Hali ni mbaya ward A na B za watoto walioko MOI (Muhimbili)

madaktari wana wajua wagonjwa wao kwa moyo, kama amelazwaa siku zaidi ya moja, kumuuliza nurse kuhusu mgonjwa sio tatizo
 
Asubuhi ya leo nimetoka kumuona mgonjwa katika wodi ya watoto waliovunjika mifupa iliyopo Muhimbili chini ya taasisi ya MOI. Nilichokikuta kinasikitisha sana, na nilichosimuliwa na wazazi/walezi wanaowatazama watoto hao kinasikitisha zaidi

Nilichoona:
Vitanda vyote 23 katika wodi A vina wagonjwa wawili wawili, yaani maana yake kuna wagonjwa 46. Ukubwa wa wodi kwa uzoefu wangu wa metric units, ni 6m x 18m = 108 sq. metres

Kwa lugha ya ujumla, chumba chenye eneo la mita za mraba 108 kinatumika kuwalaza watoto 46, na hapo bado waangalizi wao wanaoshinda nao, ambao nao wapo 46, kufanya jumla ya msongamano wa watu 92 ndani ya kaeneo hako! Hapo nimeamua kuneglect watu wanaofika na kuondoka kwa lengo la kuwaona wagonjwa, kama mimi. Hiyo ni hali ya population density ambayo niliiona kwa macho yangu

Nilichosimuliwa:
Mzazi wa mtoto niliyeenda kumuona pamoja na mzazi wa mtoto mwezie wanaoshea kitanda, wamenieleza jinsi huduma ya hovyo inavyotolewa. Daktari anapopita hamuangalii mgonjwa na kutumia utaalamu wake kujua hali yake, bali anamuuliza muangalizi kuwa mgonjwa anaendeleaje, chochote atakachosema muangalizi ndicho hicho daktari anaandika na kuondoka kwenda kitanda kingine!

Hana muda wa kuangalia kiungo cha mtoto kilichovunjika kinaendeleaje, bali anatumia maelezo ya muangalizi pekee, halafu wala hachanganyi utaalamu wake, anaandika na kuondoka. Dada wa pembeni akalalamika kuwa ameambiwa asaini document ambayo hajui inahusu nini, na kwa kutumia udhaifu wa uelewa wa watu wetu, daktari/muuguzi amemsainisha tu.

Watoto wamewekewa mawe yananing'inia tu, hawapewi dawa yoyote! Jamani hakuna siasa hapa, waliopo Dar waende wodi ya watoto waliovunjika viungo leo hii wakafanye mahojiano hata kwa siri siri, halafu waje tuone kama kuna kuongeza chumvi au ndio hali iliyopo!

Wito:
Serikali iachane na siasa katika afya za wanadamu wananchi wake. Wataalamu wanaposema kuna upungufu wa vifaa,rasilimali watu au miundombinu ya hospitali, hatua za kurekebisha zichukuliwe, au walau watu waambiwe ukweli ili wajipange na wagonjwa wao kukabiliana na hali ya hospitalini. Wagonjwa wanaposema kuna uzembe wa wafanyakazi, hatua zichukuliwe. Hakuna haja ya kubishana kwenye vyombo vya habari kuficha uovu

Karibuni Muhimbili wodi ya watoto waliovunjika viungo, nyuma ya wodi ya Sewa Haji

cc: HKigwangalla

Wenyewe wanasema "hapa kazi tu"!!!! Hii dhihaka kubwa kwa watu wasiokuwa na hatia itatuangamiza waswahili. Niliwahi kushauri kuwa watanzania wanakosa huduma za jamii na ndo hitaji kubwa kwa waswahili hawa. Afya ikiwa safi na elimu ikawa safi, ajira watatafute wenyewe kutokana na maarifa waliopata. Viwanda tutajenga ikiwa tuna wataalam wazawa, sera nzuri sana ya viwanda ila tunaenda kutafuta wakoloni waje wejenge na sisi tunawatolea mimacho!!! Kwa sasa we are absolutely doing right thing in a wrong way. Vipaombele kila mtu anakuja na cha kwake na kabla hajamaliza alichokianza anarukia kingine nacho anaishia njian! Anyway, watanzania wanaona wenyewe na wanasikia kwa masikio yao, tunaishi kwa mujibu wa kile tulichoamua. "All actions results from thoughts, It's thoughts that matters".
 
Tunasema kila siku hii nchi doctor patient ratio na nurse patient ratio ni kubwa mno! Kwa hiyo tufanyeje sasa? Wagonjwa ni wengi, watoa huduma wachache na utawala hautuheshimu matokeo yake ndo hayo.

Solution hapa ni kuajiri Watumishi wengi kwenye kada za Udaktari na Unesi.
Tatizo lililopo kwa sasa ni Serikali hii kukosa vipaumbele. Mkuu wa kaya hataki kuajiri mpaka sasa anafanya uhakiki wa vyeti feki na mwaka unaishia. Wanatuambia wamekuta wafanyakzi hewa 17,000+ na hawa walikuwa wanalipwa mishahara ya Mabilioni.
Kwanini sasa wasiajiri Watu muhimu kama Madaktari ili hiyo pesa iliyokuwa inatumika kulipa HEWA iwalipe Madaktari wapya??
 
Vingine umekosea kuripoti ni vya kitaalamu mfano hizo tractions sio lazima dawa .
 
