Hata yale makontena tuliyozuia bandarini tutawalipa ACACIA tu, huu ni ukweli mchungu ila ni ukweli

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Naam muda utafika na haya yanayozungumzwa leo yatatekelezwa tu.

Sisi wote ni wazalendo, tena wazalendo tuliopiga kelele kwa muda kwelikweli. Tatizo letu kubwa huwa hatuachi kusema ukweli tena ukweli mchungu. Tulifungia makontena ya ACACIA pale bandarini kwa muda sasa huku tukiunda tume kuyachunguza. Sasa tuchague moja, kuwalipa fidia pale watakapodai ama kuishi kama watu ndani ya handaki, hakuna kutoka nje ama kutoa chochote. Hapo nimetumia mfano ila ni kuwa tutakapoamua kwenda kinyume na mikataba CCM waliyosaini basi tutaumia wote.

ACACIA hawakufanya biashara hewani, wamefanya biashara Tanzania na wamekaguliwa na vyombo huru tulivyojiundia sisi wenyewe, wao kama wao hawajawahi kutoka nje ya vyombo lukuki mliojiwekea enyi serikali ya CCM. Mna TMAA, mna CAG, mna ofisi ya AG, mna mahakama ya kibiashara na mbaya zaidi wanapitia kwenye njia zenu kupeleka mali zao huko ughaibuni.

Leo mnakurupuka kuwafungia kwa muda lakini tutalazimika kubuni vyanzo vingine vya mapato kuwaifidia kwa haya tunayofanya leo pale watakapoamua kufanya hivyo.

Uzalendo ukiambatana na mambo ya kujifariji na kuishi kwa matumaini ndani ya muda mfupi, huo sio uzalendo. Uzalendo huambatana na ukweli na suluhisho ambalo ukiliangalia tu unajua kuwa hili ni suluhisho. Badala yake sasa tunapiga tu blah blah na mbaya zaidi wanaotuchezesha zumari hili la blah blah wanaujua ukweli. Ole kwa wale wasiojua ukweli huo.

Jana rais Magufuli alichofanya ni kuwakumbusha tu watanzania kuwa Mkapa katuingiza cha kike. Akakumbushia machungu wee huku tukiuma meno kwa hasira. Lakini ni bora angesema pia hata haya makontena niliyozuia nitalazimika kulipa fidia pale itakapodaiwa. Huo ndiyo ukweli.

Narudia tena kuwa, ACACIA aki-step forward tu nitashangaa sana kama AG atatuma mawakili kwenda kutetea serikali! Kushinda kesi itakuwa ni ndoto ya mchana. Ni kweli tumepigwa kwa muda sana na sasa madini ni kama yanaishiaishia lakini kwa sasa tunayo maamuzi mawili tu (Haramu)
1) Kukubali kuendelea kupigwa kutokana na mkataba tuliosaini wenyewe.
2) Tuamue kufanya kama Mugabe (Huyu ni mwenzetu. Kamwe tusijilinganishe na kina Cuba, Ana Venezuela maana hawa wanajiweza sana kiuchumi). Na tukiamua kuishi kama Mugabe basi watakaoanza kuumia ni wale mafukara wa kutupwa. Kuumia kutaenda ngazi kwa ngazi hilo lipo wazi. Nje ya hapo tutakuwa tunapiga tu porojo.

Bahati mbaya sana yapo mavuvuzela humu ambayo tukiongea ukweli huu yanaleta kejeli na kuona kama tumenunuliwa! Lah! Acha tu muone hivyo lakini ukweli ndio huo! Hawa wamefanya biashara wakisimamiwa na vyombo lukuki vya serikali ya CCM, leo hawapaswi kamwe kulaumiwa. Na kinara anayelaumu naye alikuwa kwenye vikao halali vya baraza la mawaziri tangia mwaka 1998 hajawahi kuwa nje hata mara moja mpaka anakuwa rais. Bora hata Muhongo yeye aliyakuta ila siyo Magufuli.

