Hali ni mbaya, waziri Bashe chukua hatua

Hali ni mbaya, waziri Bashe chukua hatua

ilikuaje akawa Waziri huyu, Mtu ana asili ya Somalia ameoa mwenye asili ya Rwanda na anaingia baraza letu la Mawaziri akishikilia wizara uti wa mgongo wa Taifa
Angalia akili za maharage hizi , ukabila tuu na uchawi tuu ndio mnachoweza halafu mnataka maendeleo
 
Unaijua composition ya wananchi waliopo Dar es Salaam na vipato vyao? unaijua hali ya vipato vya wananchi wa kawaida hapa nchini, achilia mbali Dar........au ukishajiona wewe unaweza kununua kilo 4000/- basi huna habari na maisha ya wananchi walio wengi.........

You are too senseless my friend, hata huko ulaya kwenye majiji yaliyoendelea kuna regulatory bodies kuangalia bei za bidhaa muhimu kama vyakula viwe affordable kwa watu wengi hata kama kuna matajiri wenye uwezo wa kununua vyakula vyote kwa bei yoyote ile.
Nyie mumekimbia mashamba Kazuramimba na Nangurukulu, mumekuja Dar es Salaam halafu unataka uishi maisha kama ya huko swekeni kwenu? It is impossible!! Msioweza kumudu maisha ya jiji pungukeni rudini kijijini mkalime. Hii kazi ya kuuza karanga na mayai mjini haiwapeleki popote
 
We chawa aliye kuambia Kuna maisha mepesi ni Bashe?
Njoo na hoja za kujenga siyo kuwaita watu chawa. Raia kama wewe ndiyo mnafanya maisha yawe magumu Tanzania. Unamuandama Waziri wakati mwenyewe umetoka huko bara umekuja kuishi kwenye nyumba ambayo dada yako ameolewa. Unasubiri shemeji are ampe hela dada yako na dada yako akugawie. Lazima uone bei ya mchele iko juu.
 
Mnapiga kelele tuu bila data, kwa taarifa yenu Tanzania haijawahi kujitosheleza kwa chakula kwa kutegemea mkulima wa ndani, miaka yote hakuna njaa kwa sababu tunaagiza kutoka nje, kinachofanyika ni wamezuia uagizaji ili kumsaidia bei mkulima wa ndani lakini inaonekana wahusika wameshindwa kufanya balance inayotakiwa ndio maana soko linayumba, dunia haijaishiwa chakula kipo kingi tuu ni swala la kuagiza na kwa teknoloji tunayotumia kulima, chakula cha nje ni bei nafuu kuliko tunacholima, ni siasa ndio zinafanya yote haya ila chakula kipo
 
Mkuu unataka bei ishuke ili sisi tuliolima tupate hasara
Bei inatakiwa ikae hapo hapo ilipo ili mavuno yakichanganya ishuke kidogo alafu itapanda tunauza mazao yetu tupate faida
Tunatumia mbolea wakati wa kilimo,tunashinda mashambani jua na mvua zinatunyeshea leo unamuomba waziri aangalie bei inakuaje,tulia tu mkuu hiyo ni ishara ya neema kwa wakulima kila mtu anufaike na anachokifanya ..
 
Hao wanaokupinga ni kawaida yao, walishajipanga humu jukwaani......kila ukianzishwa uzi wa namna hii wanakuja kumshambulia mtoa mada wakisema wanamtetea mkulima. Lakini ukifuatilia wengi wanakuwa ni madalali na walanguzi wa mazao ambao wanajificha kwenye kichaka cha kumtetea mkulima.

