Halotel mnatuibia wateja wenu

Halotel mnatuibia wateja wenu

Kyawanjubu

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2017
Posts
2,453
Reaction score
2,205
Halotel baada ya kusifiwa kua na huduma nzuri lakini saizi ni tofauti kabisa spidi yao ya intanet imepungua sana afu wanakula Mb unaweza sema simu imetoboka znavujia chini mwanzo Mb 600 nilikua natumia hata kwa siku 3 lakini saizi hata masaa 24 hazimalizi muda sio mrefu natupa line lenu maana nilinunua kwa ajili ya Mb

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilidhani ni mimi pekeangu, mb sikuhizi hazikai pamoja na kwamba wamezipunguza kiasi flani ila nina imani hata nikiweka data manager ikawa inanipa records za data kiasi gani nimetumia toka nimejiunga bando lao, ita detect wizi wanaoufanya!
 
Washenzi af sasa wanachokifanya yani, siku hizi nikiingia youtube tu hata kuangalia nyimbo moja tu, kama nilijiunga nusu saa iliopita basi masaa 24 hayafiki mb zinakata. Ila usipotumia youtube bando linavumilia hata siku mbili.
 
Hawa tuwaanzishie tu kama tigo, kuwapa market share ya 7% ishawapa jeuri sana hawa. Ngoja tuangalie upepo tutimukie mtandao mwengine
 
he he he he

Mwacheni mukulu mstaafu aokote chenchi chenchi zenu aiseeee.

Mbona mna roho mbaya hivyo??
 
Mi nimeshawachoka halotel, nahamia ttcl nasikia wako vizuri.
 
Back
Top Bottom