Nape: Kama kuna mtu kaibiwa bundle alete ushahidi

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,554
Waziri Nape - Clouds TV
Trh 20. 08. 2022

11036601-116F-419D-93E8-BC4AF029F44B.jpeg


Serikali ilifanya tathimini ya mwisho ya gharama za data mwaka 2018 ambayo ndiyo inatumika hadi sasa.

Tathimini hii ilionesha kuwa gharama ya kusafirisha unit ya data ipo kati ya tsh 2.09-9.35

Tathimini mpya kwa sasa inafanyika ambayo itaanza kutumika tena mwaka kesho. Hii ina maanisha kuwa mapitio haya hufanyika kila baada ya miaka 4.

Hali ya sasa inaonesha kuwa kuna line milioni 58 za simu nchini. Jambo hili lilifanya tuwe na wateja wengi kuliko watoa huduma.

Kwenye data, wingi huu wa watu uliathiri ubora wa huduma. Hatupaswi kuwa wapiga kelele wakati wa kuongea na simu, hatupaswi kumpigia mtu simu afu asipatikane.

Baada ya kuona ongezeko kubwa sana la bei, Serikali iliamua kuwavuta watoa huduma kutoka tsh 40.41 hadi 9.35, kazi hii imefanywa na Serikali ya awamu ya 6.

Hivi sasa tunavyozungumza bei ya kununua data Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa tsh 1.71-9.35 na watoa huduma hawapaswi kuzidisha hapo.

Hata hapa tulipo, tunabanana kuuza data chini ya kiwango inachozalishwa.

Kwa takwimu za sasa, Tanzania ni nchi ya 6 Afrika kwa unafuu wa gharama za data, ya 50 duniani kwa unafuu huu. Tafiti hizo zimefanywa na mataifa tofauti, hazijafanywa na Serikali.

Hii bei ni ya chini sana kwa kuangalia, sisi watu wetu bado maskini. Purchasing power yao ni ndogo ndiyo maana Serikali inadhibiti ili isipande sana.

Sasa tunafanya tathimini upya ili kuja na mapitio mapya ya maeneo yanayo toa mwongozo wa bei. Maeneo hasa ya usafirishaji wa data ndiyo tunashughulikia kwa sasa. Lengo ni kupunguza gharama hizi.

Mwanzoni gharama ilikuwa ndogo kwa sababu baadhi ya watoa huduma wali compromise ili kuiweka chini zaidi lakini huduma zao zikawa mbovu.

Serikali haipuuzi na haitakuja kupuuza malalamiko ya watu wake. Tunasikia na tunashughulikia.

KUHUSU VIFURUSHI

Hizi ni huduma za ziada, siyo huduma za msingi. Kuna ambavyo vimeshuka na vingine vimepanda. Hili nalo tunapitia

Mtoa huduma hawezi tu kupandisha bei pasipo kuleta mapendekezo kwa mamlaka (TCRA) . Hii nayo hufanyika kila baada ya miezi 3.

Kazi ya makampuni siyo kuomba ridhaa kwa wananchi, isipokuwa ni kuwapa tu taarifa juu ya biadhaa mpya wanazotoa. Lakini, bidhaa hizo hupitia kwanza TCRA

MASWALI NA MAJIBU

MDAU 1:
Unapewa MB 550 tu kwa siku, na kabla ya masaa 24 kimeisha hata haujatumia sana. Hii imekaaje?

Nape: Kwenye kuchagua unapewa muongozo, ni mitambo wameseti ambayo watoa huduma na mamlaka wanapitia kuhakiki usahihi wa mitambo hii.

Hii nime address sana, na nilisema tangu mwanzo. Kama kuna mtu kaibiwa aje atoe ushahidi wa kuibiwa bando. Wengi wamekuja na baada ya uchunguzi wanaelewa.

Ni vizuri kuwa makini na matumizi ya smart devices tunazotumia. Kuna mambo mengi yanaendelea nyuma ya pazia ambayo unaweza ukawa hujui.

Unaweza tu kuwa unapakua WhatsApp. Kitendo cha kubonyeza sehemu ya kukubali kikaja na mambo mengine ambayo pia yanakula data yako. Tuwe makini.

Leo pia narudia, kama kuna mtu hajatendewa haki aje. Mimi pia natamani nipate kesi moja ya wizi ithibitishwe ili iondoe yote haya.

==

MDAU 2: Tunapewa tu taarifa na makampuni kuwa vifurushi vimepanda, lakini hatuna nafasi ya kutoa maoni. Tufanye nini?