Wakulima tunaowajua huwezi kuwakuta huku JF hasa kipindi hiki cha mavuno.
Wakulima wa Sasa ni watu wapo sana jamiiforum, Hivi Kweli mtu mwenye akili Timamu anaweza kusema mkulima apangiwe Bei na mtu mwengine? Hivi nyie mnafahamu gharama za mbegu Kwa kG? Unajuwa Bei ya mbolea ya DAP, urea can, s/a, Bei ya Disiel? Unajuwa Bei ya viwatilifu? Gharama za kupalilia Shamba? Gharama za kuvuna? Kupukucha? Kubeba kutoka Shambani? Bei ya viroba? Unajuwa mabadiliko ya Tabia nchii yanavuowasiri wakulima kupunguza mavuno mashambani.
Sasa Kwa taarifa tu gharama za Gunia Moja Kwa mkulima ni zaidi ya Tshs 65000/ mkulima anadubiri zaidi ya miezi Saba ndio apate Hela, Mkulima ni lazima auze Mahindi ndio chanzo pekee anachokitegemea Alipe ada za watoto, matibabu , nguo, kujenga, Kununuwa pembejeo maandalizi ya Kilimo.
 
Dkt Mwijuma na wapumbavu wenzio, toka hapa JF nenda ukalime uone mkulima anavyoteseka kuliko kupoteza MBs humu kuandika utumbo.

Mkulima wa Tanzania asipangiwe bei na mtu yeyote!! Unataka bei ziterrmke ili iweje?

Kuanzia mwaka juzi toka Hussein Bashe awe Waziri wa Kilimo alisema muache mkulima amuuzie mtu anayempa bei nzuri!! Nashangaa badala ya kwenda kulima mchangamkie fursa ya bei nzuri instead mnataka kurudisha maisha ya wakulima nyuma.

Wacheni UJINGA
Shangaaa na wewe,yaani mvua zinanyesha wewe uko mjini umechomekea unasubili bei zishuke ili ufaidike thubutu
 
Hao wanaokupinga ni kawaida yao, walishajipanga humu jukwaani......kila ukianzishwa uzi wa namna hii wanakuja kumshambulia mtoa mada wakisema wanamtetea mkulima. Lakini ukifuatilia wengi wanakuwa ni madalali na walanguzi wa mazao ambao wanajificha kwenye kichaka cha kumtetea mkulima.

Wakulima tunaowajua huwezi kuwakuta huku JF hasa kipindi hiki cha mavuno.
Sisi wakulima wa jamiiforum tunasema hivi Dr mzima unashindwa kuwa na ufahamu mdogo tu wakujuwa Demand na Supply ndio vinaamus Bei ya bidhaa Sokoni??
Unashindwa kuona viashria mapema kuwa bidhaa za kilimo zitapanda Bei Sokoni Kwa kuangalia Factors of production zimeongezeka Bei mfano Swala Disiel, vita vya Russia / Ukraine hai ni wazalishaji wakubwa wa ngano, Mafuta ya kula, Disiel, mbolea, Dr. Unashindwa kujuwa kuwa chanzo Cha Bei ya Mazao ya Chakula kuwa Juu sababu mojawapo ni kutegemea mvua na kutokuwa na mioundo mbinu na umwagiliaji, Nilitegemea mtu mwenye Elimu kiwango Cha Dr aje na majibu ya kuongeza uzalishani mbegu Bora, Nilitegemea Dr ushauri serikali ifanye kitu Gani Eli uzalishani uongezeke na gharama za uzalishaji zipungue. Ila piya sishangae sana wewe kuitwa Dr inawezikana ikawa ni Dr wa mtaani sio Dr wa
taaluma.
 

Attachments

  • IMG_20230122_174242_340.jpg
    IMG_20230122_174242_340.jpg
    818.4 KB · Views: 20
Mkuu nadhan ww utakuwa ni motivation speaker unaongea lugha laini sana, hiyo laki 2 ongea na mtu ambaye ana eneo tayari sio huyu ambae hana lazima akodi kutoka kwa mmiliki, watu wanakwepa kufanya vitu vinavyohitaji uwekezaji mkubwa,, kilimo sio kigumu wala kama unavyosema mm naamini ugumu upo kwenye mtaji

Mjini kazi ni ngumu kupita maelezo, mji kama Dar watu wanaamka saa 11 alfajiri na kulala saa 7 usiku mwaka mzima,, niambie ni kijiji gani watu wanaishi hivii? Mtu anapandisha juu ghorofa ya tano kifusi cha mchanga kilichomwagwa na lori (mende), hesabu kilometa anazotembea machinga kwa siku hawa hawashindwi kufanya kilimo bali hawana mitaji

Lkn jambo la msingi na ndio lengo la uzi huu serikali iangalie ni namna gani ya ku-balance bei za mazao bila kuathiri soko (walaji) na pia mkulima,, hatuwezi kulima wote na hata tukilima wote tutamuuzia nani ikiwa kila mtu ana mazao?
Sekta zote zinatakiwa zifanye kazi,, mda huo ww unalima kuna utalii, uchimbaji madini, uvuvi nk
Mjini Manisha ni simple Kwa nyie mliouza muda wenu na kutumikishwa, wewe Kila mwisho wa mwezi unapata mshahara, ila mkulima anakaa miezi Saba akiwa anafanya kazi usiku na mchana, mchana juani Usiku analinda wanyama Wakali Kuna maeneo Tembo ni kero, mkulima anakaa kwenye baridi Shambani, snakunywa Maji ya mitaroni huko mashambani, nyoka Wakali wenye sumu, wezi, Wewe upo kwenye kiyoyozi unakula Raha huku ubunifu na utemdaji ukiwa mbovu Bado wanakulipa mshahara wako, Kama Kulima eahisi njoo nikupe Shamba Bure ulime ila sharti acha kazi uone kilimo kilivyo. Sio wote wanaolima hawajasoma, wamesoma na kufanya hizo kazi za kukariri madesa wakamua kuwacha nakuingia kwenye kilimo
 
Ulichokisema Ni sahihi, hali ya bei ya chakula bado sio nzuri,na kusema kwamba mkulima anafaidika nadhani si wakulima wote,asilimia kubwa ya wakulima wa Tz ni wakulima wadogo wadogo,na hao ndio wanalisha nchi kwa kiasi kikubwa,swala la bei ya mazao kuwa nzuri si kweli kwamba wanafaidika nayo,wanaofaidika sanasana ni walanguzi na wakulima wa kubwa,mkulima mdogo akivuna anahifadhi kidogo kwa ajili ya chakula kingine anauza kwa walanguzi kwa bei ya kawaida, na mwisho wa siku mkulima huyo huyo akiishiwa chakula anakuja kununua kwa bei kubwa sana, kwahiyo ili swala liangaliwe upya, wachache sana ndio wanaofaidika wananchi wengi wanabaki wanaumia na mfumuko wa bei ya chakula
  • Wakulima tunanufauka na bei nzuri. Baki na akili za kizamani.
  • Wakulima tunaodharaulika kwa sasa tunalima na kuboresha makazi (nyumba za ramani n.k) na kuboresha kilimo.
  • TARURA wameboresha barabara na walanguzi toka hata nje wanafika chocho kabisa kutafuta mazao.
  • Endeleeni kuuza makorokocho ya mchina mkidhani kuna maksai zenu zinawalimia kijijini. KILA MTU ASHINDE MECHI ANAYOWEZA!
 
N muda wa wakulima kutajirika...vjn wapo mjn wanauza vwembe hawatak kulima...serikali isiingilie swala hili...atakayekufa njaa na afe... BASHE ALISEMA KBS HAWATAINGILIA KAT BEI YA MAZAO..watu tumekuwa tukiwekeza kwenye kilimo lkn outcome miaka yote n ndogo achaaa kila mtu ashinde mechi zake...over
Wanaoteseka sana ni hao hao wakulima baada ya kuuza chakura chote ...
 
