Hatimaye fedha kurudi mitaani

Haishangazi kuona wahitimu wenye kiwango cha chini wakiongezeka kama wahadhiri wenyewe ndio wenye uelewa huu!
 
Haishangazi kuona wahitimu wenye kiwango cha chini wakiongezeka kama wahadhiri wenyewe ndio wenye uelewa huu!
Utafikiri tumelaaniwa, huyu kesho unaweza kumkuta Tanesco. Hajui mbele ni wapi na nyuma ni wapi?
 
Zilienda wapi? Kwa hiyo serikali ikikopa katika mabenki ya ndani pesa inarudi mtaani, yaani Ph.D zingine hizi!
 
Afu mbna maana ya serikal kukopa benk za ndan wanamaanisha ni kupunguza hela mtaan sasa huyu mtaalamu vp
 
Halafu nipashe nayo imekuwa ya hovyo sana.Nao waandishi wanandika huu ujinga.Sasa kwanini hela ikopeshwe serikali kwanza na si wananchi directly?
 
Sijui itaanza lini,mfukoni jua kali balaaa!!!
Serikali inakudalalia imekopa kwa niaba yako kama vile wewe huwezi fika bank.Oh.Hapana inapigana vikumbo na wewe kupata kiasi kidogo cha mkopo wa bank.Serikali ilipofunga account ikatumbua hela na kufulia.
 
Waliziondoa pesa za serikali bank binafsi wakidai kuwa bank zimekuwa zikitumia pesa za serikali kuikopesha serikali. Kwa maana kuwa serikali ilikuwa inajikopesha yenyewe huku bank ndiyo zinapata faida.

Sasa hii ya kuishiwa na kwenda kukopa tena huko inaleta picha gani!?

Wachumi tufafanulieni!
 
Vigeregere basi jamani ....... !!! mbona kimya na hela mmerudishiwa ?

Erythrocyte;
Vigeregere au vilio?? Hakika mwaka huu, tutanyooka tu. Baada ya kuwanyang'anya zile pesa serekali ilikuwa inaziweka fixed account kwenye mabenk binafsi ili yayumbe wakaona bado majamaa yamekomaa kichizi. Sasa wamekuja na mbinu mbadala, kuwanyang'anya hiyo mitaji yao wananchi wayarudishe hazina wakayaweke kule BoT. Haya jamani. Tungojee muziki munene very very soon. Kama nje sasa tumewekwa kwenye lile kundi la wasiokopesheka, tutegemee nini??
Namuunga mkono Mh. Rais, Serekali haina shamba, hivyo haigawi vyakula. Nendeni mkalime mihogo huko Jyang'ombe mle msitegemee chakura cha bure. Tafuteni mitaji hukooo wala msitegemee mikopo ya bank. Serekali haitapasua kichwa kumbe mihela kichele imekaa kwenye mabenk hapa hapa nchini.
 
Serikali inakudalalia imekopa kwa niaba yako kama vile wewe huwezi fika bank.Oh.Hapana inapigana vikumbo na wewe kupata kiasi kidogo cha mkopo wa bank.Serikali ilipofunga account ikatumbua hela na kufulia.
Unaambiwa hata ule uongo wa mapato ya TRA ya kila mwezi kimyaaaaaa !!!!
 
Naona bwana Ngosha ameshaishiwa sasa ...!!! Makusanyo yote hayo ya TRA..?! Kubana kote matumizi..?!

Nasikia BOT inawahudumia watu wa Chato pekee, mpaka waseme poo...!!

Kweli nyumban ni nyumban mtan wangu, Chato oyeeeeeee......!!
 
Kunawakati wasomi wetu ni janga kuliko kawaida wasomi badala ya kupeleka ushauri namna ya kunusuru uchumi anashangilia serikali kukopa

Elimu haina mwisho ila mawazo ya binadamu yana ukomo nae huyu msomi wetu mawazo yake ndo yalipo ishia

Serikali kuanza kukopa kutoka benki za ndani hakutaleta afueni kwa mzunguko wa fedha nchini kwasababu ukopaji huo wa serikali utafanya wale wa secta binafsi wapate shida sana kupata mikopo!!!! It is the private sector that takes loans from banks and invests and it is through these investments that money circulation increases in the economy; government borrowing from commercial banks crowds out the private sector from accessing loans and it is not good for the growth of the economy!!
 
Wanazikomba zote wanazitoa benki binafsi na kuzipeleka benki kuu.

Unaweza kukuta wanazikusanya kuzipeleka kwa vitoto vya kizungu vyenye kampuni ya bombadia na Boeing huko marekani na kanada

Upande wa pili mabenki yamegoma kukopesha wafanyakazi,na wafanyabiashara wanakopeshwa kiduchu

Mabenki yataacha kukopesha wamama wa tandale na manzese ambao hawaaminiki,watasubiri kuikopesha serikali,nayo ikishakopa inazikimbiza mbio benki kuu

Baadae serikali wataanza kukopa kwenye viccoba na saccos
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…