele basi nchi yetu ingeweza kupiga hatua sana . Lakini huyo bwana uchumi unayemsema wewe akujali hilo bali alijali tumbo lake ! Angalia nchi nyingi duniani wanavyotumia rasilimali zao vizuri katika kujenga nchi yao . Moshi angali jinsi Mkapa alichofanya pale bandari Dar es Salaam, pamoja na kwamba wataalamu walimwambia ya kuwa TSCAN kampuni ya Karamagi imetia serikali hasara yeye aliextend muda wa mkataba kwa miaka 10 zaidi....
 
Jim ,

Nakubalina na wewe kabisa , Augustine Moshi ameonyesha na anazidi kudhihirisha ubias wake inapokuja kwenye ishu ya Mkapa. Aingii akilini kwa mtu kusema ya kuwa Mkapa ameleta maendeleo ya ajabu wakati ukweli ni kuwa Mkapa ametumbukiza nchi yetu kwenye umasikini wa ajabu. Hivi kweli tunaweza kukaa hapa na kusema inflation ilishuka kwa kiasi fulani wakati hata hatujui ni vigezo walivyotumia kupata hiyo figure ?

Vile vile ni lazima tutambue ya kuwa hizo figure zinakuwa cooked na BOT , Jee tutawezaje kutathmini ukweli wa hizo figure ambazo zinatolewa na kina Balali ? Pili huwezi ukasema ya kuwa Nyerere akuhusika na success ya awamu ya kwanza ya Mkapa, ni lazima tutambue ya kuwa kama isingekuwa Nyerere ...mkapa singekuwa rais wa Tanzania . Kwa hiyo JK ndiye aliyemshika mkono na kumpa strategy za jinsi ya kurevamp masuala ya uchumi. Mimi napinga argument ya kusema kwa kuwa simply mtu alifanya makosa fulani hawezi kuyarectify in future.

Mwisho , ni lazima tutambue ya kuwa kama ile mikataba ingeweka manufaa ya mtanzania mbele basi nchi yetu ingeweza kupiga hatua sana . Lakini huyo bwana uchumi unayemsema wewe akujali hilo bali alijali tumbo lake ! Angalia nchi nyingi duniani wanavyotumia rasilimali zao vizuri katika kujenga nchi yao . Moshi angali jinsi Mkapa alichofanya pale bandari Dar es Salaam, pamoja na kwamba wataalamu walimwambia ya kuwa TSCAN kampuni ya Karamagi imetia serikali hasara yeye aliextend muda wa mkataba kwa miaka 10 zaidi....
Tunasikilizia ripoti tu..we're still around!Tunataka kuona whats going,what went on and ofcourse what should be done!
 
Ni kwamba kamati ikishatoa taarifa yake kwa Rais, basi Rais ataunda kamati nyingine ya kuaangalia hiyo taarifa na kumwambia inasema nini na afanye nini. Ndio mtindo walio nao hawa "wenzetu".

Wakati haya yote yakiendelea, walafi wanachimba madini kwa kasi kubwa. Kwa nini Rais hawaambii wasitishe uchimbaji kwanza mpaka kieleweke?

Kwa sasa, Kamishina wa Madini anatakiwa atoe tamko la kusitisha uchimbaji mpaka akague usalama wa migodi yote kwanza. Hawapashwi kuendelea kuchimba tu wakati hakuna hata uhakika kwamba wameweka vizuio vya maji ya mvua. Fikiria Watanzania wako kwenye mashimo ardhini wakati hata kitu kidogo cha kuzuia maji ya mvua yanayotiririka yasiingie hakipo!

Nasema wasitishe mpaka kieleweke kwanza!
Kwasababu Mh Rais mwenyewe ameshakubali kuwa mikataba ni mibovu na kinyonyaji..kwanini asisitishe huo uchimbaji/mikataba iliyopita hadi hapo hiyo kamati itakapotoa taarifa na mapendekezo?
 
Kwasababu Mh Rais mwenyewe ameshakubali kuwa mikataba ni mibovu na kinyonyaji..kwanini asisitishe huo uchimbaji/mikataba iliyopita hadi hapo hiyo kamati itakapotoa taarifa na mapendekezo?

Kikwete anajiweka kwenye nafasi ya kushitakiwa kutimiza kazi zake akiwa kama amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa Tanzania.

Kama haya madini sio ulinzi na usalama wa Tanzania, then sijui nini tena kinafit hiyo tafsiri!
 
Back
Top Bottom