Sisi wakulima wa jamiiforum tunasema hivi Dr mzima unashindwa kuwa na ufahamu mdogo tu wakujuwa Demand na Supply ndio vinaamus Bei ya bidhaa Sokoni??
Unashindwa kuona viashria mapema kuwa bidhaa za kilimo zitapanda Bei Sokoni Kwa kuangalia Factors of production zimeongezeka Bei mfano Swala Disiel, vita vya Russia / Ukraine hai ni wazalishaji wakubwa wa ngano, Mafuta ya kula, Disiel, mbolea, Dr. Unashindwa kujuwa kuwa chanzo Cha Bei ya Mazao ya Chakula kuwa Juu sababu mojawapo ni kutegemea mvua na kutokuwa na mioundo mbinu na umwagiliaji, Nilitegemea mtu mwenye Elimu kiwango Cha Dr aje na majibu ya kuongeza uzalishani mbegu Bora, Nilitegemea Dr ushauri serikali ifanye kitu Gani Eli uzalishani uongezeke na gharama za uzalishaji zipungue. Ila piya sishangae sana wewe kuitwa Dr inawezikana ikawa ni Dr wa mtaani sio Dr waView attachment 2607686View attachment 2607686 taaluma.
Demand na supply kwenye soko lipi? unaporuhusu mazao kupelekwa kiholela nje ya nchi lazima usababishe uhaba mkubwa nchini.......nchi hii kwa asilimia kubwa imekuwa ikilishwa na wakulima wadogo.

Baada walanguzi kupata upenyo wa kupeleka mazao nje kiholela wanamyonya mkulima mdogo kupitia kubana mizani, kumpa bei ndogo, kupitia lumbesa na kangomba. Mwisho wa siku mkulima hafaidiki na bei kubwa ya soko bali walanguzi wa mazao. Kwa hiyo nchi inaathirika mara mbili, moja mkulima mdogo anaendelea kubaki kwenye hali duni ya kipato, na hapo hapo walanguzi wa mazao wanasababisha mfumuko mkubwa wa bei kwa kusafirisha mazao muhimu ya nafaka kiholela nje ya nchi.​
 
Kama wewe unaona wakulima wanawauzia walanguzi kwa bei ndogo kwa nini na wewe usiende huko kijijini ukanunue kwa bei hiyo ndogo uhifadhi uache kulalamika.
Kama unadhani huku kijijini bei ya mazao kwa wakulima ni chini njoo uje ujionee.
Mfano mchele huku Rukwa ambako ndiyo unalimwa kilo moja ni 3000/
Mahindi huku kijijini yanauzwa kwa 100kg shilingi 70,000/ sasa hapo mkulima anaibiwaje
Hiyo hali imesababishwa na nyinyi walanguzi kupata upenyo wa kusafirisha mazao kiholela kwenda nje, mwisho wa siku huyo mkulima atawauzia mazao yote kwa bei chee na yeye atakuwa mhanga wa njaa baada ya muda kidogo na nyie hao hao mtapata vibali vya kuagiza chakula kibovu kutoka nje ili mumuuzie huyo mkulima ambaye kwa wakati huo atakuwa hana tena mazao na pengine hata pesa ameshamaliza.........yaani mnatengeneza scenario ya hovyo kabisa!​
 
Demand na supply kwenye soko lipi? unaporuhusu mazao kupelekwa kiholela nje ya nchi lazima usababishe uhaba mkubwa nchini.......nchi hii kwa asilimia kubwa imekuwa ikilishwa na wakulima wadogo.

Baada walanguzi kupata upenyo wa kupeleka mazao nje kiholela wanamyonya mkulima mdogo kupitia kubana mizani, kumpa bei ndogo, kupitia lumbesa na kangomba. Mwisho wa siku mkulima hafaidiki na bei kubwa ya soko bali walanguzi wa mazao. Kwa hiyo nchi inaathirika mara mbili, moja mkulima mdogo anaendelea kubaki kwenye hali duni ya kipato, na hapo hapo walanguzi wa mazao wanasababisha mfumuko mkubwa wa bei kwa kusafirisha mazao muhimu ya nafaka kiholela nje ya nchi.​

Nenda kanunue kwa bei ndogo kama hao walanguzi halafu uhifadhi kwaka mzima kwa ajili ya kula mwenyewe
 
Back
Top Bottom