Hali ya barabara ya Dumila - Handeni - Korogwe, Je ni barabara ya lami au vumbi?

muuza ubuyu

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
3,511
3,477
Habari wakuu,

Mwezi wa kumi na moja nina safari ya kwenda Lushoto kwa kutumia usafiri binafsi. Kiufupi mimi ni mgeni katika mkoa wa Tanga na sijui hali ya barabara mkoani humo. Ninaishi kwenye moja ya mikoa ya kanda ya magharibi mwa Tanzania.

Barabara ninayotaka kutumia ni ile ya kutoka Dodoma kwenda Morogoro. Ningependa kupita njia fupi pindi nitakapofika Dumila, yaani nitumie barabara ya Dumila - Handeni - Korogwe (wastani wa kilomita 230 kwa mjibu wa google map).

Kwa wenyeji wa mkoa huu au wale waliowahi kutumia barabara hiyo, ningependa kupata maelekezo yenu yatokanayo na uzoefu wenu, je barabara hii Dumila - Korogwe ni lami? Kama ni ya vumbi, inapitika wakati wa masika?

Asanteni sana.
 
Siungewauliza "google map" kama walivyokwambia kilometa wangekwambia pia na hali ya barabara ilivyo

Maswali mengine yanachosha "hakili" na roho
 
Habari wakuu,

Mwezi wa kumi na moja nina safari ya kwenda Lushoto kwa kutumia usafiri binafsi. Kiufupi mimi ni mgeni katika mkoa wa Tanga na sijui hali ya barabara mkoani humo...
Nakushauri tumia barabara ya Chalinze-Korogwe-Lushoto chief, Barabara hii ina kipande cha vumbi kutoka Turiani hadi Handeni na wakati wa Masika siyo rafiki sana
 
Kipande cha Dumila ~ Turiani kina lami safi sana. Kutoka Turiani kwenda Handeni ni km 99 ni raugh road barabara ya vumbi, kuna sehemu nzuri na kuna sehemu mbovu. Hii barabara ina Mkandarasi lakini yupo very slow, na kuna maeneo anajenga madaraja. Sikushauri upite hasa kama una gari ndogo la chini, labda kama una gari kubwa Design ya prado au Harrier unaweza kupita ingawa spidi yake haitazidi 60 kwa ile barabara.

Barabara hiyo ya vumbi haina kona kali kama mdau hapo juu alivyosema. Ukifika Handeni Mjini kwenda Korogwe ni barabara ya lami ingawa ile lami ina matuta mengi mno.

Kutokea Korogwe kufika Mombo ni mkeka, kutoka Mombo kufika Lushoto ni lami. But lami hii uwe nayo makini sana, Lushoto ni milimani, barabara ni nyembamba na ina sharp corner Na Ni Milimani mwanzo mwisho. Kuna sehemu nyingi hamuwezi kupishana hivyo wakati unapandisha ukiona gari[lori] inashuka ni vizuri gari yako isimame pembeni mpaka lori lipite ndipo uendelee na Safari. Hii ni caution kwa dereva mgeni, always stay on your side, usikae katikati ya barabara.

Kutoka Mombo to Lushoto ni km 38 tu lakini driving yake ni 1hr+, so you can feel it.

Ukifika Lushoto nicheki nikupeleke kidimbwi, uwe na Safari njema in advance.
 
Nakushauri tumia barabara ya Chalinze-Korogwe-Lushoto chief, Barabara hii ina kipande cha vumbi kutoka Turiani hadi Handeni na wakati wa Masika siyo rafiki sana
Chalinze kote huko Kwa nini?

Dar-Bagamoyo-Msata-Korogwe-Kushoto
 
Asante mkuu, Dumila to Turiani ni km ngapi?

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Kipande cha Dumila ~ Turiani kina lami safi sana. Kutoka Turiani kwenda Handeni ni km 99 ni raugh road barabara ya vumbi, kuna sehemu nzuri na kuna sehemu mbovu...
Asante sana kiongozi kwa maelezo yaliyojaa nyama za kutosha! Uzuri gari langu ni Harrier hivyo inaweza kupita rough road sema tu comfortability baada ya kuendesha safari ndefu kwenye lami inapungua na inahalibu ladha ya safari.

Nitaona muda ukifika na ukizingatia msimu huu TMA nao wanasema kuna el nino sasa sijui kama haitakuwa na shida sana hasa hivyo vipande vya vumbi.

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Umemuingiza chaka vibaya mno mwenzako🤣🤣🤣🤣
 
Asante sana kiongozi kwa maelezo yaliyojaa nyama za kutosha! Uzuri gari langu ni Harrier hivyo inaweza kupita rough road sema tu comfortability baada ya kuendesha safari ndefu kwenye lami nadhani inahalibu ladha ya safari...
OK most welcome, mvua zikianza achana na hiyo barabara, pitia Morogoro road via Msolwa Lugoba Msata Mkata Segera Korogwe Mombo Lushoto
 
Back
Top Bottom