Halima Mdee: Kuna dhamira ya kutaka kumfunga Sugu

Halima Mdee: Kuna dhamira ya kutaka kumfunga Sugu

Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Mhe. Halima Mdee amefunguka na kumuomba Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma kufuatilia mwenendo wa kesi za kisiasa nchini na kudai kuwa baadhi ya mahakimu wamekuwa wakipindisha mambo kwa sababu za kisiasa.




halima%20mdee.jpg

Halima Mdee amesema hayo wakati akiongea na www.eatv.tv na kusema kuwaa Jaji Mkuu anaposema wanasiasa wasiingilie Mahakama hivyo na yeye anapaswa kusimama na kuhakikisha kuwa Mahakimu wakitenda haki na kukemea wale ambao kwa makusudi wamekuwa wakipindisha haki za watu.

"Ni zaidi ya wiki sasa Mhe. Sugu yupo ndani lakini amenyimwa dhamana kwa kosa ambalo linadhaminika kisheria na kiutaratibu kwa muhibu wa sheria zetu kama kosa linadhaminika ni wajibu wa polisi kutoa dhamana na polisi wakikushikilia ndani ya zile saa 48 wakikupeleka mahakamani ni jukumu la Mahakama kufanya hivyo sasa suala la Sugu limeenda Mahakamani ambapo huo ndiyo muhimili pekee ambao tunautegemea . Sasa unapokwenda Mahakamani sehemu pekee ambayo unaitegemea kupata haki halafu unaona hiyo haki haipatikani kwa makusudi kabisa hivyo Jaji Mkuu na yeye anapaswa kuyatambua haya na kuwakemea baadhi ya Mahakimu ambao wanafanya vitu kama hivi" alisema Mdee

Mbali na hilo Halima Mdee amedai kuwa kuna tetesi za kutaka kumfunga Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi “Sugu' kama ambavyo alifungwa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali
Kwa hiyo angepata dhamana ndiyo asingefunwa hata kama ana hatia?
Kama ni njama kaitengeneza yeye ili afungwe, kwa manana hakuna aliyemwambia aropoke
 
Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Mhe. Halima Mdee amefunguka na kumuomba Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma kufuatilia mwenendo wa kesi za kisiasa nchini na kudai kuwa baadhi ya mahakimu wamekuwa wakipindisha mambo kwa sababu za kisiasa.




halima%20mdee.jpg

Halima Mdee amesema hayo wakati akiongea na www.eatv.tv na kusema kuwaa Jaji Mkuu anaposema wanasiasa wasiingilie Mahakama hivyo na yeye anapaswa kusimama na kuhakikisha kuwa Mahakimu wakitenda haki na kukemea wale ambao kwa makusudi wamekuwa wakipindisha haki za watu.

"Ni zaidi ya wiki sasa Mhe. Sugu yupo ndani lakini amenyimwa dhamana kwa kosa ambalo linadhaminika kisheria na kiutaratibu kwa muhibu wa sheria zetu kama kosa linadhaminika ni wajibu wa polisi kutoa dhamana na polisi wakikushikilia ndani ya zile saa 48 wakikupeleka mahakamani ni jukumu la Mahakama kufanya hivyo sasa suala la Sugu limeenda Mahakamani ambapo huo ndiyo muhimili pekee ambao tunautegemea . Sasa unapokwenda Mahakamani sehemu pekee ambayo unaitegemea kupata haki halafu unaona hiyo haki haipatikani kwa makusudi kabisa hivyo Jaji Mkuu na yeye anapaswa kuyatambua haya na kuwakemea baadhi ya Mahakimu ambao wanafanya vitu kama hivi" alisema Mdee

Mbali na hilo Halima Mdee amedai kuwa kuna tetesi za kutaka kumfunga Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi “Sugu' kama ambavyo alifungwa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali
who cares let him face the law
 
Kama kosa lipo afungwe tu kwani yy yupo juu ya sheria afanye makosa na aachiwe kisa mpinzani,katenda kweli uthibitisho upo apewe haki anayostahili tena hiyo kesi ikimbizwe haraka kumuheshimu asipopatikana na hatia aachiwe na akikutwa nayo apate haki yake kama wengine,tushachoka siasa za Maji taka.
 
Kama kosa lipo afungwe tu kwani yy yupo juu ya sheria afanye makosa na aachiwe kisa mpinzani,katenda kweli uthibitisho upo apewe haki anayostahili tena hiyo kesi ikimbizwe haraka kumuheshimu asipopatikana na hatia aachiwe na akikutwa nayo apate haki yake kama wengine,tushachoka siasa za Maji taka.
Chenge na tibaijuka safi!!!
 
