Halima Bulembo: Bunge si lazima kuonekana live

Halima Bulembo: Bunge si lazima kuonekana live

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Halima Bulembo anasema anaunga mkono bunge kutorushwa live na kusema kurushwa live bunge kuna faida kwa wabunge wakongwe pekee.

"Nashangaa kumuona Mbunge kama Mbowe mwenye umaarufu mkubwa anataka aonekane 'live' bungeni, wakati hata mdogo wangu wa miaka sita anamfuhamu vizuri, wabunge vijana ndiyo waliopaswa kulalamikia hili,"

Kama mwananchi wa kawaida unapenda kumwambia nini mbunge huyu
87613147d1f35505f5a4bb3c1e96a63b.jpg

chanzo EAST AFRICA RADIO
Mkuu haijawah kutokea dunani mbuzi akazaa binadamu,hivyo basi huyu mbunge anatabia zote za baba yake,yule mgogo
 
huyu ni wa kumsamehe bure, hata ubunge wa viti maalumu aliupata kwa kupitia kwa baba yake Abdallah Bulembo aliyekuwa kampeni meneja wa Raisi Magufuli. Kwa hiyo ni lazima ataongea kama wanavyotaka waliompa ubunge
Tumekuelewa sana kiongozi ubarikiwe sana
 
Huyo ni asante baba na Magufuli mlimtegemea asemeje wakati anahitaji na kipindi cha pili?Pia hayuko mwenyewe wapo na kina Msukuma wa Geita anaeshukuru bunge kutoenda live eti wananchi wa jimbo lake walikuwa wanahangaika kuwasha majenerator kuangalia bunge sasa wataenda mashambani kufanya kazi.Hajiulizi ni kwa nini hao wananchi walikuwa wanahangaika kuyawasha hayo majenerators kuangalia bunge live ilihali mashamba ya kulima yakiwepo.Haoni kuna walichokua wanakikosa na kugharamikia hayo majenerator.
Sijui wananchi wa huko geita kama walitafakari kabla ya kumchagua huyo msukuma
 
Siyo yeye tu wabunge wengi humu bungeni ni mizigo hasa hawa wa kuteuliwa, wanakwenda kulinda maslahi yao peke yao na ya waliowachagua. Hii si kwa CCM tu hata upinzani ndiyo maana kwa hili nampenda Zitto kabwe maana yeye hajali kuitwa msaliti pale anapoona kuna ukweli lakini watu walioelimika kama kina Tundu Lisu nao wananaswa katika mtego kama huu hata wale wa CCM walioelimika wanakisemea chama chao CCM bila kujali kama ni kwa manufaa ya umma ama manufaa ya CCM na kundi la majambazi. Demokrasia tanzani ni ya ujanja ujanja tu. Taabu sana ndiyo maana wakati mwingine nashangaa hata sisi wananchi tunaingia katika mkenge wa vyama vyetu ku support kila ujinga ili mradi unatoka katika midomo ya watu wenye itikadi moja na sisi utadhani ni lazima kuunga kila neno analosema Magufuli ama Mbowe tunajisahau kuwa sisi ndiyo mabosi wao hao wanasiasa.

Mkuu sisi ni Watwana na hao uliowataja ni mabosi wetu ukibisha omba kukutana nao leo ay kesho,kama mta-meet
 
Hahaha CHADEMA ni CHADEMA tu mmoja akienda na wote wanafuata alianza Nape na kila mwana CCM lazima afate inakera sana
 
Ni kweli ni mtoto wa bhurembo jamaa alikuwa anauza urembo enzi hizo si unajua ukiuza urembo lazima upate mrembo ndo maana kazaa mrembo. Lakini kichwani... Mtanisaidia si mnakumbuka kauli tata za mshua wake kipindi cha kampeni. Wapinzani tunaweza kuwapa vyote lakini si IKURU ndo alivyoitaja IKURU
 
wewe umeathirika vipi bunge kutorushwa, ebu onesha kiasi ulicho athirika. husifanye vitu kwa kufuata mkumbo
 
Nashukuru sana Mungu kwetu hawachaguagi wabunge wa aina hii. Wabunge kama hawa ni msiba mzito kwa taifa na inaonesha jinsi IQ ya watu wetu ilivyo chini pia ni ushaidi jinsi elimu yetu ilivyoshindwa kufuta ujinga kwa baadhi ya watu kama huyu mheshimiwa mbunge
 
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Halima Bulembo anasema anaunga mkono bunge kutorushwa live na kusema kurushwa live bunge kuna faida kwa wabunge wakongwe pekee.

"Nashangaa kumuona Mbunge kama Mbowe mwenye umaarufu mkubwa anataka aonekane 'live' bungeni, wakati hata mdogo wangu wa miaka sita anamfuhamu vizuri, wabunge vijana ndiyo waliopaswa kulalamikia hili,"

Kama mwananchi wa kawaida unapenda kumwambia nini mbunge huyu
87613147d1f35505f5a4bb3c1e96a63b.jpg

chanzo EAST AFRICA RADIO

Elimu anayo mkuu. Hawa kwao ni wasomi sana. Baba yake ni alhaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom