MTOTO wa kike mwenye umri wa miaka 3 (jina linahifadhiwa) aliyedaiwa kubakwa na mwanaume aitwaye George Mshana (30) ndani ya daladala katika Kituo cha Mabasi Mwenge, jijini Dar es Salaam, jana (Jumatatu) aliliza watu katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakati mwanaume aliyedaiwa kumfanyia unyama huo akipandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake ya ubakaji...
"HII NOMA WASHKAJIII...."
Mtoto huyo ambaye alifika Mahakamani hapo akiwa na mama yake, Bi. Amina Issa na bibi yake mzaa mama, Kahungu Paschal alijikuta akizungukwa na kundi kubwa la watu ambao walikuwa wakimsikitikia na kumpa pole kwa unyama anaodaiwa kutendewa huku baadhi ya kina mama wakijikuta wakitokwa na machozi.
"POLE MAMA NA MWANA..."
Uchungu wa wananchi hao ulionekana kuzidi baada ya
mtuhumiwa George ambaye kitaaluma ni Mwandishi wa habari kupandishwa kizimbani,ambapo baadhi ya watu walisikika wakimstaajabu mwanaume huyo kuwa ni mtanashati na mzuri wa umbo na sura, hivyo kujiuliza ni sababu zipi zilimsukuma hadi kufikia hatua ya kumbaka mtoto ndani ya daladala tena mchana kweupe.
Akisoma mashitaka ya shauri hilo, mwendesha mashitaka Inspekta wa Polisi Nassoro Sisiwaya, mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo, Emelius Mchauru, alidai kuwa mnamo Aprili 16, mwaka huu majira ya saa 4 asubuhi katika Kituo cha mabasi Mwenge , Kinondoni jijini Dar es Salaam, George alimbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu ndani ya Daladala bila lidhaa yake.
Kumbe jamaa ni mtu mwenye akili timamu na maarifa yaliyokamilika na anataaluma yake???😕 Kama ni ilikuwa ni kukidhi tamaa za kimwili; mbona kina dada poa wapo wengi???maana c rahisi awe amekosa japo elf10 ya kumpa dada poa!!! Au kuna jambo jengine nyuma ya pazia!!! "TUTAFAKARI NINI CHANZO"
SOURCE: UWAZI LA LEO