Amani iwe kwenu wapendwa.
Background: Mifuko ya hii ya NSSF na PPF (siku hizi PSSSF) ilikuwa na utaratibu kwamba unapoacha kazi kwa hiari, kufukuzwa, mkataba kuisha unachukua hela yako maisha yanaendelea.
Around 2014/2015 huo utaratibu ulisitishwa, ukiuliza unaambiwa sheria hairuhusu, ingawa kuna baadhi walikuwa wanapata kwa mikakati maalum.
Mifuko ikaunganishwa, likaja swala la vikokotoo na Fao la Kukosa Ajira.
Tar 28 Dec 2018, Mh Rais alitengua swala la vikokotoo vipya na kusema mambo yawe kama zamani, ni baada ya kufanya kikao na wadau husika SSRA, wawakilishi wa wafanyakazi, wahusika wa taasisi hizo nk. Na tumeona maandamano ya kumpongeza Rais kwa tukio hili.
Bahati mbaya, kinachoonekana ni kwamba swala la Fao la Kujitoa limewekwa kando, tukifatilia tunaambiwa hakuna mwongozo.
Kuna watu kibao wako mtaani na kazi zimekuwa ngumu kupata, kuna walio maofisini wangetamani kuacha wachukue mitaji wafanye mambo yao, kuna walio maofisini muda wowote watakuwa vijiweni nao wanatamani kuwa na uhakika wa hii fedha.
Kama hili swala lisipopatiwa ufumbuzi kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, tusahau kulipatia ufumbuzi.
Nini cha kufanya:-
Wahanga, na wote ambao ni wazalendo tunatakiwa kwa pamoja tutoe mapendekezo kuhusu hili swala, kama ni kutengeneza petition, kama ni kufanya maandamano kuonana na waziri husika, waziri mkuu au kuelekea SSRA, kama pia ni kufanya utaratibu wa kuonana na Rais, etc.
Kupitia hii thread, tunaweza ku-brainstorm ni njia ipi tunaweza kuitumia kuhakikisha taarifa zinamfikia Rais kwamba kuna watu wanakufa njaa wakati hela zao zipo, haki yao ipo.
Tukumbuke kwamba jinsi tutakavyoonesha wingi wetu, influence yetu ndivyo hivyo hivyo swala letu litachukuliwa serious.
Naomba kuwasilisha.