Hali ni mbaya ward A na B za watoto walioko MOI (Muhimbili)

Muumbuaji

Member
Aug 24, 2016
70
84
Asubuhi ya leo nimetoka kumuona mgonjwa katika wodi ya watoto waliovunjika mifupa iliyopo Muhimbili chini ya taasisi ya MOI. Nilichokikuta kinasikitisha sana, na nilichosimuliwa na wazazi/walezi wanaowatazama watoto hao kinasikitisha zaidi

Nilichoona:
Vitanda vyote 23 katika wodi A vina wagonjwa wawili wawili, yaani maana yake kuna wagonjwa 46. Ukubwa wa wodi kwa uzoefu wangu wa metric units, ni 6m x 18m = 108 sq. metres

Kwa lugha ya ujumla, chumba chenye eneo la mita za mraba 108 kinatumika kuwalaza watoto 46, na hapo bado waangalizi wao wanaoshinda nao, ambao nao wapo 46, kufanya jumla ya msongamano wa watu 92 ndani ya kaeneo hako! Hapo nimeamua kuneglect watu wanaofika na kuondoka kwa lengo la kuwaona wagonjwa, kama mimi. Hiyo ni hali ya population density ambayo niliiona kwa macho yangu

Nilichosimuliwa:
Mzazi wa mtoto niliyeenda kumuona pamoja na mzazi wa mtoto mwezie wanaoshea kitanda, wamenieleza jinsi huduma ya hovyo inavyotolewa. Daktari anapopita hamuangalii mgonjwa na kutumia utaalamu wake kujua hali yake, bali anamuuliza muangalizi kuwa mgonjwa anaendeleaje, chochote atakachosema muangalizi ndicho hicho daktari anaandika na kuondoka kwenda kitanda kingine!

Hana muda wa kuangalia kiungo cha mtoto kilichovunjika kinaendeleaje, bali anatumia maelezo ya muangalizi pekee, halafu wala hachanganyi utaalamu wake, anaandika na kuondoka. Dada wa pembeni akalalamika kuwa ameambiwa asaini document ambayo hajui inahusu nini, na kwa kutumia udhaifu wa uelewa wa watu wetu, daktari/muuguzi amemsainisha tu.

Watoto wamewekewa mawe yananing'inia tu, hawapewi dawa yoyote! Jamani hakuna siasa hapa, waliopo Dar waende wodi ya watoto waliovunjika viungo leo hii wakafanye mahojiano hata kwa siri siri, halafu waje tuone kama kuna kuongeza chumvi au ndio hali iliyopo!

Wito:
Serikali iachane na siasa katika afya za wanadamu wananchi wake. Wataalamu wanaposema kuna upungufu wa vifaa,rasilimali watu au miundombinu ya hospitali, hatua za kurekebisha zichukuliwe, au walau watu waambiwe ukweli ili wajipange na wagonjwa wao kukabiliana na hali ya hospitalini. Wagonjwa wanaposema kuna uzembe wa wafanyakazi, hatua zichukuliwe. Hakuna haja ya kubishana kwenye vyombo vya habari kuficha uovu

Karibuni Muhimbili wodi ya watoto waliovunjika viungo, nyuma ya wodi ya Sewa Haji

cc: HKigwangalla
 
Si waziri kasema nchi haina tatizo la huduma za afya? Huu utakuwa uchochezi. Haiwezekani kutumia mitandao kuipinga serikali! ;););):(:(
 
NB: Nilitaka nichukue picha lakini nafsi ikanisuta. Pamoja na nia yangu njema ya kutolea taarifa, lakini nikajiuliza kuwa kwa upande mwingine, hawa wauguzaji wanaweza wasijisikie vizuri kuchukuliwa picha katika mazingira hayo. Lakini nasisitiza, kwa aliyepo Dar, awe kama vile anapita tu, aingie ward hiyo ajionee
 
Asubuhi ya leo nimetoka kumuona mgonjwa katika wodi ya watoto waliovunjika mifupa iliyopo Muhimbili chini ya taasisi ya MOI. Nilichokikuta kinasikitisha sana, na nilichosimuliwa na wazazi/walezi wanaowatazama watoto hao kinasikitisha zaidi

Nilichoona:
Vitanda vyote 23 katika wodi A vina wagonjwa wawili wawili, yaani maana yake kuna wagonjwa 46. Ukubwa wa wodi kwa uzoefu wangu wa metric units, ni 6m x 18m = 108 sq. metres

