Harmonize ameuliza, tumjibu!

Harmonize ameuliza, tumjibu!

Kesha unafanya kazi,
siyo ukeshe unaomba Mungu, ambaye kiuhalisia hayupo.
Mara mia ukeshe usiku kucha unamuomba mwanadamu mwenzako, atakupa msaada.
Aseeh!!
Wewe Muha umekutana na kitu gani hadi kuwa atheist?
Ila Usifike Mbali Mkuu..
Umetumia Kejeli Kubwa Sana kwa sisi tunaoamini katika Mungu.
 
Kama ulimbukeni unanisumbua, ni jambo jema.
Na kama sijapata matatizo makubwa ya duniani, ni jambo jema sana.
Na kama napotea pia ni jambo jema mno!

Nikipotea au nisipo potea, haupati faida yoyote.
Labda tu ili nipotee vizuri, itoshe kusema mungu hayupo. Na kama yupo, basi ni mshenzi.
MOD JF katika jambo jema na lenye Thawabu mbele za Allah ni KUMTOA huyu mtu humu. Kama anatolewa mtu kwa kumtukana Mwanadamu je kwa Mungu wako inakuaje. USIKUBALI HUMU JF MWANADAMU AMTUKANE MUNGU
 
Ulaya wamefunga makanisa huyohuyo Homo anaendakupiga shoo huko kwa pesa ndefu!??
 
Muda utaongea
Time will tell.

Ni bora uamini kua Mungu yupo ili hata ukifa ukimkuta au usipomkuta unakua huna hasara yeyote kuliko kutokuamini uwepo wa Mungu halafu siku ya hukumu umkute,

Dini ni imani na matendo,anayeamini aendelee kuamini na asiye amini pamoja na kuelekezwa basi aendelee na msimamo wake kwani watu wa aina hiyo ya ubishi na uasi walikuwepo pia toka zama za kale.
 
Kesha unafanya kazi,
siyo ukeshe unaomba Mungu, ambaye kiuhalisia hayupo.
Mara mia ukeshe usiku kucha unamuomba mwanadamu mwenzako, atakupa msaada.
Kiburi cha pumzi hiki,yakikufika shingoni utaanza kuomba msaada wake.
Si wewe wa kwanza kufuru,walipita majemedari na waliofikia hatua ya kujiita wao ndo mungu lakini mwisho wake wakahitaji msaada wa huyo ambaye hawaamini kama yupo
 
Maandiko yote ni michongo ya wazungu hakuna cha ziada. Swali wali waliokufa kabla ujio wa ukristo kupitia wamisionari na uislam kupitia waarabu na biashara ya utumwa. WATAHUKUMIWAJE
Biblia ipo wazi.
watahukumiwa kwa dhamili zao.
 
Sasa unasema Mungu hayupo pumzi unayovuta unaitoa wapi, na si ajabu hiyo pumzi akaichukua mda huu, watu wakikusanyika huku wakisema marehemu tulikuwa naye jana tu leo hatunaye,

hiyo pumzi siku akihihitaji ndo utajua kuwa yupo, siku akimtuma malaika mtoa roho ukiwa umetazamana nae face 2 face kwa mara ya Kwanza akiichomoa roho yako na kusepa nayo akiipeleka kwa Muumba.
Ni muda sahihi sasa dini nazo zithibitishe uwepo wa Mungu ili kuondoa sinto fahamu kwa baadhi ya wanadamu.

unapo sema pumzi anayo vuta mjumbe hii tangu utotoni nimakalilishwa ni Oxygen vivyo hivyo Oxygen inakuwa na source yake wala siyo Mungu nazani kwa hili wakemia wanaweza kutusaidia.
 
Huenda wamechagua utajiri wa kiroho badala ya vitu. Kupanga ni kuchagua
 
Wameaminishwa kua ukiwa upande wa yesu unakua na thamani kuliko elon max mwenye billions of dollars.

Hiyo imewajengea spirit ya utegevu na kujiona wao ndio bora kuliko wengine, huku wakijikuta wana invest muda wao mwingi kwenye majumba ya ibada na kupuuza shughuli za utafutaji pesa

Kuna mwamba mtaani aligoma kumpeleka mtoto wake shule, mtoto alipofika darasa latatu akamtorosha akampeleka madrasa

Na mchizi anajigamba kua ilmu akhera ndio tunu na kwa kitendo hicha cha kumtorosha mtoto wake tayari kapata thawabu

Source ya haya yote ni UJINGA
Sasa hapo hatuwezi kuilaumu dini badala yake alaumiwe huyo mja.kwasababu dini zote zimehimiza kutafuta maarifa na riziki kusoma ni miongoni mwa hizo Njia.
 
Kesha unafanya kazi,
siyo ukeshe unaomba Mungu, ambaye kiuhalisia hayupo.
Mara mia ukeshe usiku kucha unamuomba mwanadamu mwenzako, atakupa msaada.
Nimeogopa sana kwa hii statement yako.
 
Konde Gang, msanii wa Bongo Flava ameuliza kwenye wimbo wake wa dunia, kuwa ni kwa nini watu wanaokesha kusali misikitini na makanisani wana hali mbaya kiuchumi, wana maisha mabovu, hawapati baraka ambazo Biblia na Quran imeahidi kwa waumini wake, kama ambavyo Wayahudi na Waarabu wa kale walivyopata?

Anauliza kuwa ni kwa nini kila kitu kizuri kinaitwa ni cha shetani?!

Haya wanajamvi tumjibu!
Injili ya Mathayo Sura ya 7

13 Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
 
Konde Gang, msanii wa Bongo Flava ameuliza kwenye wimbo wake wa dunia, kuwa ni kwa nini watu wanaokesha kusali misikitini na makanisani wana hali mbaya kiuchumi, wana maisha mabovu, hawapati baraka ambazo Biblia na Quran imeahidi kwa waumini wake, kama ambavyo Wayahudi na Waarabu wa kale walivyopata?

Anauliza kuwa ni kwa nini kila kitu kizuri kinaitwa ni cha shetani?!

Haya wanajamvi tumjibu!
Majibu anayo nay wa mitego
 
Biblia ipo wazi.
watahukumiwa kwa dhamili zao.

Dhamila zao zilikua zinasema kuvamia tawala nyingine kuua watu ni swala la kawaida. Kuolewa na mtemi au kiongozi ata wake 10 ni swala la kawaida. Dhamili ipi unasema.
 
Kesha unafanya kazi,
siyo ukeshe unaomba Mungu, ambaye kiuhalisia hayupo.
Mara mia ukeshe usiku kucha unamuomba mwanadamu mwenzako, atakupa msaada.
Nimekuelewa
 
Kesha unafanya kazi,
siyo ukeshe unaomba Mungu, ambaye kiuhalisia hayupo.
Mara mia ukeshe usiku kucha unamuomba mwanadamu mwenzako, atakupa msaada.
Naunga mkono comment yako.Hizi dini zimekuja kuchota ubongo wetu hapa Africa
 
Mungu Kama yupo au kama hayupo, mimi hainihusu!

Huyu Mungu hanisaidii kwa chochote, wala hanisaidii kwa lolote!
Maisha yangu hayahitaji wala hayategemei Mungu.
You are totally wrong, unajua pumzi kakupa nani? Unajua kuna magonjwa mazito ya ajabu yasiyo na tiba duniani, ambayo ukiumwa utatumia hela mpaka senti tano yako ya mwisho na kubaki masikini? Nani anakuepusha nayo? Hivi unajua ndani ya mwili wako unaishi with lots of bacteria? Unafikiri anashindwa kuwaamuru wakuminye kidogo ujiharishie? Usicheze kabisa na Mungu kaka, hachezewagi huyu. Jitathmini!
 
Na Mimi nakwambia utakufa na hutakutana na kiumbe chochote kinachoitwa Mungu hizo ni hekaya za Assyrian, Sumerian, Babylon, Egyptian hazina ukweli wowote hao mnaowaita Mungu ni jamii za Annunaki wa kale ni pale watu wa kale wakashindwa kujua nao ni viumbe wa kawaida kama walivyo wao ila wanatoka garaxy za Mbali huko wakaamua wawaite Mungu Hata Babu yenu wa bandia Abraham baba ya Wayahudi aliwaahusudu kama miungu viumbe Hao Kwa sababu nae alitokea Kwenye jamii za waashuru wa kale waliocollaborate na viumbe hivyo na vikawapa ujuzi na maarifa ya Hali ya juu na wakianzisha civilization za kale,Leo nyie mmekopi hekaya hizo za kina ibrahim na kuzimeza kama zilivyo mkidhani Kila mtu ataendelea kua mtumwa na mjinga
Hapana nimeamka haabudiwi kiumbe yeyote hapa Mimi ndie Mungu mkuu wa maisha yangu!

The robots rebellion!.
 
You are totally wrong, unajua pumzi kakupa nani? Unajua kuna magonjwa mazito ya ajabu yasiyo na tiba duniani, ambayo ukiumwa utatumia hela mpaka senti tano yako ya mwisho na kubaki masikini? Nani anakuepusha nayo? Hivi unajua ndani ya mwili wako unaishi with lots of bacteria? Unafikiri anashindwa kuwaamuru wakuminye kidogo ujiharishie? Usicheze kabisa na Mungu kaka, hachezewagi huyu. Jitathmini!

we umemjuaje huyo mtoa pumzi!?. anaenipushana hayo magonjwa deadly, mbona wengine anawapa!?.
 
Back
Top Bottom