Nape: Unaweza kutoa maoni yako TCRA, wanasikiliza. Tena kuna desk moja pale kwa ajili ya watu wa aina hii.

==

MDAU 3: Bei zitashuka?
Nape: Tunashughulikia

==

MDAU 4: (Alitoa lugha ya matusi)
Nape: Niulize vizuri, nitakujibu vizuri. Matusi hayawezi kusaidia. Tuwe na utaratibu wa kuzungumza kwa staha.

==
MDAU 5: Kwanini gharama za kusajili line zisipande ili kuzuia watu wengi kuwa na line nyingi ambazo zinaelemea makampuni?

Nape: Haya ni maoni, nimeyapokea.

==

MDAU 6: Mimi natumia kiswaswadu. Nikiunga kifurushi cha dakika na data, internet yangu huenda wapi na sijaitumia?

Nape: Nunua kifurushi kisicho na internet ili kuondokana na kadhia hii.

==

MDAU 7: Kwanini mnatumia US dollar kwenye comparison na siyo Tsh ambayo ndiyo uhalisia wa maisha ya mtanzania?

Nape: US dollar ni swala la kidunia. Ndiyo kiasi kinachotumika kulinganisha gharama zetu na huko duniani.

Tunapozungumza kwa lugha ya ndani tunatumia Tsh, tukiweka mizani nje ya mipaka ya nchi tunatumia dollar.

==

MDAU 8: Kwanini bando lina expire hata kama sijatumia?

Nape: Weka salio la kawaida, masharti ya bado yapo hivyo.

Ni kama tiketi ya mwezi (kwenye basi), mwezi ukiisha hata kama haujatumia ina expire.

==

AGIZO
Kila kampuni ya simu na TCRA waendelee kuelimisha watu, nataka kuona TCRA wakijibu maswali ya watu na makampuni ya simu yakiendelea kutoa elimu.

Wito wangu ni watu wapunguze hasira, watoe maoni kwa lugha ya staha kwani lengo letu ni moja tu, kujenga.
 
Serikali ilifanya tathimini ya mwisho ya gharama za data mwaka 2018 ambayo ndoyo inatumika hadi sasa.

Tathimini hii ilionesha kuwa gharama ya kusafirisha unit ya data ipo kati ya tsh 2.09-9.35

Tathimini mpya kwa sasa inafanyika ambayo itaanza kutumika tena mwaka kesho. Hii ina maanisha kuwa mapitio haya hufanyika kila baada ya miaka 4.

Hali ya sasa inaonesha kuwa kuna line 58 za simu nchini. Jambo hili lilifanya tuwe na wateja wengi kuliko watoa huduma.

Kwenye data, wingi huu wa watu uliathiri ubora wa huduma. Hatupaswi kuwa wapiga kelele wakati wa kuongea na simu, hatupaswi kumpigia mtu simu afu asipatikane.

Baada ya kuona ongezeko kubwa sana la bei, Serikali iliamua kuwavuta watoa huduma kutoka tsh 40.41 hadi 9.35, kazi hii imefanywa na Serikali ya awamu ya 6.

Hovi sasa tunavyozungumza bei ya kununua data Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa 1.71-9.35 na watoa huduma hawapaswi kuzidisha hapo.
Chawa

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mwanzo: gharama ya kusafirisha unit ya data ipo kati ya tsh 2.09-9.35

Sasa: sasa tunavyozungumza bei ya kununua data Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa 1.71-9.35

Sasa hapa kuna punguzo gani ikiwa kiwango cha juu kingali kile kile?
 
Huyu jamaa anafikiri internet ni siasa,mkongo wa taifa(seacom) umemshinda na hiyo ndio nguzo ya kushusha bei.
 
Magu ameingia 2015 kakuta shilingi elfu 1 tunapata GB 1.5 hadi 2.

Magufuli amefariki mwaka jana shilingi elfu moja tunapata GB 1.

Ndani ya mwaka mmoja wa serikali ya kikatiba shilingi elfu 1 unapata MB 400, hakafu tunaambiwa mama ameshusha gharama, ameshusha nini hapo?

Mwaka jana serikali ya kikatiba iliposhika hatamu shilingi elfu 50 tulikua tunapata kati ya GB 50 hadi 60 kwa mwezi, baada ya miezi 6 wakashusha hadi GB 37 kisha wakashusha hadi GB 32 na leo elfu 50 unapata GB 28, je hii ndio maana ya kuupiga mwingi?

Wao kina nape kw akua wanalipiwa bando kwa kodi zetu hawaoni shida.

Nape asivyo na akili anatolea mfano nchi kama Marekani, Canada na Uingereza kwamba soko linaamua. Hii nchi ina viongozi wa hovyo sana.

