mtima nyongo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 1,947
- 2,047
Pamoja na maonyo ya watu wazima ya kwamba mgonjwa wetu yu mahututi hata mkimpa dawa ni sawa na kujisumbua maana ile pumzi ya uhai imeshakata.
Lakin kwa kuwa bado tulikua na imani na mgonjwa wetu na bado tulimhitaji ikatubidi tuwe na kichwa ngumu na kutosikiliza maneno ya watu wazima.
Tukampa dawa ili angalau asogeze siku za kuishi japo hata miaka 5 lakini naona kama tulimzidishia dozi maana aliinuka kwa sipidi sana na muda mwingne wanandugu tukapata matumaini ya kwamba sasa mgonjwa wetu kapona.
Lakini hata mwaka aujaisha toka tumpe dawa naona ameanza kulegalega kila uchwao sasa sijui kama tutafika nae hiyo miaka mitano au ndio atatufia njiani sijui ila ni maombi tu ndio yanahitajika kwa sasa wananzengo.
Lakin kwa kuwa bado tulikua na imani na mgonjwa wetu na bado tulimhitaji ikatubidi tuwe na kichwa ngumu na kutosikiliza maneno ya watu wazima.
Tukampa dawa ili angalau asogeze siku za kuishi japo hata miaka 5 lakini naona kama tulimzidishia dozi maana aliinuka kwa sipidi sana na muda mwingne wanandugu tukapata matumaini ya kwamba sasa mgonjwa wetu kapona.
Lakini hata mwaka aujaisha toka tumpe dawa naona ameanza kulegalega kila uchwao sasa sijui kama tutafika nae hiyo miaka mitano au ndio atatufia njiani sijui ila ni maombi tu ndio yanahitajika kwa sasa wananzengo.