Hata binadamu wa sasa ipo siku atatoweka kabisa (extinct)

kwaiyo kuna kaukweli gwajima anaongea kuhusu chip
Watu walio kuwa wanaidharau bible kuna baadhi ya watu wameanza kusoma ufunuo upyaa coz wameanza kujionea mambo. huku bongo bado makanisa yanayofunguliwa huko nchi za wenzetu dunia si salama sasa. serikali yoyote haitaki mtu wa kuwasumbua
 
Watu walio kuwa wanaidharau bible kuna baadhi ya watu wameanza kusoma ufunuo upyaa coz wameanza kujionea mambo. huku bongo bado makanisa yanayofunguliwa huko nchi za wenzetu dunia si salama sasa. serikali yoyote haitaki mtu wa kuwasumbua

mkuu [mention]Waterbender [/mention] ivi we ni Atheism,
 
Hicho chanzo ni wewe mwenyewe tuu kua na amani/kuchagua uamini ipi

Either uamini Chanzo cha maisha Ni Mungu..
Kuna wanaosema maisha yametokana na vitu visivyo hai na vilivyooza,
Kuna wanaodai maisha yametoka kutoka sayari nyingine kama mbegu yakaja sayari hii.
Kuna wanaodai Maisha yametokana na Muunganiko wa Elements kama Hydrogen zikaleta Compound na Compound zikaleta simple Organism baadae Complex organisms..

Kuna wanaodai Maisha yametokana na Kubadilika kwa hali ya hewa duniani Hasa Joto.

Hakuna mtu atakupa jibu la moja kwa moja la asili ya uhai, ni imani yako ichague.
Kuna mimi mwingine hapa nitakwambia maisha ni upuuzi tu kama upuuzi mwingine, yaan wewe angalia unaishije usiyaangalie maisha sababu hayana tafsiri inayotambulika rasmi
 
Evolution ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo.....

Inshu inakuja, evolution iliyopita ilikua inaangalia strong specie ndio ina survive, halafu inaendelea, then weak inatoweka.

Kwa sasa tumefikia mwisho kabisaa, Sioni tofauti kati ya strong na weak specie, unless New specie yenye sifa tofauti kabisa itokee, kitu ambacho Ki Sayansi Ni ngumu...

Kwa hio hasa hasa naona umri wa kuishi ukipungua kadiri miaka inavyozidi kwenda.
Corona imekuwa factor
 
HATA BINADAMU WA SASA IPO SIKU ATOWEKA (EXTINCT)