Sasa namkumbuka Ndugai, alishauri 2025 tuondoe hawa watu.
 
Magu ameingia 2015 kakuta shilingi elfu 1 tunapata GB 1.5 hadi 2.

Magufuli amefariki mwaka jana shilingi elfu moja tunapata GB 1.

Ndani ya mwaka mmoja wa serikali ya kikatiba shilingi elfu 1 unapata MB 400, hakafu tunaambiwa mama ameshusha gharama, ameshusha nini hapo?

Mwaka jana serikali ya kikatiba iliposhika hatamu shilingi elfu 50 tulikua tunapata kati ya GB 50 hadi 60 kwa mwezi, baada ya miezi 6 wakashusha hadi GB 37 kisha wakashusha hadi GB 32 na leo elfu 50 unapata GB 28, je hii ndio maana ya kuupiga mwingi?

Wao kina nape kw akua wanalipiwa bando kwa kodi zetu hawaoni shida.

Sasa namkumbuka Ndugai, alishauri 2025 tuondoe hawa watu.
Na bado kulikuwa na free wifi, ukiwa na mia 5 unapata mb za kutosha kwa wanachuo au maeneo ya karibu na chuo.

Sasa hivi bando la chuo ni gharama kubwa kuliko hata la kawaida!

Nawaonea huruma wadogo zangu hasa kwa vyuo visivyo na free wifi ya kudownload module!
 
Sielewi hiki kitu, huo unafuu wa gharama huwa anaupimaje?

Nakumbuka miaka miwili nyuma, GB moja ilikuwa ikiuzwa kwa 1500/= leo tshs 1500/= ni MB 850.

Nape akiwa anazungumza sijui huwa anatumia vigezo gani.
 
Na sioni kama ni sahihi kwa yeye waziri kulisemea hili kwa kutoa ufafanuzi.

Nadhani ilitakiwa atoe maagizo kwa wahusika wa mitandao kutoa ufafanuzi wa kwanini wanaongeza gharama za vifurushi na kukata salio kwenye simu bila makubaliano.

Kuwajibia ni sawa na kukubaliana na wanachofanya. Ilihali si sahihi
 
Waziri Nape - Clouds TV
Trh 20. 08. 2022
View attachment 2329004


Serikali ilifanya tathimini ya mwisho ya gharama za data mwaka 2018 ambayo ndiyo inatumika hadi sasa.

Tathimini hii ilionesha kuwa gharama ya kusafirisha unit ya data ipo kati ya tsh 2.09-9.35

Tathimini mpya kwa sasa inafanyika ambayo itaanza kutumika tena mwaka kesho. Hii ina maanisha kuwa mapitio haya hufanyika kila baada ya miaka 4.

Hali ya sasa inaonesha kuwa kuna line milioni 58 za simu nchini. Jambo hili lilifanya tuwe na wateja wengi kuliko watoa huduma.

Kwenye data, wingi huu wa watu uliathiri ubora wa huduma. Hatupaswi kuwa wapiga kelele wakati wa kuongea na simu, hatupaswi kumpigia mtu simu afu asipatikane.

Baada ya kuona ongezeko kubwa sana la bei, Serikali iliamua kuwavuta watoa huduma kutoka tsh 40.41 hadi 9.35, kazi hii imefanywa na Serikali ya awamu ya 6.

Hivi sasa tunavyozungumza bei ya kununua data Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa tsh 1.71-9.35 na watoa huduma hawapaswi kuzidisha hapo.

Hata hapa tulipo, tunabanana kuuza data chini ya kiwango inachozalishwa.

Kwa takwimu za sasa, Tanzania ni nchi ya 6 Afrika kwa unafuu wa gharama za data, ya 50 duniani kwa unafuu huu. Tafiti hizo zimefanywa na mataifa tofauti, hazijafanywa na Serikali.

Hii bei ni ya chini sana kwa kuangalia, sisi watu wetu bado maskini. Purchasing power yao ni ndogo ndiyo maana Serikali inadhibiti ili isipande sana.

Sasa tunafanya tathimini upya ili kuja na mapitio mapya ya maeneo yanayo toa mwongozo wa bei. Maeneo hasa ya usafirishaji wa data ndiyo tunashughulikia kwa sasa. Lengo ni kupunguza gharama hizi.

Mwanzoni gharama ilikuwa ndogo kwa sababu baadhi ya watoa huduma wali compromise ili kuiweka chini zaidi lakini huduma zao zikawa mbovu.

Serikali haipuuzi na haitakuja kupuuza malalamiko ya watu wake. Tunasikia na tunashughulikia.

