Hati ya Mashtaka dhidi ya CAG Assad: Anachomokaje?

Hati ya Mashtaka dhidi ya CAG Assad: Anachomokaje?

Status
Not open for further replies.
Uhuru wa kukosoa matumizi ya kodi anayoitoa ASSAD katika serikali ya Ccm ni jukumu la Ccm pekee?


Kazi ya CAG ni kusema ukweli nje ya nchi au kukagua na kutuletea ripoti yenye mapendekezo?
 
sarakasi zote tunazoshuhudia za ukiukwaji wa katiba, wizi , kuviziana, ubabe , ufisadi kutekana , kuuana, kutukanana, kutesana and the like zitakufa a natural death in 50 years baada ya genge la wahusika wote kufukiwa na udongo, i wish wabongo wangetulia tu na kutafuta mkate wa familia, this is my theory of generation/ population! yaani huwa nacheka sana wabongo wakilalamikia chochote from the state!!! imani yangu hakuna ambacho kelele na mayowe vitabadilisha sababu we deal with the same manifesto , the same heads/brains/minds in power for almost 58 years now, si wanazeeka na kuchoka hamna macho? wengine hata kuongea kwa kitetemeshi!!wengine kutembea kwa shida! wengine wako kwenye coma! wengine spana mkononi kila siku wako India!!! for me kulalamika is just a waste of energy and time!! wenye akili watanielewa!!!
 
Umeishia darasa la ngapi?unafikiri cag anayefuata atakuwa na uhuru gani kufichua wizi wa ccm?
Atakuwa na uhuru kama huu alionao CAG wa sasa....na aliyepita kwani uhuru huo ni wa kikatiba na hakuna aliyeukiuka ...
 
Sio mshabiki wa vyama. Ila ccm kuacha wizi labda Yesu arudi. I am sorry kusema hivyo coz namwamini sana magufuli.. anafanya kazi iliyotukuka.
Lakin licha ya jitihada za rais huku chini badow atu wanapiga pesa kama kawa.. this time mpaka polisi wamo.
Kama mnapiga hela magufuli.. aija rais mpole si ndio mtaiba wazi wazi.

Ukweli ni kwamba si ccm wala chadema. Wote wale wale. Wezi wale wale. Isipokuwa ccm inapiga hela kubwa kubwa.
Report ya CAG ifanyiwe kazi.
Wakati CCM inaacha wizi Chadema inaanza wizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nduu yaii anajaribu kumtafutia kosa ila katiba inamlinda sana c.a.g na yule jamaa ninavyomjua kwa kujiamini nduu yai hawezi
 
Magazeti ya leo yamemnukuu Spika wa Bunge, Job Ndugai, akitaja mashtaka yanayomkabili CAG Assad. Ni kama ametaja hati ya mashtaka yenye tuhuma mbili, kama ifuatavyo:

Tuhuma ya kwanza: Huku ukijua kwamba, Bunge ni taasisi inayojumuisha Wabunge, Mawaziri na Rais, ambapo Rais ndiye mwajiri na mteuzi wa CAG Assad (1); na ukiwa unaelewa kwamba, Hati ya Majukumu ya CAG haisemi kuwa kutathmini utendaji wa taasisi ya Bunge ni kazi yake mojawapo, ulichukua hatua ya kufanya tathmini ya utendaji wa Bunge na kugundua kwamba Bunge ni dhaifu; na hivyo, kumdharau mteuzi wako kwa kufanya kazi iliyo nje ya majukumu yako rasmi. Mwenendo huu ni kinyume cha kifungu cha X kinachoongoza ajira yako kama CAG.

Tuhuma ya pili: Ukijua kwamba, wewe sio msemaji wa ofisi inayohusika na kutathmini utendaji wa Bunge; alibeba jukumu la kuitangazia dunia kwamba, Bunge la Tanzania ni dhaifu kwa mujibu wa Utafiti wako; na hivyo kulidhalilisha Bunge mbele ya Jumuiya ya KImataifa. Mwenendo huu ni kinyume cha kifungu cha Y kinachoongoza ajira yako kama CAG.

Wito: Hivyo, ndani ya masaa 48 baada ya kupata barua hii, unatakiwa kujitokeza mbele ya Mteuzi wako na kujieleza kwa mdomo na kwa maandishi kwa nini usichukuliwe hatua za kinidhamu.

Wako katika ujenzi wa Taifa,
Ayubu Ndugai.
Dah Mama Amon kinachoniumiza si kwa hoja zako, bali nilipata mtoto mwaka jana nikampa jina hilo bahati mbaya akafarikia after two weeks kwa uzembe wa madaktari!

Niliwasamehe ila kila nikikumba jina hili la Amon najikuta nahasira, na kutaka kulipiza kisasi!


Mungu nisaidie
 
Kuna swali nikiwauliza huwa mnapotea kuhusu sakata hili.
Je ni ripoti ipi ya CAG ilioonesha udhaifu wa bunge?

Hilo la CAG ni kama alikuja tu kukazia kilio chetu cha siku nyingi kwamba bunge ni dhaifu. Usidhani sisi kusema bunge ni dhaifu tumejikita tu kwenye hiyo ripoti ya CAG. Toka bunge limezuiwa kurushwa live. Kisha sheria za mitandao na vyombo vya habari, sheria ya vyama vya siasa nk. Wakati spika anaunda kamati ya madini na kutaka ushauri kwa rais kuhusu wajumbe. Spika kuagizwa na rais kuwanyany'anyasa wapinzani ndani ya bunge kisha yeye rais awafanyizie huku nje. Yote hayo ukichanganya na maelezo ya CAG sasa kwamba bunge ni dhaifu, kwanini tuseme bunge ni dhaifu? Ni mara ngapi bunge limefanya maamuzi kabisa ya kuonyesha lengo lake ni kujipendekeza kwa rais?
 
Safari hii CAG aweke hekima pembeni, asiende popote atakapoitwa labda court, na waje wamchukue kwa pingu dunia ione. Katiba inamlinda. Wao na wavunje katiba tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom