Harbinder Singh Sethi aliyenunua IPTL ni nani?

Harbinder Singh Sethi aliyenunua IPTL ni nani?

Nimeisoma hiyo hadithi kwenye post #1 , sijaona mpaka sasa tatizo ni nini?

Naona mambo ya kawaida kibiashara, kulikuwa na mgogoro wa wabia wawili, Singh kupitia company yake ya PAP kazinunua kampuni zote mbili zilizokuwa na mgogoro, katatua tatizo na mkwanja uliowekwa escrow account ni wake, na hilo liliamuliwa kisheria na mahakama "The court ruled - on September 5, 2013 – in favour of VIP and all the cases were dropped. PAP was thus granted the ownership of all of IPTL assets -including money in the escrow account. PAP also agreed to pay all IPTL creditors." Kwanini usiwe wake wakati kamaliza tatizo?

Na kama alivyosema balozi wa Uingereza “Let’s wait for the results and see what really happened,” baada ya uchunguzi wa CAG na PAC.

Silioni tatizo hapo unless kuwe kuna pesa zimetolewa bila IPTL kuifanya kazi iliyokusudiwa. Nijuavyo, IPTL walifanya kazi na mahakama ilishaamuwa zamani walipwe fedha zao, tatizo lilikuwa ni baina ya wabia wawili IPTL na ndiyo maana fedha ikafunguliwa akaunti BOT mpaka hao wabia watapo maliza matatizo yao.

Tatizo ni nini?
upo sahihi kabisa
 
Jamani si mnajua Tanzania ni nchi ya tisa kati ya nchi ambazo watu wake hawafikiri vizuri?!! Ndo maana wenzetu Watanzania wakishirikiana na wageni wanateki advantage na kutuibia hasa uchaguzi unapokaribia.
 
When the incumbent President was the Minister for Energy, later Finance?

"1995-2005Minister for Foreign Affairs and International Cooperation
1995-2005Member of Parliament for Chalinze Constituency
1994-1995 Minister for Finance
1990-1995 Member of Parliament for Bagamoyo Constituency
1990-1994 Minister for Energy, Minerals and Water Development
1988-1990Deputy Minister for Energy and Minerals...ref. JF" ... Mkuu ktk mambo ambayo Watanzania walikuwa wanaamini ni Uzalendo wa JK na uweledi wake mpana kwenye sekta ya Madini! wengi tuliamini kuwa Sasa tumepata kiongozi mzalendo takaehakikisha kuwa kwa mara ya kwanza Watanzania wataanza kufaidi mapato yatokanayo na madini yao!!! Bahati mbaya sana JK alikuta BWM amekwisha ingia mikataba ya miaka 25 plus ...mbaya zaidi ni kuwa mikataba iliyofungwa ilihakikisha kuwa hawalipi kodi wala mgawo wowote kwa Watanzania... KOSA la JK ni kufumbia macho madudu ya Serikali ya BWK...
 
Chamlevi HULIWA na mgema! ... Mkuu nakubaliana na wewe lakini siyo wote katka familia ni walevi! Walevi ni wachache walioko CCM ndiyo wanaogawa mali zetu in exchange of zanzi na viroba vya pombe ya mnazi! Wagema (Westerners) wanafurahia sana biashara yao maana hawa ndugu zetu kila wakiamka asubihi wanagida ili kichwa kisiwaume kutokana na malalamiko yetu sisi tusiokuwa walevi! Sasa wameanza kuiba hadi unga wa ugali (Billions za BoT)... grrr

Wanyakyusa wanasema "MBOMBO NGAFU"

 
Sijui ni nani aliyefanyia amendments ule wigo wa kukusanya taarifa, kuanalyse na kuchukua action pale inapoonekana kuna sababu ya kufanya hivyo...wala sitaki kumjua, ilauhalifu wa Tanzania nachelea kuuita uhalifu kwa kuwa ni michezo tu ya watoto wa mjini wanaotumia advantaje ya kutopenda kwetu kufuatilia mambo kupiga tu hela..

Hautuhitaji hata ofisa wa ngazi ya wilaya (D.S.O) kujua/kufatilia uhuni unaoendelea maeneo anuai ambayo kwa kiwango kikubwa ni uhujumu wa uchumi usio na SI unit...Taarifa zinakusanywa, na nina hakika zinafika zilikokusudiwa,ila kwa sababu ya upofu/ukiziwi wa kujitakia watawala wetu wanaweza kukutuma tena ukamshauri mhujumu/mwizi badala ya kuchukua proper action juu yake...
Mkuu walioichakachua TISS wanajulikana! Kombe alikataa ujinga huo, kilichompata imebaki historia! APSON et al wana kesi ya kujibu! Nchi yetu ilikuwa inaheshimika duniani, Muundo wa TISS ni bora sana ILA TOR waliyopewa (KUSHAURI) imeiondolea meno kwa kiasi kikubwa na sasa wanaonekana kama wapo likizo! ... Unless wapewe TOR nyingine, we are done!... Tushukuru Mungu kuwa Military Intelligence bado Iko Imara ...
 
Singa singa anaonekana ana mawazo hapo.

Mkuu huyo hapo ana husika ki kampuni tu, Yeye anakula posho ya jina la kampuni yake..Wahusika wapo Tanzania na labda wengine walisha tutoka. Na ndio maana anakuambia hakuna tatizo lolote la kimkataba. Viongozi wachache wa Tanzania ni tatizo. Wizi usio na tija ndio unatuingiza sisi wenyewe kwenye matatizo. Kila kukicha unaletewa taarifa ya kwamba hela za budget hazitoshi kwasababu tunalipa watu hewa. Singa Singa na Wahindi wengi wametumika sana kuzungusha hela za wizi East africa. Huu ni mwanzo tu.. Atakapo kuja kutoka Kikwete haki nchi itakuwa ngumu kutawalika.. Yataibuka mambo mengi ambayo yatasambaza chuki kwa watanzania!!!
 
yaani hata mijitu mipumbavu isiyokuwa na mbele wala nyuma inakuja tanzania kuvuna fedha? ni nani aliyeturoga hasa?
 
Mkuu walioichakachua TISS wanajulikana! Kombe alikataa ujinga huo, kilichompata imebaki historia! APSON et al wana kesi ya kujibu! Nchi yetu ilikuwa inaheshimika duniani, Muundo wa TISS ni bora sana ILA TOR waliyopewa (KUSHAURI) imeiondolea meno kwa kiasi kikubwa na sasa wanaonekana kama wapo likizo! ... Unless wapewe TOR nyingine, we are done!... Tushukuru Mungu kuwa Military Intelligence bado Iko Imara ...

Pamoja na uwepo wa C.M.I na CID ila majukumu ya TISS yatabakia pale pale...hayatakiwi kuingiliwa hata kidogo! Haitoshi kulinda mipaka ya nchi na kuimarisha displine ya jeshi wakati adui akiwa ndani ya himaya yako...DMI watafanya nini kwenye uhujumu uchumi?
 
Hiyo list of closed corporations tena nyingine zinapishana siku mbili ndiyo inakuambia kabisa kuwa ni tapeli wa kimataifa!!
 
uchaguzi umekaribia lazima yatokee mmesahau EPA mnadhani fedha ya T-shirt, kanga, kofia na misafara mirefu zinatoka wapi ndo mana wanasema ccm ina wenyewe na wenyewe ndo hawaa sio wale wamama wanapewa kanga na kubebwa kwenye malori kuzunguka na intarahamwe walkikagua miradi bubu ya wazalendo
 
Naombeni kujuzwa huyu singasinga aliyechota hizo bilion 200 ni nani katika hii nchi na nani yupo nyuma yake anampa kiburi namna hii mbona sisi huu upuuzi hatuwezi kuufanya kwenye nchi za wenzetu ?
Bungeni kwa sasa ndugu mbunge kutoka kambi ya upinzani amewasilisha ushahidi kwa spika na anasema Kifo cha Mgimwa kinatakiwa kuchunguzwa kwa vile alipingana kwa nguvu zote hizo hela zisitoke na baada ya kuugua na kulazwa south afrika ndipo ubaradhuli huo ulipofanyika sasa najiuliza hii nchi haina kiongozi?
Bila kumungunya maneno kwa hatua tulipofika jeshi halina budi kuichukua nchi ikairudisha kwenye mstari kwa vile sasa hivi hakuna utawala wa sheria tena ni danganya toto mwenye macho haambiwi tazama.
 
Hivi nyie mnajua maana ya account ya Escrow? hizo hela sio za Serikali, acheni siasa chafu.
 
Hivi nyie mnajua maana ya account ya Escrow? hizo hela sio za Serikali, acheni siasa chafu.
Hakika umenena.
Umenikumbusha mtu mmoja aliwahi kuporwa wallet yake na kibaka na wakati akijaribu kuomba msaada kwa walioshuhudia hilo tukio yule kibaka anaongea tena kwa kujiamini kuwa "hii wallet sio yako, ni yangu"! Na kwa vile yule kibaka ndiye aliyekuwa ameishika kwa muda huo wengi walimwamini isipokuwa wachache na waelevu ndio walijua kuwa yule ni kibaka! Tanzania yangu wee...!