KUHUSU VIFURUSHI

Hizi ni huduma za ziada, siyo huduma za msingi. Kuna ambavyo vimeshuka na vingine vimepanda. Hili nalo tunapitia

Mtoa huduma hawezi tu kupandisha bei pasipo kuleta mapendekezo kwa mamlaka (TCRA) . Hii nayo hufanyika kila baada ya miezi 3.

Kazi ya makampuni siyo kuomba ridhaa kwa wananchi, isipokuwa ni kuwapa tu taarifa juu ya biadhaa mpya wanazotoa. Lakini, bidhaa hizo hupitia kwanza TCRA

MASWALI NA MAJIBU

MDAU 1:
Unapewa MB 550 tu kwa siku, na kabla ya masaa 24 kimeisha hata haujatumia sana. Hii imekaaje?

Nape: Kwenye kuchagua unapewa muongozo, ni mitambo wameseti ambayo watoa huduma na mamlaka wanapitia kuhakiki usahihi wa mitambo hii.

Hii nime address sana, na nilisema tangu mwanzo. Kama kuna mtu kaibiwa aje atoe ushahidi wa kuibiwa bando. Wengi wamekuja na baada ya uchunguzi wanaelewa.

Ni vizuri kuwa makini na matumizi ya smart devices tunazotumia. Kuna mambo mengi yanaendelea nyuma ya pazia ambavyo unaweza ukawa hujui.

Unaweza tu kuwa unapakua WhatsApp. Kitendo cha kubonyeza “Accept” kikaja na mambo mengine ambayo pia yanakula data yako. Tuwe makini.

Leo pia narudia, kama kuna mtu hajatendewa haki aje. Mimi pia natamani nipate kesi moja ya wizi ithibitishwe ili iondoe yote haya.

==

MDAU 2: Tunapewa tu taarifa na makampuni kuwa vifurushi vimepanda, lakini hatuna nafasi ya kutoa maoni. Tufanye nini?

Nape: Unaweza kutoa maoni yako TCRA, wanasikiliza. Tena kuna desk moja pale kwa ajili ya watu wa aina hii.

==

MDAU 3: Bei zitashuka?
Nape: Tunashughulikia

==

MDAU 4: (Alitoa lugha ya matusi)
Nape: Niulize vizuri, nitakujibu vizuri. Matusi hayawezi kusaidia. Tuwe na utaratibu wa kuzungumza kwa staha.

==
MDAU 5: Kwanini gharama za kusajili line zisipande ili kuzuia watu wengi kuwa na line nyingi ambazo zinaelemea makampuni?

Nape: Haya ni maoni, nimeyapokea.

==

MDAU 6: Mimi natumia kiswaswadu. Nikiunga kifurushi cha dakika na data, internet yangu huenda wapi na sijaitumia?

Nape: Nunua kifurushi kisicho na internet ili kuondokana na kadhia hii.

==

MDAU 7: Kwanini mnatumia US dollar kwenye comparison na siyo Tsh ambayo ndiyo uhalisia wa maisha ya mtanzania?

Nape: US dollar ni swala la kidunia. Ndiyo kiasi kinachotumika kulinganisha gharama zetu na huko duniani.

Tunapozungumza kwa lugha ya ndani tunatumia Tsh, tukiweka mizani nje ya mipaka ya nchi tunatumia dollar.

==

MDAU 8: Kwanini bando lina expire hata kama sijatumia?

Nape: Weka salio la kawaida, masharti ya bado yapo hivyo.

Ni kama tiketi ya mwezi (kwenye basi), mwezi ukiisha hata kama haujatumia ina expire.

==

AGIZO
Kila kampuni ya simu na TCRA waendelee kuelimisha watu, nataka kuona TCRA wakijibu maswali ya watu na makampuni ya simu yakiendelea kutoa elimu.

Wito wangu ni watu wapunguze hasira, watoe maoni kwa lugha ya staha kwani lengo letu ni moja tu, kujenga.
Nape ni mchafu kama ilivyo oil, kauli yako Nape ya kuonesha kushangilia kifo cha Dkt Magufuli kitakugharimu maisha yako yote, usidhani kusema eti awamu ya 5 kulikuwa na gharama kubwa kunamchafua Dkt Magufuli, bali unazidi kujianika ulivyo na furaha na kifo cha Dkt Magufuli. Hivyo kaa ukijua watanzania wanakuchukia sana tena sana kwa kuonesha kufurahia kifo cha Dkt Magufuli na hapo ndipo ulishajichimbia kaburi la siasa
 
Back
Top Bottom