Ulichoandika hapa ni mipasho tu hamna hata point


Halima mdee kasema dhamana ipo wazi kwa nn asipewe? Hilo ni swali la kwanza.

Mwanasheria wa serikali kasema yupo ndani kwa usalama wake kapata taarifa atauliwa

Kesi hiyo ilikuwepo toka mwaka jana sugu akiwa nje kakamatwa tarehe 16 je angekufa kabla ya kwenda mahakaman mwanasheria hizo taarifa za usalama wake Angezificha toka kwa watu wasiojulikana waliomwambia na anawafaham? Kwa nini alisubilia had aende mahakama ndo ajali usalama wake wakati alikuwa nje hakujali? Dogo watu wana akili sana achana na michezo ya kitoto ya serikali ya magufuli hata chizi anajua hii michezo ya kijinga

Haya, waache wenye akili wakae ndani!
 
Halima nilidhani umekomaa kumbe bado.
Unajua kesi ipo mahakamani halafu unataka kuaminisha Umma wa Watanzania kuwa Sugu hana hatia? Umejuaje kuwa hana hatia?
Jitahidi utoe hoja zenye mashiko kama mwanasiasa mkomavu. Hoja dhaifu waachie vijana
Kama Sugu anamakosa atahukumiwa tu kwani sheria ni msumeno, lakini kama hana hatia ataachiwa huru.
 
Yaani akiachwa huru hii tabia ya wabunge kujiona wako juu ya Sheria haitakoma, halima mdee tulia dawa iwaingie hii Nchi kwa sasa iko huru sio zama za kikwete matusi ya wanasiasa hayakuwa sehemu ya kosa.

Kwa usawa wa Magu Sheria lazima ifanye kazi, kwa hiyo acha pupa na kuingilia muhimili wa Mahakama wacha ufanye kazi yake .
Hivi mawaziri wapumbavu ni wa awamu ipi?

Kauli ya mfano ya kuigwa! te ,te ,te!

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
KWANI SUGU SI ANAITWAGWA RAIS? KUMBE NI JINA TU HAHAHAHAAA! MNAUTANI NYINYI!!!
 
Sugu usela sana ndio una mcost,alikuwa anahisi anapambana na RUGE.

Lazima Serikali na taasisi ya rais iheshimiwe ata kama umpendi ila kachaguliwa kwa njia ya ki demokrasia.
 
Ingekuwa mtu una fursa ya kuchagua uzaliwe nchi gani na ningechagua kuzaliwa katika nchi hii,ningejilaumu mpaka kufa.

Si ujilipue kama vijana wa Libya wanavyo jilipua kwenda ulaya badala ya kulalamika na kuusononesha moyo wako?
 
Wanataka kumuandalia jimbo naibu wa spika!!
 
Halima nilidhani umekomaa kumbe bado.
Unajua kesi ipo mahakamani halafu unataka kuaminisha Umma wa Watanzania kuwa Sugu hana hatia? Umejuaje kuwa hana hatia?
Jitahidi utoe hoja zenye mashiko kama mwanasiasa mkomavu. Hoja dhaifu waachie vijana
Kama Sugu anamakosa atahukumiwa tu kwani sheria ni msumeno, lakini kama hana hatia ataachiwa huru.
Wewe kada mfurukutwa hujaelewa!! Anazungumzia haki ya dhamana iliyopo kisheria hajasema hana kosa!!
 
Sasa kama ni ujinga kihere here gani kilichokufanya kudandia!Nyie ni mtaji wa CDM endeleeni kutumika,Hizo mahakama anazozisemea huyu zikiwapa haki nyinyi zinakuwa zinatenda haki ila zikitenda haki kwa upande wa serikali mahakama zinaingiliwa lini mtaachaga tabia za kindumilakuwili!
huna akili wewe???? ama ndo nyie mnaotumwa mitandaoni????
 
Yaani akiachwa huru hii tabia ya wabunge kujiona wako juu ya Sheria haitakoma, halima mdee tulia dawa iwaingie hii Nchi kwa sasa iko huru sio zama za kikwete matusi ya wanasiasa hayakuwa sehemu ya kosa.

Kwa usawa wa Magu Sheria lazima ifanye kazi, kwa hiyo acha pupa na kuingilia muhimili wa Mahakama wacha ufanye kazi yake .
Mkuu sasa hivi upo salama Kama upo CCM
 
Back
Top Bottom