Tangantika
JF-Expert Member
- Aug 12, 2018
- 5,806
- 7,414
Kuwasaidia watu kwa kumuumiza mtu ni dhambi. Mazao yangu haujanisaidia kwa lolote vipi uyapangie.Kwanza mimi hakuna sehemu nimemtukana mtu hapa, naamini kwenye kujadili jambo kwa hoja haijalishi mtu kaleta hoja inayokinzana nitajibu kwa hoja na sio kutoa matusi
Pili kilimo ni sehemu ya maisha yangu, naamini kushiriki kilimo sio lazima nikalime hata nikikuletea pembejeo kuzitoa mjini kukusogezea kujijini nitakuwa nimeshiriki kilimo
Lengo la huu uzi sio kumuathiri mkulima kwenye suala la bei no, nilikuwa nawasilisha hoja kuhusu uhaba/uchache wa mavuno msimu huu serikali idhibiti soko mazao yasiuzwe yote kwa haraka soko la nje ilihali soko la ndani bado linauhitaji
Chakula kilichopo hakitoshi kwa humu humu ndani vipi tena kiende nje,, serikali ifunge mipaka kiuzwe hapa pekee
Harafu narudia tena hatuwezi kulima wote mkuu, unataka walimu, madaktari, mapolisi, wavuvi, wahandisi, wafanyabiashara watu wa madini na utalii wote waende shamba?
Ishauri serikali inunue kwa bei ya soko halafu ije iuze chini ya bei ili iwasaidie masikini wasiotaka kufanya kazi wanaozurura tu mijini.