Iko hivi, hakuna species yoyote ambayo itaishi milele(hakuna immortal species),Kila kundi la viumbe wa jamii moja(species) ipo siku litatoweka (extinct) na kubaki historia tu kuwa lilikuwepo juu ya uso huu wa dunia..
Miaka zaidi ya million 230 iliyopita kabla hata mwanadamu hajatokea duniani kulikuwa na viumbe wanaitwa dinosaurs ambao ndio walikuwa dorminant kwenye ardhi yote ya dunia (terrestrial)lakini hadi leo imebaki historia tu hawapo wametoweka (they extinct)..
Hadi sasa kuna mabilioni ya species ambazo tayari zimetoweka(they became extinct) kwa sababu mbali mbali ikiwemo organic evolution na kushindwa kuyakabili mazingira hasa kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi..
Asili ya mwanadamu imetokea mbali zaidi ya miaka milion 5 hadi 7 iliyopita wakati dunia ipo tangu miaka zaidi ya bilion 4 iliyopita umesha jiuliza kwanini binadamu
Kachelewa mno kuwepo duniani?
Kabla ya kuwepo sisi binadamu wa kisasa kuna species nyingi tu za binadamu wa kizamani ambazo zimeshatoweka na hazipo tena ikiwemo ndugu zetu kina homo habilis, homo erectus n.k na sasa tupo sisi tolea jipya la wanadamu tunajiita homo sapiens umesha jiuliza hata sisi ipo siku tutatoweka? Jibu ni ndio
Species yetu(Homo sapiens) pia miaka mingi ijayo itatoweka na haita kuwepo kabisa kwanini dalili zimeanza kuonekana mapema mno..
Binadamu wa sasa ameanza kuwa dhaifu kuhimili magonjwa mfano hai ni COVID 19 n.k,life style ya binadamu wa sasa imeongeza hatari ya kutoweka mapema mno ikichagizwa na maendeleo ya science na teknologia,Binadamu sasa anazidiwa na mabadiliko ya tabia ya nchi ndio maana visa vya watu wengi kufa kwa joto siku hizi imekuwa kawaida tu..Kuna mtalaam mmoja aliwahi kunambia binadamu waliokufa zamani mifupa yao ilichukua muda mrefu sana kuoza(decomposition) ila binadamu anakufa leo ni miaka michache tu unaweza kuta kabuli lake halina mabaki yoyote..mifupa inaoza ki rahisi tu
Kiufupi ni kwamba hakuna species yoyote ile inayo pendelewa kwamba iishi vizuri kuliko nyingine na hii ndio maana halisi ya nature,Maneno ya kwenye dini kuwa binadamu ana akili kuliko kiumbe yoyote huwa nayo yana ukakasi kwa maana kila kiumbe kila akili kwenye mazingira yake..
#itaendelea
Jeremiah Kipoya

 
Ukingalia picha na vieo clips kutoka sayari ya Mars, unaweza kushawishika kuwa kulikuwa na maisha kwenye sayari hiyo. Lakini taratibu ilibadilika na kuwa jangwa na maji kutoweka.
Hata sisi tunaweza kukumbwa na hayo, tukatoweka kabisa.
 
Baada ya UVIKO-19.sijui Kuna janga gani laja.nikweli kizazi hiki kitatoweka haraka Sana.
Baada ya uviko apocalypse Kuna kimondo kinakuja kuipiga dunia dunia itawaka moto temperature itakua 150°C hapo binadam wataota magamba kama kobe yatakua na ac kwa ndani kwa ufupi hatutotoweka tuta adapt na tuta survive we here to stay
 
Hili nimewahi kulifikiria pia.

Historia na Biblia vyote vinaeleźea kuwa watu wa kale waliishi miaka mingi sana. Historia ikisema zaidi ya miaka elfu moja (1,000) huku Biblia ikisema binadamu aliyeishi miaka mingi aliishi miaka 930 ambaye ni Adam.

Musa anakufa na miaka 120 akiwa mwenye nguvu... Kutoka kwa Adam hadi kwa Musa ni miaka mingi sana, zaidi ya 2,000. Na Musa hakufa kwa uzee ndo maana Biblia inasema alikuwa akiwa mwenye nguvu.

Kutoka kwa Adam, Musa na sasa binadamu wa dunia ya leo ni takribani miaka 6,000 kwa mjibu wa Biblia ila lifespan (umri wa kuishi) umetoka miaka 930 ya Adam hadi 80 ya mwanadamu wa sasa (Na hii miaka 80 mtu anafika kachoka kweli kweli)

Hii inanipatia picha kwamba, miaka 100 au 200 ijayo, mtu kufikisha umri wa miaka 50 hadi 60 itakuwa jambo gumu sana (Kama tunavyoona Covid ikawatafuna wazee zaidi, na wengine ni watu wa miaka 40+ tu)

Je, hii inakupa picha gani baada miaka 1,000 ijayo??

Pia tutazame mabadiliko ya miili yetu kwa sasa.... watoto wanawahi sana kubalehe na kuvunja ungo. Si ajabu kwa sasa kuona binti wa miaka 8 au 9 kashaanza kubalehe. Zamani kidogo ilihitaji miaka 12 hadi 15 kwa mtoto wa kike kuingia balehe.

Tazama pia maumbo ya wachezaji mpira wa miaka ya 1980 hadi mwanzoni mwa 2000 ni tofauti kabisa na maumbo ya wachezaji mpira wa kizazi cha sasa.

Extinction ipo, japo ni miaka mingi ijayo, kadri tunavyozidi kuwa wengi ndivyo umri wa kuishi unavyozidi kupungua pia... kama ambavyo hatujui mwanzo wa dunia ndivyo ambavyo hatutojua mwisho wa dunia.
Sio kweli adam hakuwa binadamu aliyeishi miaka mingi zaidi. According to the bible ni Methuselah ambaye aliishi miaka mingi zaidi kwa vizazi vilivorekodiwa kwenye biblia
 
Sio kweli adam hakuwa binadamu aliyeishi miaka mingi zaidi. According to the bible ni Methuselah ambaye aliishi miaka mingi zaidi kwa vizazi vilivorekodiwa kwenye biblia
Thanks for correction mkuu japo lengo lilikuwa ni ku_correlate lifespan ya vizazi vya mwanzo na sasa.
 
Dah nikiangalia na dunia ilivo bomoka na inavoendelea kubomoka basi yawezekana binadamu ndo tukawa tumeishi kipindi kifupi zaidi katika sayari hii
 
Dah nikiangalia na dunia ilivo bomoka na inavoendelea kubomoka basi yawezekana binadamu ndo tukawa tumeishi kipindi kifupi zaidi katika sayari hii
Leo nimeota ndoto niliposhtuka nikacheka tu, eti dunia inabomoka bomoka radi inapiga balaa halafu kuna sauti inasema ni mwisho wa dunia😀.

Kwakweli binadamu tumekuwa dhaifu kwelikweli.
 
Sio kweli adam hakuwa binadamu aliyeishi miaka mingi zaidi. According to the bible ni Methuselah ambaye aliishi miaka mingi zaidi kwa vizazi vilivorekodiwa kwenye biblia
Miaka mingap aliishi
 
Mambo ya evolution hayo..

Control of population na balance of nature inaipa nguvu point zako ...

Mfano china mm huwa naamini covid ilitokea ili ibalance population japo yawezekana ilishindikana kuiweka stable . ...kama nimetoka nje ya mada sorry
 
Species kuisha kabisa nalo ni jambo lingine kabisa japo mabadiriko ya hali ya nchi na science inachangia kwa namna zote mbili kupungua kwa species au kuongezeka , ila kwa kuwa tunazaliana kila kukicha itasaidia homo sapiens kuendelea kuwepo , japo as times goes weak species zinaendelea kuzaliwa ,
 
1630174959116.png

Hahaaaaa....
Lin inaendelea,,. Species Tradeoff
 
Aise kuna kaukweli hapa mkuu. Kadri siku zinavyozidi kwenda binadamu anazidi kua dhaifu. Na sio binadamu tu hata wanyama wanaotuzunguka nao wanaishi kwa machanjo na madawa tu la sivyo wakiachwa bila tiba na wao wanajifia mapema kwa magonjwa.
Mkuu hivi mbuzi /mbwa nao watapigwa hii kitu ya chanjo?
 
Nimeipenda mada yako.Kuna ukweli ndani yake ila ningependa kujua zaidi kuhusu hayo mabadiliko uliyoyaelezea hapo juu.Je asili ya kizazi cha bnadamu kitabadilika au kutoweka kabisa?Maana nimewahi kupitia mara kadhaa historia za madinosar na nyingi znasema kuwa kuna tukio ambalo lilitokea na dunia kuharibiwa vibaya.Na baada ya hapo hakukuwa na kiumbe kilichobaki hai.Yakapita mamilioni ya miaka kabla ya kuwepo tena kwa viumbe.Swali langu ni,Je binadamu anaelekea kwenye kubadilika na kuwa kiumbe mwingine au ndio anatoweka?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom