Hatimaye David Kafulila akabidhi ofisi, aendelea kusisitiza Rais Samia hakamatiki utekelezaji wa Ilani, amtaja kuvunja rekodi ya miaka 20 kwenye maji

CM 1774858

JF-Expert Member
May 29, 2021
4,984
4,083
IMG-20220810-WA0013.jpg

Mhe. David Kafulila akimkabidhi Katiba ya JMT Mkuu Mpya wa Mkoa Mh. Dkt Yahya Mawanda kama nyenzo yake ya kufanyia maamuzi

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mh. David Kafulila amesema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi ya utekelezaji wa bajeti ya maji ya miaka ishirini (20) mfululizo iliyopita tangu mwaka 2000.

Mh. David Kafulila ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi majuzi huku akiwaahidi wakuu hao wa Mikoa walioachwa kuwatumia maeneo mengine anasema, "Wakati nakuja Simiyu kama mkuu wa mkoa baada ya kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan nilikuta kero kubwa kuliko zote kwa Mkoa wa Simiyu ni "Maji".

IMG-20220810-WA0003.jpg

Mh. David Kafulila akiwa katika picha ya pamoja na mkuu mpya wa Mkoa wa Simiyu Mhe Dkt Yahya Mawanda wakati wa makabidhiano ya ofisi mkoani Simiyu

Mh. David Kafulila anaendelea kwa kusema, Leo Mwaka mmoja huu niliokaa hapa Mkoa wa Simiyu tumeshirikiana kusimamia vizuri Sana mabilioni ya fedha za miradi ya maji zilizoletwa Mkoa wa Simiyu na Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan ninyi nyote mtakuwa mashahidi wa hili.

Mh. David Kafulila anaendelea kwa kusema, Leo naondoka katika Mkoa huu wa Simiyu wote tunaona tatizo la maji limepungua sana hapa lazima tumshukuru sana na kumpongeza Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan.​


IMG-20220810-WA0004.jpg

Mh. David Kafulila akimkabidhi mkuu mpya wa mkoa wa Simiyu ripoti ya CAG ili aendelee kusimamia majibu yote ya hoja za CAG zinazohusu mkoa wa Simiyu

Anaendelea kwa kusema, Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa maji safi na salama kwa mwaka wa 2020/21 Wakati Rais Samia anaingia madarakani nilikuta ni asilimia 56% leo tumefikia asilimia 73% na hii ni kufikia Juni 2022 lazima wana Simiyu kumshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan. Mh. Kafulila anasema, Lakini Rais Samia huyu huyu tayari ametuletea mradi mkubwa wa bomba la kilometa 190 kutoka Ziwa Victoria wenye thamani ya shilingi billioni 400. "Ndugu zangu Wanasimiyu mradi huu utapita kwenye zaidi ya vijiji vyenu 200 ambao kazi za awali nadhani tayari mnaona zimeanza. Asanteni sana kwa ushirikiano wenu huu mkubwa mliouonesha kwangu na kwa Rais Samia Suluhu Hassan".​

IMG-20220809-WA0015.jpg

Mh. David Kafulila akikishukuru Chama cha Mapinduzi mkoa wa Simiyu kwa ushirikiano katika kuitekeleza Ilani ya Uchaguzi 2020/25

Mh. Kafulila anaendelea kwa kusema, "niwambie ukweli, mimi nimesoma bajeti za miradi ya maji za miaka 20 mfululizo kuanzia ile ya mwaka 2000 mpaka ya mwaka 2020. Nataka niwaambie kwa miaka yote hii hakuna mwaka ambao fedha za miradi ya maji zilitolewa hata kwa asilimia 80 Tu. Lazima mfahamu, bajeti ya kwanza tu ya awamu ya sita( 2021/22) fedha za miradi ya maji zilizotolewa ni billioni 743 sawa na asilimia 95% ya bajeti iliyopitishwa na bunge na hii ni ndani ya miezi 9 tu Sio mwaka."​

IMG-20220809-WA0009.jpg

Mh. David Kafulila akimkabidhi Mkuu mpya wa Mkoa "SIMIYU MODEL" inayotamka kuwa "IF NO CASH THEN NO COTTON-SIMIYU"

Mh. Kafulila anaendelea kusema, "huu ni ushahidi mwingine kuwa Rais wetu anatekeleza kauli mbiu yake ya kumtua ndoo mama kichwani kwa vitendo. Rais Samia anaelewa kuwa maji ni uchumi, maji ni ustaarabu, maji ni afya na maji ni uhai. Mtakumbuka Ripoti ya shirika la Afya Duniani mwaka 2014 ilionesha kuwa kwenye kila dola moja inayowekezwa kwenye maji, inaokoa dola 4.2 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi na salama (UN- News, Nov19, 2014). Vivyo hivyo billioni 743 za miradi ya maji katika mwaka mmoja wa Rais Samia wa 2021/22 ni sawa na kusema Rais wetu kaokoa Shilingi trilioni 3.1 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji."​