Naona UVCCM wamepongeza, tofauti ni kuwa wakati Mkapa anasaini hii mikataba UVCCM ya wakati huo ilipongeza pia na kuuita uzalendo. UVCCM hiyohiyo ya enzi za Kikwete ilipongeza pia. Hawa huwa ni kazi yao kupongeza kila tukio la mkuu wao wa wakati huo. Ukweli ni kazi yetu sisi kuusema na ndiyo maana tunausema. Sisi ni wazalendo kweli ila pia ni wasema ukweli kweli.
 
Ni swala la muda tu.

Alafu nachojiuliza, kwa mujibu wa mkataba tulioingia,ukitokea mgogoro wa kibiashara baina ya pande mbili husika yaani sisi na wao, tunapaswa kukaa chini na kujadiliana na tukishindwana tunapelekana katika mahakama za kimatifa zinazotambulika kwa mujibu wa mkataba au upande mmoja unaruhusiwa kusitisha biashara kama tulivyofanya?
 
Kazi yenu kupinga tu

Mnaudhi sana, Sijui mnapenda tuendelee kuibiwa

Mnajifanya wajuaji sana, Serikali inajua inachokifanya, mnaropoka utadhan hiyo mikataba mshawahi hata kuiona na kujua ugumu upo wapi

Ndio maana raisi Aliunda tume mbili, Hakukurupuka,

Na kwa staili hii 2020 HAMPITI, Wa tanzania washajua udalali wenu

Yupo wapi Zitto, Lissu ? Kelele nyiiiingi hata formula ya Gold, copper, sulphur, tin ,titanium Hamzijui, Ila ujuaji mwingiiii


Shenzi kabisa
 
Si ni nyinyi mlikuwa mnalalamika kuwa mikataba ni mibovu ya Madini. Mkawa mnashauri ipitiwe upya?. Sasa utaanzaje kujenga hoja ya kupitia mikataba upya wakati huna ushahidi?? Au mlikuwa mna tudhiaki sisi watanzania?? Serikali kwa sasa inakusanya ushahidi. Tulia.
 
Kwenye liwalo na liwe ,personally naona issue ya fraud maana kuna madini yamo jamaa hawakudeclare.
Container ziko na over weight.
Tuna makosa nao pia wana makosa apa upatanishi lazima.
Wahenga walisema mwanzo mgumu ila kwenye ili tutakuwa tumewastua wawekezaji wapigaji kuwa Tz sio ya kupiga tena.
Na wanapaswa kufanya biashara ambayo iko na win win siutaion na sio win loose situation
 
Nakubaliana na wewe mkuu ila, tuombe Mungu kuwe kumepatikana ka mwanya tu ka kumkosoa huyo Accacia ili ionekane kuwa katuibia ndipo tuutumie mwanya huo kuwang'oa bila ganzi meno yao. Lakini kama ni kukurupuka, basi tujiandae kuula wa chuya
 
Yeye kasema: Pamoja na kuwa mkataba unaruhusu yale yote mnayofanya .........nataka kujiongezea umaarufu .... ninyi tulieni nikimaliza nendeni mahakamani mtalipwa fidia na gharama za kesi.... halafu katika fidia ongezeni dau langu.
Wao: Hilo nalo ni jambo. Sisi tunatulia na tutajiandaa kwenda mahakamani maana ushahidi wote tunao.
Walee: Masfaaa... huu ni uzalendo kweli kweli. Haijawahi tokea!!!
 
Ndio maana huwa munaitwa Nyumbu.. Jana hapa wote tulisifia, leo tayari mmebadili upepo..

Hatuwezi kuendelea kama nchi ina two faced people.. Sitashangaa kama Lissu nae kesho atakuja kuponda kazi ya Tume wakati alitweet kuisifia, na Zitto nae akageuka fasta na kuanza kuponda. Hatuwezi kuendelea kama nchi kwa tabia za ajabu ajabu kama hizi..
 
