A
Anonymous
Guest
Naziomba mamlaka za Mkoa wa Singida zitusaidie watumiaji wa Barabara ya Singida - Arusha kuboresha kipande kilichopo Manispaa kuanzia NBC Banki hadi kwenye jiwe lililopo katikati ya barabara maeneo ya Kirima Night Club.
Maeneo hayo kuna mashimo ya kutisha sehemu za watembea kwa miguu ambayo yamedumu muda mrefu mpaka unajiuliza hivi hapa “Kuna M/kiti wa Mtaa, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya mpaka mkuu wa mkoa? Ina maana hayaoni haya mashimo? Au tusubiri Waziri Mkuu au mama Samia waje tuwaeleze?
Maeneo hayo kuna mashimo ya kutisha sehemu za watembea kwa miguu ambayo yamedumu muda mrefu mpaka unajiuliza hivi hapa “Kuna M/kiti wa Mtaa, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya mpaka mkuu wa mkoa? Ina maana hayaoni haya mashimo? Au tusubiri Waziri Mkuu au mama Samia waje tuwaeleze?