Titho Dyakiye Philemon
Member
- Nov 15, 2019
- 49
- 128
Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ni Miongoni mwa Halmashauri 8 zinazounda Mkoa wa Kagera ikiwa na Jumla ya Vitongoji 389, Vijiji 75, Mitaa 34, Kata 22 na Tarafa 4.
Mapema mwaka huu Halmashauri hii iliwasilisha Rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti kwa Mwaka 2025/2026 huku wadau wengi wa maendeleo ya wilayani hapa wakiwa wamefanikiwa kuipitia vilivyo na kwa upana wake, na mimi nikiwa miongoni mwa wadau hao.
Katika Rasimu hiyo, Kipengele cha Mapitio ya Bajeti kwa Mwaka 2024/2025 iligundulika wazi KUKOSEKANA kwa uwiano kati ya hesabu ya kile kilichoandikwa katika matumizi ikilinganishwa na hali halisi ya kile kinachoonekana Mtaani (vijijini) kwenye UHALSIA.
Lakini pia, wadau tumekuja kubaini kuwa baadhi ya matumizi ya fedha ndani ya Halmashauri zetu huwa hawazingatii thamani ya fedha yaani Value for Money kiasi cha kuweka uwiano kati ya Mradi ulioandikwa na gharama zake na kulinganisha na thamani ya Mradi.
Tumejikuta kwenye Halmashauri zetu tukiwa na Ripoti za Bajeti za Kupikwa na walengwa ili kuwavutia serikali kuu na kule wanapopeleka ripoti hizo na siyo uhalsia wa kile kinachofanyika. Fedha za umma zimekuwa zikitumiwa hovyo kiasi cha kutotambua thamani ya walipa kodi katika Halmashauri husika.
NINATAMBUA kuwa, kwa Mujibu wa Kifungu cha 48(1) cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Namba. 9 ya Mwaka 1982 Sura ya 290 Toleo la Mwaka 2019 ya sheria za Tanzania, imeelekezwa kuwa Hesabu za kila Halmashauri ya Wilaya na za Mamlaka za Miji zitakaguliwa na Mkaguzi wa ndani aliyeajiriwa na mamlaka husika.
Kwa kulitambua hilo na kwa kuthamini nguvu waliyonayo Wakaguzi wa Ndani pamoja na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, ninawaomba waweze kuweka kambi Halmashauri ya Ngara ili waweze kuikagua kabla Baraza la Madiwani halijavunjwa ili kuweza kubaini dosari nyingi ambazo zingine sijaweza kuziainisha hapa ambazo huenda pengine zikaja kuwa sehemu ya matokeo ya Ukaguzi wao.
Zingatia: Kuna Viongozi na Watumishi wa Halmashauri wamejilimbikizia mali, kuna decorations za majengo na miradi inayoripotiwa kwamba imejengwa wakati wamepaka rangi, kuna shida kubwa na nyingi sana Ngara!.
Mapema mwaka huu Halmashauri hii iliwasilisha Rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti kwa Mwaka 2025/2026 huku wadau wengi wa maendeleo ya wilayani hapa wakiwa wamefanikiwa kuipitia vilivyo na kwa upana wake, na mimi nikiwa miongoni mwa wadau hao.
Katika Rasimu hiyo, Kipengele cha Mapitio ya Bajeti kwa Mwaka 2024/2025 iligundulika wazi KUKOSEKANA kwa uwiano kati ya hesabu ya kile kilichoandikwa katika matumizi ikilinganishwa na hali halisi ya kile kinachoonekana Mtaani (vijijini) kwenye UHALSIA.
Lakini pia, wadau tumekuja kubaini kuwa baadhi ya matumizi ya fedha ndani ya Halmashauri zetu huwa hawazingatii thamani ya fedha yaani Value for Money kiasi cha kuweka uwiano kati ya Mradi ulioandikwa na gharama zake na kulinganisha na thamani ya Mradi.
Tumejikuta kwenye Halmashauri zetu tukiwa na Ripoti za Bajeti za Kupikwa na walengwa ili kuwavutia serikali kuu na kule wanapopeleka ripoti hizo na siyo uhalsia wa kile kinachofanyika. Fedha za umma zimekuwa zikitumiwa hovyo kiasi cha kutotambua thamani ya walipa kodi katika Halmashauri husika.
NINATAMBUA kuwa, kwa Mujibu wa Kifungu cha 48(1) cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Namba. 9 ya Mwaka 1982 Sura ya 290 Toleo la Mwaka 2019 ya sheria za Tanzania, imeelekezwa kuwa Hesabu za kila Halmashauri ya Wilaya na za Mamlaka za Miji zitakaguliwa na Mkaguzi wa ndani aliyeajiriwa na mamlaka husika.
Kwa kulitambua hilo na kwa kuthamini nguvu waliyonayo Wakaguzi wa Ndani pamoja na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, ninawaomba waweze kuweka kambi Halmashauri ya Ngara ili waweze kuikagua kabla Baraza la Madiwani halijavunjwa ili kuweza kubaini dosari nyingi ambazo zingine sijaweza kuziainisha hapa ambazo huenda pengine zikaja kuwa sehemu ya matokeo ya Ukaguzi wao.
Zingatia: Kuna Viongozi na Watumishi wa Halmashauri wamejilimbikizia mali, kuna decorations za majengo na miradi inayoripotiwa kwamba imejengwa wakati wamepaka rangi, kuna shida kubwa na nyingi sana Ngara!.