CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,984
- 4,083
Mhe. David Kafulila akimkabidhi Katiba ya JMT Mkuu Mpya wa Mkoa Mh. Dkt Yahya Mawanda kama nyenzo yake ya kufanyia maamuzi
Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mh. David Kafulila amesema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi ya utekelezaji wa bajeti ya maji ya miaka ishirini (20) mfululizo iliyopita tangu mwaka 2000.
Mh. David Kafulila ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi majuzi huku akiwaahidi wakuu hao wa Mikoa walioachwa kuwatumia maeneo mengine anasema, "Wakati nakuja Simiyu kama mkuu wa mkoa baada ya kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan nilikuta kero kubwa kuliko zote kwa Mkoa wa Simiyu ni "Maji".
Mh. David Kafulila ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi majuzi huku akiwaahidi wakuu hao wa Mikoa walioachwa kuwatumia maeneo mengine anasema, "Wakati nakuja Simiyu kama mkuu wa mkoa baada ya kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan nilikuta kero kubwa kuliko zote kwa Mkoa wa Simiyu ni "Maji".
Mh. David Kafulila akiwa katika picha ya pamoja na mkuu mpya wa Mkoa wa Simiyu Mhe Dkt Yahya Mawanda wakati wa makabidhiano ya ofisi mkoani Simiyu
Mh. David Kafulila anaendelea kwa kusema, Leo Mwaka mmoja huu niliokaa hapa Mkoa wa Simiyu tumeshirikiana kusimamia vizuri Sana mabilioni ya fedha za miradi ya maji zilizoletwa Mkoa wa Simiyu na Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan ninyi nyote mtakuwa mashahidi wa hili.
Mh. David Kafulila anaendelea kwa kusema, Leo naondoka katika Mkoa huu wa Simiyu wote tunaona tatizo la maji limepungua sana hapa lazima tumshukuru sana na kumpongeza Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan.
Mh. David Kafulila anaendelea kwa kusema, Leo naondoka katika Mkoa huu wa Simiyu wote tunaona tatizo la maji limepungua sana hapa lazima tumshukuru sana na kumpongeza Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan.
Mh. David Kafulila akimkabidhi mkuu mpya wa mkoa wa Simiyu ripoti ya CAG ili aendelee kusimamia majibu yote ya hoja za CAG zinazohusu mkoa wa Simiyu
Anaendelea kwa kusema, Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa maji safi na salama kwa mwaka wa 2020/21 Wakati Rais Samia anaingia madarakani nilikuta ni asilimia 56% leo tumefikia asilimia 73% na hii ni kufikia Juni 2022 lazima wana Simiyu kumshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan. Mh. Kafulila anasema, Lakini Rais Samia huyu huyu tayari ametuletea mradi mkubwa wa bomba la kilometa 190 kutoka Ziwa Victoria wenye thamani ya shilingi billioni 400. "Ndugu zangu Wanasimiyu mradi huu utapita kwenye zaidi ya vijiji vyenu 200 ambao kazi za awali nadhani tayari mnaona zimeanza. Asanteni sana kwa ushirikiano wenu huu mkubwa mliouonesha kwangu na kwa Rais Samia Suluhu Hassan".
Mh. David Kafulila akikishukuru Chama cha Mapinduzi mkoa wa Simiyu kwa ushirikiano katika kuitekeleza Ilani ya Uchaguzi 2020/25
Mh. Kafulila anaendelea kwa kusema, "niwambie ukweli, mimi nimesoma bajeti za miradi ya maji za miaka 20 mfululizo kuanzia ile ya mwaka 2000 mpaka ya mwaka 2020. Nataka niwaambie kwa miaka yote hii hakuna mwaka ambao fedha za miradi ya maji zilitolewa hata kwa asilimia 80 Tu. Lazima mfahamu, bajeti ya kwanza tu ya awamu ya sita( 2021/22) fedha za miradi ya maji zilizotolewa ni billioni 743 sawa na asilimia 95% ya bajeti iliyopitishwa na bunge na hii ni ndani ya miezi 9 tu Sio mwaka."
Mh. David Kafulila akimkabidhi Mkuu mpya wa Mkoa "SIMIYU MODEL" inayotamka kuwa "IF NO CASH THEN NO COTTON-SIMIYU"
Mh. Kafulila anaendelea kusema, "huu ni ushahidi mwingine kuwa Rais wetu anatekeleza kauli mbiu yake ya kumtua ndoo mama kichwani kwa vitendo. Rais Samia anaelewa kuwa maji ni uchumi, maji ni ustaarabu, maji ni afya na maji ni uhai. Mtakumbuka Ripoti ya shirika la Afya Duniani mwaka 2014 ilionesha kuwa kwenye kila dola moja inayowekezwa kwenye maji, inaokoa dola 4.2 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi na salama (UN- News, Nov19, 2014). Vivyo hivyo billioni 743 za miradi ya maji katika mwaka mmoja wa Rais Samia wa 2021/22 ni sawa na kusema Rais wetu kaokoa Shilingi trilioni 3.1 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji."
Vijana wa Mama Samia wakifurahia jambo katika ofisi ya mkuu wa mkoa Simiyu
Kafulila anaendelea kusema, "Labda niwakumbushe tu kwamba utafiti uliofanywa na taasisi ya SYNOVATE mwaka 2008 ulionesha kuwa kero namba moja kwa mtazania ni maji. Msiojua SYNOVATE ni taasisi 5 kwa sayansi ya uratibu wa maoni duniani wakati huo kabla haijachukulia na IPSOS ambayo kwa sasa ni moja ya taasisi 3 kubwa duniani kwa kazi hiyo(OPINION SURVEY)."
Mkuu mpya wa mkoa wa Simiyu Mh. Dkt Yahya Mawanda(kulia) katika makabidhiano ya ofisi ya Mkoa wa Simiyu toka kwa Mhe David Kafulila
Mkuu huyu wa mkoa Mstaafu anasema, "hiki ni kielelezo kuwa kiongozi anaetatua tatizo la maji anagusa maisha ya watanzania walio wengi na hasa vijijini ambao inawezekana hawana kelele nyingi kwenye mitandao wanaofahamika kama 'silent majority'. Hivyo tunaposema Mama anaupiga mwingi sio sisi ni takwimu za kitafiti."
Mh. David Kafulila akiwashukuru viongozi wenzake kwa upendo na ushirikiano mkubwa waliompa
"Hivyo tuendelee kuwasaidia wananchi kwa kuhakikisha wakandarasi wanatekeleza mikataba na tuendelee kuvunja mikataba ya wababaishaji kama tulivyofanya siku zote kuhakikisha kuwa fedha anazoleta Mh. Rais kukabili kero ya maji zinafanya kazi kwelikweli."
Mh. Dkt Yahya Mawanda akiwalisha wafanyakazi wenzake keki kama ishara ya unyenyekevu wake kwao
Hayo yamesemwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh. David Kafulila wakati wa makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kati yake na Mkuu wa Mkoa Mpya Mhe Dr Yahaya Mawanda.