IMG-20220810-WA0006.jpg

Vijana wa Mama Samia wakifurahia jambo katika ofisi ya mkuu wa mkoa Simiyu

Kafulila anaendelea kusema, "Labda niwakumbushe tu kwamba utafiti uliofanywa na taasisi ya SYNOVATE mwaka 2008 ulionesha kuwa kero namba moja kwa mtazania ni maji. Msiojua SYNOVATE ni taasisi 5 kwa sayansi ya uratibu wa maoni duniani wakati huo kabla haijachukulia na IPSOS ambayo kwa sasa ni moja ya taasisi 3 kubwa duniani kwa kazi hiyo(OPINION SURVEY)."​

IMG-20220810-WA0010.jpg

Mkuu mpya wa mkoa wa Simiyu Mh. Dkt Yahya Mawanda(kulia) katika makabidhiano ya ofisi ya Mkoa wa Simiyu toka kwa Mhe David Kafulila

Mkuu huyu wa mkoa Mstaafu anasema, "hiki ni kielelezo kuwa kiongozi anaetatua tatizo la maji anagusa maisha ya watanzania walio wengi na hasa vijijini ambao inawezekana hawana kelele nyingi kwenye mitandao wanaofahamika kama 'silent majority'. Hivyo tunaposema Mama anaupiga mwingi sio sisi ni takwimu za kitafiti."​

IMG-20220810-WA0011.jpg

Mh. David Kafulila akiwashukuru viongozi wenzake kwa upendo na ushirikiano mkubwa waliompa

"Hivyo tuendelee kuwasaidia wananchi kwa kuhakikisha wakandarasi wanatekeleza mikataba na tuendelee kuvunja mikataba ya wababaishaji kama tulivyofanya siku zote kuhakikisha kuwa fedha anazoleta Mh. Rais kukabili kero ya maji zinafanya kazi kwelikweli."​

IMG-20220809-WA0011.jpg



Mh. Dkt Yahya Mawanda akiwalisha wafanyakazi wenzake keki kama ishara ya unyenyekevu wake kwao

Hayo yamesemwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mh. David Kafulila wakati wa makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kati yake na Mkuu wa Mkoa Mpya Mhe Dr Yahaya Mawanda.​
 
Kama kuna RC alimwelewa na kumwelezea Vizuri Rais Samia kwa Umma basi ni Kafulila

Hamu yangu RCs waige mazuri ya Kafulila hasa kusema mazuri ya Rais wetu na Serikali anayoiongoza.

Hebu angalia hii ni kazi ya Rais Samia kwa mkoa mmoja tu Simiyu ,

Yule anayebisha Rais Samia kiboko yao anashida kubwa ya akili
 
Kafulila maneno mengi kuliko matendo

Labda ateuliwe nafasi za kwenye chama
Ivi kweli, Kafulila ni maneno matupu?

1. Kuvunja mkataba na CHICCO baada ya kuteengeneza barabara chini ya kiwango na kuokoa fedha za serikali 15bilioni ni maneno matupu haya?

2. Ivi kweli kuzui michomoko iliyoua maelfu Tanzania ni maneno matupu?

3. Ivi kweli Kuongeza bei ya pamba toka 800/kg mpaka 1,800/kg haya ni maneno matupu?

4. Ivi kweli kukamata wezi wa Pamba na kuwafunga na wengine kujinyonga ni haya ni maneno matupu?

5. Kumnyang'anya kada wa CCM yaani MNEC soko la madini alilolimiliki kinyume cha sheria haya ni maneno matupu?

Let's be serious guys Kafulila ni asset kwa Taifa letu,


Ova.
 
Ilani ya Nani ?

Huyu kuwa mpinzani alikuwa anapinga itikadi au Watu ?

Kweli Siasa full Usanii especially Bongo Chama ni Platform tu ya kuweza kwenda kupata ulaji na sio sehemu ya mawazo mbadala
 
"RAIS SAMIA AMEVUNJA REKODI YA MIAKA 20 SEKTA YA MAJI, AMEOKOA TRILIONI 3 AMBAZO ZINGETUMIKA KUTIBU MAGONJWA YATOKANAYO NA UKOSEFU WA MAJI."


Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe David Kafulila amesema Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi ya utekelezaji wa bajeti ya maji ya miaka ishirini mfululizo iliyopita,

Mhe David Kafulila anasema, wakati nakuja Simiyu baada ya kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan nilikuta kero kubwa kuliko zote kwa Mkoa wa Simiyu ni " Maji "

Leo Mwaka mmoja huu niliokaa hapa tumeshirikiana kusimamia mabilioni ya fedha za miradi ya maji ninyi nyote mtakuwa mashahidi wangu,

Leo naondoka Mkoa Simiyu wote tunaona tatizo la maji limepungua sana hapa lazima tumshukuru Sana na kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan,

Simiyu upatikanaji wa maji safi na salama kwa mwaka 2020/21 nilikuta ni asilimia 56% leo tumefikia asilimia 73% na hii ni kufikia Juni 2022 lazima wana Simiyu kumshukuru Sana Rais Samia Suluhu Hassan,

Lakini Rais Samia huyu huyu tayari ametuletea mradi mkubwa wa bomba la kilometa 190 kutoka ziwa victoria wenye thamani ya Shilingi billioni 400.