 
Naombeni kujuzwa huyu singasinga aliyechota hizo bilion 200 ni nani katika hii nchi na nani yupo nyuma yake anampa kiburi namna hii mbona sisi huu upuuzi hatuwezi kuufanya kwenye nchi za wenzetu ?
Bungeni kwa sasa ndugu mbunge kutoka kambi ya upinzani amewasilisha ushahidi kwa spika na anasema Kifo cha Mgimwa kinatakiwa kuchunguzwa kwa vile alipingana kwa nguvu zote hizo hela zisitoke na baada ya kuugua na kulazwa south afrika ndipo ubaradhuli huo ulipofanyika sasa najiuliza hii nchi haina kiongozi?
Bila kumungunya maneno kwa hatua tulipofika jeshi halina budi kuichukua nchi ikairudisha kwenye mstari kwa vile sasa hivi hakuna utawala wa sheria tena ni danganya toto mwenye macho haambiwi tazama.

Red:
MEREMETA je umeshaisahau. Nchi hii hakuna mkweli na wa kumuamini. ni wananchi tu popote pale walipo BILA WANASIASA watumie raslimali zinazowazunguka kwa nguvu ya UMMA. Hakuna cha jeshi wala nini - hapa tulipo unayafahamu madudu ya jeshini - ya mnadhimu mkuu alie "staafu" umeyasahau!!

Wa Tz tunaishi kwa neema tu ya MUUMBA - hakuna cha vyama vya siasa wala vitukuu wao
 

Red:
MEREMETA je umeshaisahau. Nchi hii hakuna mkweli na wa kumuamini. ni wananchi tu popote pale walipo BILA WANASIASA watumie raslimali zinazowazunguka kwa nguvu ya UMMA. Hakuna cha jeshi wala nini - hapa tulipo unayafahamu madudu ya jeshini - ya mnadhimu mkuu alie "staafu" umeyasahau!!

Wa Tz tunaishi kwa neema tu ya MUUMBA - hakuna cha vyama vya siasa wala vitukuu wao

Ndugu kwa jeshi waliofaidi ni wakubwa tu ndugu nchi zoote jeshi linaposhika hatamu wale wasiokua na vyeo vikubwa ndo huwa wanakuwa na nguvu na ni robo tatu ja jeshi lote na wale wakiamua wakubwa hawana jinsi ndugu na wengi wao ndio hao tumebanana nao kwenye vyumba vya kupanga uswazi shida tunazopata wanaziona nina imani freedom is coming soon.
 
Mkuu huyo hapo ana husika ki kampuni tu, Yeye anakula posho ya jina la kampuni yake..Wahusika wapo Tanzania na labda wengine walisha tutoka. Na ndio maana anakuambia hakuna tatizo lolote la kimkataba. Viongozi wachache wa Tanzania ni tatizo. Wizi usio na tija ndio unatuingiza sisi wenyewe kwenye matatizo. Kila kukicha unaletewa taarifa ya kwamba hela za budget hazitoshi kwasababu tunalipa watu hewa. Singa Singa na Wahindi wengi wametumika sana kuzungusha hela za wizi East africa. Huu ni mwanzo tu.. Atakapo kuja kutoka Kikwete haki nchi itakuwa ngumu kutawalika.. Yataibuka mambo mengi ambayo yatasambaza chuki kwa watanzania!!!

..na hapa anazungumzwa singasinga tu....watu wameshasahau kuwa hii kampuni ya PAP iliuziwa share zake 30% kimagumashi na ile kampuni ya VIP Engineering ya kina James Rugemalira (mzee wa senti)....In fact swala la VIP kugawa 30% ya share zake za IPTL kwa PAP limekuja wakati wanachota fedha za escrow kule BOT....


....Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa pia hata hawa PAP mgao wa escrow hawakupata.....fedha ya esrow kuna uwezekano mkubwa imetafunwa na VIP na vigogo wa seriali ya TZ....pamoja na kwamba hata VIP wamiliki wake ni wahindi...Na hawa woote wameshtakiwa kule UK na bank ya Standard Chatered HK......Ukweli utajulikana watakaposhindwa kesi na kuanza kutupiana mpira.....ni swala la mda tu....

...Kama usemavyo kweli mkuu...huu utawala wa mapanya na mafisi utakapoondoka ndipo watanzania wengi watakapojua madhila waliyofanyiwa na utawala huu.....sasa hivi watawala wanajitahidi kila wawezalo kuficha mambo ili raia wengi watanzania wasijue...haswa kipindi hiki kuelekea 2015 .. .utaona hata jitihada zinazofanywa humu JF kwa mfano.....watu wanang'ang'ana kutetea wizi bila aibu.....yana mwisho lakini...watu wanasahau kuwa vyombo vya sheria vipo hata watakapotoka madarakani....watajibu tu...its just a matter of time....waache wajiridhishe sasa...
 
Back
Top Bottom