Ni swala la muda tu.

Alafu nachojiuliza, kwa mujibu wa mkataba tulioingia,ukitokea mgogoro wa kibiashara baina ya pande mbili husika yaani sisi na wao, tunapaswa kukaa chini na kujadiliana na tukishindwana tunapelekana katika mahakama za kimatifa zinazotambulika kwa mujibu wa mkataba au upande mmoja unaruhusiwa kusitisha biashara kama tulivyofanya?
Hapo sasa! Huwezi kuinuka tu na kufanya maamuzi 'magumu' bila kuzingatia sheria!
 
Ndio maana huwa munaitwa Nyumbu.. Jana hapa wote tulisifia, leo tayari mmebadili upepo..

Hatuwezi kuendelea kama nchi ina two faced people.. Sitashangaa kama Lissu nae kesho atakuja kuponda kazi ya Tume wakati alitweet kuisifia, na Zitto nae akageuka fasta na kuanza kuponda. Hatuwezi kuendelea kama nchi kwa tabia za ajabu ajabu kama hizi..
Aliyekwambia "wote" tulisifia nani? Speak for yourself
 
Si ni nyinyi mlikuwa mnalalamika kuwa mikataba ni mibovu ya Madini. Mkawa mnashauri ipitiwe upya?. Sasa utaanzaje kujenga hoja ya kupitia mikataba upya wakati huna ushahidi?? Au mlikuwa mna tudhiaki sisi watanzania?? Serikali kwa sasa inakusanya ushahidi. Tulia.
Watakujibu na kukuuliza nani aliingia hiyo mikataba?
Bila kuathiri mambo ya uvyama na siasa,angalizo la mtoa mada lazima liangaliwe. Ni kama programming language ya Computer inayosema:-
If....... then..........!

Yaani kuangalia mambo kwa pande mbili za shillingi. Kwamba ikitokea (a) ambayo ni +ve then.......

Pia ikitokea (b) ambayo ni negatie -ve, then.........

Kujiandaa kwa aina mbili za mambo. Ni angalizo zuri.

Magari yote ya kisasa yana mfumo huo. Kama oil haifiki kwenye engine,badala ya gari kuwaka na ku-noki engine,mfumo mpya ni gari kugoma kuwaka kabisa. Scenario ya mtoa hoja inaangalia mambo kwa mapana hayo,kadri nilivyomuelewa.
 
Watu hawajui/wamesahau kuwa Madai ya kuibiwa au kutoridhishwa na Yaliyomo kwny Mkataba sio kigezo cha kukiuka Mkataba'

Sasa hivi najulishwa Mgodi wa Buzwagi na Bulyanhulu uko mbioni kufungwa na Serikali!

Tukiwa Pamoja na Rais kumsifia kwa haya anayofanya tusijitenge nae pale tutakapoanza kukabiliwa na gharama za Maamuzi yake tunayosifia!
 
Hakuna mwekezaji mkubwa nchi hii ambaye amejisalinlmisha kwa mamlaka ya mahakama zetu. Wote kesi zao husuluhishwa ICSID
Ni swala la muda tu.

Alafu nachojiuliza, kwa mujibu wa mkataba tulioingia,ukitokea mgogoro wa kibiashara baina ya pande mbili husika yaani sisi na wao, tunapaswa kukaa chini na kujadiliana na tukishindwana tunapelekana katika mahakama za kimatifa zinazotambulika kwa mujibu wa mkataba au upande mmoja unaruhusiwa kusitisha biashara kama tulivyofanya?
 
Ingekuwa rahisi hivyo wasingekuwa wanaomba export permit serikalini kabla ya kuyasafirisha miaka yote...
Tatizo chadema inawafanya wengi wafikiri juujuu
 
Ingekuwa rahisi hivyo wasingekuwa wanaomba export permit serikalini kabla ya kuyasafirisha miaka yote...
Tatizo chadema inawafanya wengi wafikiri juujuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom