Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,394
- 14,501
Mwimbaji Staa wa Bongo Fleva Rajabu Adbul Kahali maarufu Harmonize ametangaza rasmi dhamira yake ya kwenda kugombea Ubunge wa Jimbo la Tandahimba Mkoani Mtwara ambako ndio alikozaliwa.
Itakumbukwa October 15,2019, Harmonize ambaye kwa sasa ana-hit na wimbo mpya wa 'best couple', alitajwa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ambaye aliweka wazi kuwa anatamani Mwimbaji huyu akagombee Ubunge wa Tandahimba ingawa kwa wakati huo Harmonize alionekana kutokuwa tayari kugombea kiti hicho.
Hayati JPM alinukiwa akisema; "Lakini nampongeza sana Harmonize sijui anatoka Jimbo gani?, Tandahimba?, Mbunge wa kule ni nani?, (Katani), aah ningetamani sana Harmonize aende akagombee kule awe Mbunge wa Tandahimba"
Akiongea na Ayo TV kwa njia ya simu, Harmonize ambaye alizaliwa Kijiji cha Chitoholi Wilayani Tandahimba Mkoani Mtwara, amesema alichokiandika saa kadhaa zilizopita kuhusu dhamira ya kugombea Ubungo sio kitu cha utani bali anamaanisha ambapo muda ukifika atakwenda kuchukua fomu kupitia CCM ili aombe ridhaa ya Chama hicho kimpitishe kugombea.
Itakumbukwa October 15,2019, Harmonize ambaye kwa sasa ana-hit na wimbo mpya wa 'best couple', alitajwa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ambaye aliweka wazi kuwa anatamani Mwimbaji huyu akagombee Ubunge wa Tandahimba ingawa kwa wakati huo Harmonize alionekana kutokuwa tayari kugombea kiti hicho.
Hayati JPM alinukiwa akisema; "Lakini nampongeza sana Harmonize sijui anatoka Jimbo gani?, Tandahimba?, Mbunge wa kule ni nani?, (Katani), aah ningetamani sana Harmonize aende akagombee kule awe Mbunge wa Tandahimba"
Akiongea na Ayo TV kwa njia ya simu, Harmonize ambaye alizaliwa Kijiji cha Chitoholi Wilayani Tandahimba Mkoani Mtwara, amesema alichokiandika saa kadhaa zilizopita kuhusu dhamira ya kugombea Ubungo sio kitu cha utani bali anamaanisha ambapo muda ukifika atakwenda kuchukua fomu kupitia CCM ili aombe ridhaa ya Chama hicho kimpitishe kugombea.