Kwa lugha ya ujumla, chumba chenye eneo la mita za mraba 108 kinatumika kuwalaza watoto 46, na hapo bado waangalizi wao wanaoshinda nao, ambao nao wapo 46, kufanya jumla ya msongamano wa watu 92 ndani ya kaeneo hako! Hapo nimeamua kuneglect watu wanaofika na kuondoka kwa lengo la kuwaona wagonjwa, kama mimi. Hiyo ni hali ya population density ambayo niliiona kwa macho yangu

Nilichosimuliwa:
Mzazi wa mtoto niliyeenda kumuona pamoja na mzazi wa mtoto mwezie wanaoshea kitanda, wamenieleza jinsi huduma ya hovyo inavyotolewa. Daktari anapopita hamuangalii mgonjwa na kutumia utaalamu wake kujua hali yake, bali anamuuliza muangalizi kuwa mgonjwa anaendeleaje, chochote atakachosema muangalizi ndicho hicho daktari anaandika na kuondoka kwenda kitanda kingine!

Hana muda wa kuangalia kiungo cha mtoto kilichovunjika kinaendeleaje, bali anatumia maelezo ya muangalizi pekee, halafu wala hachanganyi utaalamu wake, anaandika na kuondoka. Dada wa pembeni akalalamika kuwa ameambiwa asaini document ambayo hajui inahusu nini, na kwa kutumia udhaifu wa uelewa wa watu wetu, daktari/muuguzi amemsainisha tu.

Watoto wamewekewa mawe yananing'inia tu, hawapewi dawa yoyote! Jamani hakuna siasa hapa, waliopo Dar waende wodi ya watoto waliovunjika viungo leo hii wakafanye mahojiano hata kwa siri siri, halafu waje tuone kama kuna kuongeza chumvi au ndio hali iliyopo!

Wito:
Serikali iachane na siasa katika afya za wanadamu wananchi wake. Wataalamu wanaposema kuna upungufu wa vifaa,rasilimali watu au miundombinu ya hospitali, hatua za kurekebisha zichukuliwe, au walau watu waambiwe ukweli ili wajipange na wagonjwa wao kukabiliana na hali ya hospitalini. Wagonjwa wanaposema kuna uzembe wa wafanyakazi, hatua zichukuliwe. Hakuna haja ya kubishana kwenye vyombo vya habari kuficha uovu

Karibuni Muhimbili wodi ya watoto waliovunjika viungo, nyuma ya wodi ya Sewa Haji

cc: HKigwangalla
Kazi ya kuhudumia wagonjwa ni ya wito. Unapokuta dakitari anapita bila kumcheki mgonjwa ujue hakuna madili kwa mhusika na pia hajali kazi yake. Najua vijana wengi wanaosomea udakitari kwa sasa wanawaza kutoka na siyo kuutumia utaalamu wao kutatua changamoto, bali kila kijana anawaza anunue BMW, anawaza ajenge gorofa, anawaza awazidi wenzake.

Kuhusu vifaa kwa kweli nadhani ni janga la kitaifa, ni tofauti sana na nchi za wenzetu.
 
Hizo wodi za muhimbili & Moi hiyo ni kawaida sana mkuu,madaktari siku zote hawana muda wanawahi kazi binafsi ..........Ukiwa mgonjwa ndio utajua tabia ya madaktari na manesi hasa ukiwa umelazwa.Tuombe mungu
 
Kama mgonjwa aliyevunjika mguu na amekuwa immobilized au amewekewa traction daktari halazimiki kugusa kiuongo husika mara kwa mara, kwa sababu anaweza Ku disturb mfupa na kuchelewesha kupona, hivyo daktari anauliza tu kama kuna tatizo lolote lililojitokeza kwa mfano, homa, kukohoa, kuharisha n.k.
 
Mkuu we sio mchochezi kweli.......teh teh........
Bahati mbaya maslahi pekee ninayoweza ku'declare katika uzi huu ni uzalendo. Niliyeenda kumuona ni mtoto wa jirani yangu. Sina haja ya kufanya uchochezi, na ndio maana nikatoa wito kwa watu wenye sauti zaidi yangu waipaze huko juu, maana kwa hali ie, mtu anaenda kutibiwa lakini ajiandae pia kuambukizwa!
 
Kama mgonjwa alivunjika mguu na amekuwa immobilized au amewekewa traction daktari halazimiki kugusa kiuongo husika mara kwa mara, kwa sababu anaweza Ku disturb mfupa na kuchelewesha kupona, hivyo daktari anauliza tu kama kuna tatizo lolote lililojitokeza kwa mfano, homa, kukohoa, kuharisha n.k.
Hata kumuangalia kwa macho pia itadisturb? Kulala wawili wawili je?
 
Ndg samahani.
Hapo tatizo ni msongamano , Huduma mbovu , wanaouguza kutojua kinachoendelea?
MTU aliyevunjika mguu anatakiwa kupewa dawa gani? Ni open fracture?, wamekaa muda gani?
Ukienda tena jaribu kuzungumza na mtoa Huduma. Majibu yake huenda ukajua namna ya kumsaidia mgonjwa wako.
Overcrowding inategemeana na rate ya ajali na uwezo was hospital husika kufawafanyia operation wale wanaotakiwa kufanyiwa.
IPO haja ya kuwa na taasisi nyingine kubwa ya mifupa yenye hadhi ya MOI... (Iwe Dodoma au iringa au mbeya) ili kupunguza msongamano huo
 
Niliwahi kuzungumza juu ya hili takribani miezi mitatu iliyopita baada ya kumtembelea ndugu yangu aliyelazwa hapo nilichokiona kinafanana na maelezo ya mtoa mada. Sioni serikali ilichokifanya mpaka hivi sasa. Zile kambi za madaktari zilizokuwa zikihudumia wagonjwa pale Moi hazipo tena. Nilipohoji sababu za kutokuwepo nikajibiwa ni ukosefu wa vifaa tiba na posho walizokuwa wakipata madaktari. Mimi naona serikali inafanya mchezo kwenye afya za watu wake siasa zimezidi mfano hivi sasa dawa hakuna na lilipigiwa kelele dalili zilipoanza ku onekana lakini serikali ikakanusha sasa ukweli unadhihirika
 
Yeye anaangalia ila huwezi kujua kama anaangalia, kulala wawili wawili sio ishu ya madaktari au manesi, hiyo ni ishu ya Wizara husika
Na mimi wala sijaelekeza jumba bovu kwa madaktari pekee, bali kwa yeyote anayewajibika katika eneo linalomuhusu
 
Daktari au nurse hawezi kumfukuza mgonjwa kwamba pamejaa.
Ni guest au lodge tu utakuta vibao vya Nafasi IPO au Pamejaa.
Issues hapo ziko nyingi.... Ajali za boda boda ambazo kimsingi havipaswi kuwa vyombo vya usafiri..na kauli za viongozi wetu " Tuwaache vijana wetu wanajitafutia riziki"
 
Msitubabaishe. Tunatekeleza ilani ya ccm. Suala mojawapo ni kufufua shirika la ndege, ATCL.

Dia Bomba hoyeeee! Na ndege zingine zinakuja.

Ebo! Mie sio mchochezi.
 
Daktari au nurse hawezi kumfukuza mgonjwa kwamba pamejaa.
Ni guest au lodge tu utakuta vibao vya Nafasi IPO au Pamejaa.
Issues hapo ziko nyingi.... Ajali za boda boda ambazo kimsingi havipaswi kuwa vyombo vya usafiri..na kauli za viongozi wetu " Tuwaache vijana wetu wanajitafutia riziki"
Nazungumzia wodi ya watoto waliovunjika viungo, sizungumzii waendesha bodaboda kwani wao ni wakubwa na wala sijawahi kuingia kwenye ward yao
 
Hizo wodi za muhimbili & Moi hiyo ni kawaida sana mkuu,madaktari siku zote hawana muda wanawahi kazi binafsi ..........Ukiwa mgonjwa ndio utajua tabia ya madaktari na manesi hasa ukiwa umelazwa.Tuombe mungu
Mkuu ukweli hausemwi tu ila watumishi wengi (sio wote) wa serikali wana mgomo fulani hivi! na shida ya nchi zetu za kiafrika ni priority zetu, kwetu sisi ni bora kununua magari mengi ya washawasha, kuliko kuimarisha huduma za afya! Kwa sasa watumishi wengi wa serikali wanaingia kazini ontime ila kacheki output yao mwisho wa siku ndo utajua tofauti ya gov na private sector! tukubali tukatae ni lazima serikali icheki tena namna pesa za walipa kodi zinavyotumika, hebu cheki vipato wanavyopata wabunge halafu leo hii mtu kasota kusoma chuo kama muhimbili tena karudiarudia weeee halafu anaanza kazi na anategemewa atende kazi kwa moyo wake wote! then kuna bint mbiiiichi kama yule mtoto wa Bulmbb ambaye hata miaka 24 hajafika keshapata mkopo wa gari ML 90, je ni wangapi watakuwa hivyo maana si wote wenye hofu kwamba wanawajibika kwa Mungu kabla ya wanadamu! Kiukweli vitu vya public quality duni!

Ndo maana ukifuatilia sana matendo ya serikali unaweza ishia mkufuru Mungu! cha msingi ni mtu kutafuta mafanikio kwa bidii na kutumia fursa zilizopo ili kuinufaisha jamii yako!
 
Back
Top Bottom