Hati ya Mashtaka dhidi ya CAG Assad: Anachomokaje?

Hati ya Mashtaka dhidi ya CAG Assad: Anachomokaje?

Status
Not open for further replies.
Ayubu Ndungai Nyoronyoro anathibitishia ulimwengu kama yeye ni Dhaifu na anasimamia chombo dhaifu
 
Ngoja ,muda si mrefu sakata litahitimishwa rasmi na bingwa kufahamika,hii sakata na ile ya Makonda awajibishwe kwa kuwavuruga nyie wauza ngada iliishaje?,till nao Makonda is RC of dar.

Kwani nani alikuwa anakitaka cheo chake? Cha msingi ungetutajia alimfunga nani kwenye wale aliowataja. Mpaka sasa kweli ni Mkuu wa mkoa umeona nani anamshobokea?
 
Kazi ya CAG ni kusema ukweli nje ya nchi au kukagua na kutuletea ripoti yenye mapendekezo?

Ukweli hauhitaji passport wala visa. Popote ukisema ukweli utabaki kuwa ukweli.
 
Ukweli hauhitaji passport wala visa. Popote ukisema ukweli utabaki kuwa ukweli.
Kuna swali nikiwauliza huwa mnapotea kuhusu sakata hili.
Je ni ripoti ipi ya CAG ilioonesha udhaifu wa bunge?
 
Ndugai anapaswa kuelewa kwamba chuki yake binafsi na CAG asiifanye kuwa vita baina ya CAG na bunge.

Kwa hali ilivyo CAG Assad ni muhim sana kwa taifa mara mia kuliko Ndugai na bunge lake lote, hata ikipigwa kura ya maoni sasa hivi iwe hapa jamvini au popote pale kati ya kura 100 zinaweza kuwepo tatu au nne tu zinazomkubali Ndugai mbele ya Assad. Hata kura hii ingefanyika Lumumba pale ila iwe ni ya siri basi Ndugai anaangukia pua.

Kingine ni ujibga wa Ndugai tu kutaka kupimana ubavu na Assad katika suala lisilo na kichwa wala miguu maana kimsingi baada ya kauli ya CAG ambapo kiuhalisia CAG hakusema kuwa bunge ni dhaifu bali alisema yeye jukum lake si ni kufanya ukaguzi na kama hatua hazichukuliwi basi huo ni "udhaifu" wa bunge hapa ilipasa Ndugai aeleze hatua ambazo bunge lake limezichukua ktk ripoti za CAG basi kauli ya CAG ingekosa mashiko automatically lakini anachokifanya Ndugai ni dhahiri vunge ni dhaifu.


Wema ni akiba.
 
Kama ana makosa angekua ameshaondolewa huyu. Tunashukuru Mh hachelewi kumbadilisha mtu
 
Ndugai akaisome katiba ibara inayohusu uteuzi, kazi na mamlaka ya cag aelewe na siyo kuwafanya watu wajinga humu!
Cag hahojiwi na hatakiwi kujieleza siyo tu kwa yeyote bali na hata mamlaka yake ya uteuzi!
Kwa maana nyingine ndugai umeonyesha udhaifu mkubwa kuliko tuliokuwa tunadhani unao! Jiuzulu haraka tafadhali!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom