Kwanza nimefurahi kuwa umefata ushauri wangu wa kusoma tena na vizuri na kunielewa niliposema kuwa balozi hakusitisha misaada, kama ulivyosema ni angalizo tu, tena kwa misaada ya inayohusu umeme pekee.
Kuhusu maswali yako yote mawili:
1) Kitu chochte kinachuhusiana na sheria mwanasheria mkuuwa serikali anaweza kuingilia inapobidi akatakiwa kutoa ufafanuzi wa sheria.
2) Kama unamaanisha Mwanasheria mkuu wa serikali kuingia kuteua, hawezi kuingia kuteua isipokuwa anaweza kuingia atapotakiwa kutoa ufafanuzi wa kisheria katika kuteua.
Mimi sijasoma CPA kwa hiyo siwezi kuelewa mpaka ripoti itakavyoletwa.
Nahisi hapa sasa tunaongelea technicalities zaidi ya uharamu au uhalali wa fedha zilizowekwa kwenye escrow account kupewa PAP.
Kwa upande wangu na nilivyoelewa, nikuwa pesa hazikutolewa kiholela tu bali sheria zilifatwa na zilizotelewa kwa amri ya mahakama. Na nilivyoelewqa ni kuwa hizo pesa zilizowekwa kwenye escrow account zilikuwaa ni malipo halali lakini ilishindikana kulipwa wabia wa awali kwa kuwa walikuwa na matatizo yao na ndiyo ikaonekana ni vyema ziwekwe escrow account ili wamalize matatizo yao. Na nnaona mahakama ilivyoridhika kuwa tatizo limekwisha na hakuna pingamizi kutoka kwa wabia walioziuza kampuni zao kwa PAP ndiyo fedha zikaruhusiwa zilipwe kwa PAP.
Sioni tatizo kuhusu hizo pesa kuwa ni za nani au kuwa zimeibiwa. masuala yaiyobaki ni uchunguzi tu CAG utakaoamuwa kama kuna technicalities ambazo hazikufatwa au zilikiukwa na kuisababishia Serikali hasara.
Hapa PAP nionavyo mimi, hana tatizo hata kidogo, tatizo lipo katika ukiritimba na watu kuzikodolea na kuzimezea mate hizo fedha. Ni fedha nyingi sana na hata mimi natamani ningepata fungu la mgao wake.
Jee, wewe unaona tatizo ni nini?
Kwanza nakushukuru na kukupongeza kwa majibu haya na ukweli wako na pengine kwa hoja hii utasaidia wengi, unajua humu ndani tumetofautiana.
Kwanza kabisa niseme kwamba watu wanachangia mada humu lakini wanatumia utalamu wao bila kujua kuwa utaalamu wako una ukomo.
Kama ulivyosema kuwa hujasoma CPA ni watu wachache sana wanaweza kuwa wakweli kama wewe .
1.Sheria inapiganiwa Bungeni na suala ambalo ni zito lipo katika ukwepaji kodi ambapo sheria yake ipo kwenye Income Tax 2004 na ndani ya Sheria hiyo Kamishina wa kodi amepewa mamlaka makubwa na mwanasheria hawezi kuingilia
Kama kuna mgogoro wote wa suala la kupinga kulipa kodi upo utaratibu maalum ambao unajipambanua kwenye Ta Appeal Act ambako Mwanasheria mkuu wa serikali hayupo.
Sasa hiki ndicho kinacho msubua Werema kapoteza
CAG anapoweka kipengere hiki katika uchunguzi wake hakika Werema haponi angalia hizo act kwenye google utapata ukishindwa nitakutumia nipe mail yako private.
2.Hoja ya pili ni kwamba Balozi wa Uk ametoa angalizo la kusitisha misaada sasa issue hapa ni kwa nini UK watoe anaglizo hilo ?? Ina maana kunatatizo kubwa ambalo linawafanya waone bora kufanya hivyo.
Kumbuka si rahisi uk kujitoa ama kutoa angaliozo la kujitoa isipokuwa kama nchi husika imepiga marufuku Ushoga kumbuka issue ya Uganda!!
3.Kwenye masuala ya Ukagaguzi ni kwamba CAG ana nguvu kubwa kwenye eneo hilo na sheria inaonyesha kuwa hakuna wa kumwingiria.
Ndo maana CHADEMA waliyumbishwa sana kwenye sakata la kukaguliwa hesabu zake kwa kuwa mwenye mamlaka ya kuteua mkaguzi ni CAG na si vinginevyo: Vyama vya siasa haviwezi kujiteulia mkaguzi wao vyenyewe;
Sasa watu wana angamia kwa kukosa maalifa.
4.Kuna kitu kinaitwa accounting practice ambapo Wahasibu wanatakiwa kutumia IAS na IFRS. Sasa mwasibu anaweza kutumia hizo standard kuhalalisha wizi
Hivyo hivyo Accountant na Tax Consultant huwa wanatofautiana.
Mwasibu akiandaa vitabu kwa kutumia IFRS watu wa TRA wanakwenda kuchunguza kama hakutumia standards kukwepa kodi
Makampuni ya Kimataifa na hapa nchini wanatumia sana hizo standards kukwepa kodi.
Wizi unaotajwa ni wizi wa kukwepa kulipa kodi tofauti kidogo na wizi wa EPA ambao ulikuwa completely fraud.
Kwenye hili huenda hata fruad ikaibuliwa kwa maana kuna usajiri wa kampuni hewa hapo ili kukwepa kulipa kodi