Hata hili nalo eti linamsubiri Rais Magufuli dah!

KooZito

JF-Expert Member
Dec 14, 2020
396
1,377
Kutoka kwenye ukuta wa Bollen Ngetti Face Book nami nawasukumia bila kuongeza neno.

Kuna mambo mengine ukikutana nayo yanachefua na kutia kinyaa. Yani utadhani viongozi woooote wa Mkoa wa Dar es salaam wameenda likizo, hawapo au wameamua kusubiri ziara ya Rais Magufuli ndio aje kutoa maagizo baada ya kuwatumbua.

Kwa walio jijini Dar watanielewa sana. Ukifika maeneo ya Akiba, mbele ya Chuo Cha Biashara na Uhasibu (NBAA) mbele ya geti la kutokea nje (OUT) kuna chemba ya majitaka imefumuka hapo sasa ni mwezi mzima!

Maji yote machafu yametapakaa barabarani ni harufu mbaya kiasi kwamba hata Inzi wanaogopa kusogelea.

Kwamba wanaosogelea maji hayo ya kinyesi cha binadamu na walioyafanya kuwa manukato ni wanafunzi wa CBE, NBAA, wateja matajiri wanaokuja kula Great Wall Restaurant na mama lishe wanaowapikia wanafunzi hao pembezoni mwa njia ambao sasa wameshiba harufu hiyo ambayo kwa mimi nimeumwa tumbo la kuhara!

Kinachofurahiaha ni kwamba, Mkuu wa Mkoa yupo, DC yupo, Mkurugenzi wa jiji yupo, madiwani wapo, Dawasco wapo, kila aina ya viongozi wapo lakini sasa ni raha kumsubiri Rais Magufuli atoe maagizo ndipo pashughulikiwe! Dah!

Rais Magufuli si unipe U-DC wa Ilala walau kwa saa 4 tu niokoe afya ya wanafunzi wa CBE?! Kinyaa!

#TwendePamoja2025
 
Kinachofurahiaha ni kwamba, Mkuu wa Mkoa yupo, DC yupo, Mkurugenzi wa jiji yupo, madiwani wapo, Dawasco wapo, kila aina ya viongozi wapo lakini sasa ni raha kumsubiri Rais Magufuli atoe maagizo ndipo pashughulikiwe! Dah!

Rais Magufuli si unipe U-DC wa Ilala walau kwa saa 4 tu niokoe afya ya wanafunzi wa CBE?! Kinyaa!
Watanzania hatuwezi kufanya matengenezo ya mara kwa mara ya mifumo, kuna mradi mkuwa ulifanya marekebisho ya hiyo mifumo nadhani kuanzia Kariakoo lakini haujafika mbali matokeo yake ni hayo, na si eneo hilo tu zipo seemu nyingi za namna hiyo, siku akicharuka akawaambia hap ma DED. DC na RC hataki kuona hiyo hali watakesha wakichota na ndoo
 
Acha DC ama RC ...uongozi wa Chuo haulioni hili? Au wanachojua ni kujaza wanafunzi madarasani tu?
 
Halafu badala ya kufatilia na kutatua hili tatizo, utasikia Maxine Mero anaombwa kumtaja mleta UZI ili ashughulikiwe! Bongo bwana.
 
Katika vitu vinavyonishangaza hapa Dar ni jinsi watu wasivyojali uwepo wa majitaka hapa mjini. Ni jambo la kawaida kabisa kukuta vinyesi vimezagaa juu barabarani, na watu wako pembeni wanapata huduma za chakula na matunda! Hata ukiingia kwenye vyoo vingi ni vichafu kupita maelezo. Ni kama watu wanafurahia uwepo wa vinyesi au vyoo vilivyooza.
 
Kinachofurahiaha ni kwamba, Mkuu wa Mkoa yupo, DC yupo, Mkurugenzi wa jiji yupo, madiwani wapo, Dawasco wapo, kila aina ya viongozi wapo lakini sasa ni raha kumsubiri Rais Magufuli atoe maagizo ndipo pashughulikiwe! Dah!

Rais Magufuli si unipe U-DC wa Ilala walau kwa saa 4 tu niokoe afya ya wanafunzi wa CBE?! Kinyaa!
Hufai kuwa kiongozi.

Nitakwambia kwa nini:
Usingehangaika na mizunguko yoooote uliyoandika huko juu, wewe ungekwenda tu kwa muhusika umwambie akupe kazi.

Lakini inaonekana hata akikupa kazi, mara utadai akupe kazi yake kwa kusingizia kazi zimemshinda. Sasa hapo sijui utakuwa unamshtaki kwa nani, kwa Mungu?

Kama huelewi ngoja nikurahisishie: Kuna sababu yoyote wewe kudhani kwamba hao viongozi wanamsubiri Magufuli? Kwa nini imekubidi umuingize Magufuli kwa jambo ambalo halimhusu?
 
Back
Top Bottom