Ndugu zangu Wanasimiyu mradi huu utapita zaidi ya vijiji vyenu 200 ambao kazi za awali nadhani mnaona zimeanza,Asanteni Sana kwa ushirikiano wenu huu mkubwa,

Kafulila anaendelea kusema, Niwambie ukweli, Nimesoma bajeti za miradi ya maji za miaka 20 mfululizo kuanzia ile ya mwaka 2000 mpaka ya mwaka 2020,

Nataka niwaambie kwa miaka yote hii hakuna mwaka ambao fedha za miradi ya maji zilitolewa hata kwa asilimia 80%.

Lazima mfahamu,Bajeti ya kwanza tu ya awamu ya sita( 2021/22) fedha za miradi ya maji zilizotolewa ni billioni 743 sawa na asilimia 95% ya bajeti iliyopitishwa na bunge na hii ni ndani ya miezi 9 tu Sio mwaka.

Huu ni ushahidi mwingine kuwa Rais wetu anatekeleza kauli mbiu yake ya kumtua ndoo mama kichwani kwa vitendo.

Rais Samia anaelewa kuwa maji ni uchumi, maji ni ustaarabu, maji ni afya... Maji ni Uhai,

Mtakumbuka,Ripoti ya shirika la Afya duniani mwaka 2014 ilionesha kuwa kwenye kila dola moja inayowekezwa kwenye maji, inaokoa dola 4.2 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi na salama( UN- News, Nov19, 2014).

Hivyo hivyo billioni 743 za miradi ya maji katika mwaka mmoja wa Rais Samia wa 2021/22 ni sawa na kusema Rais wetu kaokoa Shilingi trilioni 3.1 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji.

Kafulila anaendelea kusema, Labda niwakumbushe tu kwamba utafiti uliofanywa na taasisi ya SYNOVATE mwaka 2008 ulionesha kuwa kero namba moja kwa mtazania ni maji.

Msiojua,SYNOVATE ni taasisi 5 kwa sayansi ya uratibu wa maoni duniani wakati huo kabla haijachukulia na IPSOS ambayo kwa sasa ni moja ya taasisi 3 kubwa duniani kwa kazi hiyo(OPINION SURVEY).

Mkuu huyu wa mkoa anasema, Hiki ni kielelezo kuwa Kiongozi anaetatua tatizo la maji anagusa maisha ya watanzania walio wengi na hasa vijijini ambao inawezekana hawana kelele nyingi kwenye mitandao..wanaitwa ' silent majority'..Hivyo tunaposema Mama anaupiga mwingi sio sisi ni takwimu za kitafiti.

Hivyo tuendelee kuwasaidia wananchi kwa kuhakikisha wakandarasi wanatekeleza mikataba na tuendelee kuvunja mikataba ya wababaishaji kama tulivyofanya siku zote kuhakikisha kuwa fedha anazoleta Mhe.Rais kukabili kero ya maji zinafanya kazi kwelikweli,

Hayo yamesemwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe David Kafulila leo wakati wa makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kati yake na Mkuu wa Mkoa Mpya Dr Yahaya Mawanda ambapo mbali ya kueleza sura ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila ameleza pia maamuzi 9 ya kimkakati aliyotekeleza ndani ya mwaka mmoja na mwezi 1 wa Utumishi wake katika nafasi ya hiyo ya Mkuu wa Mkoa huo wa Simiyu
Kafulila atapangiwa kazi kubwa zaidi ya mkoa let's wait and see
 
Ivi kweli, Kafulila ni maneno matupu?

1. Kuvunja mkataba na CHICCO baada ya kuteengeneza barabara chini ya kiwango na kuokoa fedha za serikali 15bilioni ni maneno matupu haya?

2. Ivi kweli kuzui michomoko iliyoua maelfu Tanzania ni maneno matupu?

3. Ivi kweli Kuongeza bei ya pamba toka 800/kg mpaka 1,800/kg haya ni maneno matupu?

4. Ivi kweli kukamata wezi wa Pamba na kuwafunga na wengine kujinyonga ni haya ni maneno matupu?

5. Kumnyang'anya kada wa CCM yaani MNEC soko la madini alilolimiliki kinyume cha sheria haya ni maneno matupu?

Let's be serious guys Kafulila ni asset kwa Taifa letu,


Ova.
Duuh, kama ni kweli jamaa yuko vizuri
 
Back
Top Bottom