Kazi ya kuhudumia wagonjwa ni ya wito. Unapokuta dakitari anapita bila kumcheki mgonjwa ujue hakuna madili kwa mhusika na pia hajali kazi yake. Najua vijana wengi wanaosomea udakitari kwa sasa wanawaza kutoka na siyo kuutumia utaalamu wao kutatua changamoto, bali kila kijana anawaza anunue BMW, anawaza ajenge gorofa, anawaza awazidi wenzake.

Kuhusu vifaa kwa kweli nadhani ni janga la kitaifa, ni tofauti sana na nchi za wenzetu.
Ndugu unajua kuwa "profesa" maji marefu analipwa mshahara mkubwa kuliko wa profesa Janabi mkurugenzi wa taasisi ya moyo ya jakaya Kikwete, hapa ndo Penye tatizo hayo ya wito ni upuuzi na ubatili mtupu.
 
Solution hapa ni kuajiri Watumishi wengi kwenye kada za Udaktari na Unesi.
Tatizo lililopo kwa sasa ni Serikali hii kukosa vipaumbele. Mkuu wa kaya hataki kuajiri mpaka sasa anafanya uhakiki wa vyeti feki na mwaka unaishia. Wanatuambia wamekuta wafanyakzi hewa 17,000+ na hawa walikuwa wanalipwa mishahara ya Mabilioni.
Kwanini sasa wasiajiri Watu muhimu kama Madaktari ili hiyo pesa iliyokuwa inatumika kulipa HEWA iwalipe Madaktari wapya??
Mkuu nimekuelewa vizuri ,mbeya wazima lakini ?
 
Ndugu unajua kuwa "profesa" maji marefu analipwa mshahara mkubwa kuliko wa profesa Janabi mkurugenzi wa taasisi ya moyo ya jakaya Kikwete, hapa ndo Penye tatizo hayo ya wito ni upuuzi na ubatili mtupu.
Na ndiyo maana ili uonekane umefanikiwa Tz ni kwenda kugombea ubunge. Ila kusoma ni sawa na kujinyea kinyesi kichwani. Hakuna anayewajali ma dr, hakuna anayejua chnagamoto za wauguzi mahospitali. Wanasiasa wanaleta siasa kwenye afya za watu. Ila la wito lipo pale pale!
 
Kazi ya kuhudumia wagonjwa ni ya wito. Unapokuta dakitari anapita bila kumcheki mgonjwa ujue hakuna madili kwa mhusika na pia hajali kazi yake. Najua vijana wengi wanaosomea udakitari kwa sasa wanawaza kutoka na siyo kuutumia utaalamu wao kutatua changamoto, bali kila kijana anawaza anunue BMW, anawaza ajenge gorofa, anawaza awazidi wenzake.

Kuhusu vifaa kwa kweli nadhani ni janga la kitaifa, ni tofauti sana na nchi za wenzetu.
Naungana na wewe kuhusu madaktari hasa wa Muhimbili.

Mwezi wa tatu sasa wanazungusha rufaa ya jamaa yangu kwenda india. Tulipofuatilia wanataka 1,000K
 
kama unazYuria ajira jumla jumla bila kujali sekta nyeti unataji nini?

daktari atapita tu kama.ushahidi.

kama unazuia au unaweka zengwe kwenye posho za madaktari unataraji nini?

kama.afya na bombadi bora bombad unataraji nini?
 
Ndiyo sababu mashetani wanakamilisha mikakati yao ya kuifunga mitandao yote nchini. Wameweza kulizima na kuliteka Bunge na kulifanya kitengo cha MACCM. Sasa hivi adui yao mkubwa ni social media hivyo wako mbioni kuifunga.

Si waziri kasema nchi haina tatizo la huduma za afya? Huu utakuwa uchochezi. Haiwezekani kutumia mitandao kuipinga serikali! ;););):(:(
 
Kweli mkuu, nilikuwa na mgonjwa hapo ward za private Dr wake anaitwa Anthony Assey ni wa mishipa hajali,ana dharau naamna alivyokuwa anamchukulia mgonjwa yani unaweza tokwa machozi
 
Mtukufu anataka mpaka wote tuishi kama mashetani na kwa tabia hii ya kuletata habari umu ipo siku malaika 4G atazima mitandao ya kijamii kwa dua zake zilivyo,natamani kujua pesa tulizo okoa zinaenda wapi.
 
NB: Nilitaka nichukue picha lakini nafsi ikanisuta. Pamoja na nia yangu njema ya kutolea taarifa, lakini nikajiuliza kuwa kwa upande mwingine, hawa wauguzaji wanaweza wasijisikie vizuri kuchukuliwa picha katika mazingira hayo. Lakini nasisitiza, kwa aliyepo Dar, awe kama vile anapita tu, aingie ward hiyo ajionee
Atuko kisiasa bali tunaeleza hali halisi ya hapo muhimbili!kuna shemu wangu aliwahi kulazwa kwenye hiyo wodi siku niliyoenda kumuona sio siri roho iliniuma sana.
Ila kuna wapuuzi humu ukisema mazingira ya muhimbili na kuitaka serikali iwajibike kwa hili wao huja na matusi tu!
 
Bahati mbaya maslahi pekee ninayoweza ku'declare katika uzi huu ni uzalendo. Niliyeenda kumuona ni mtoto wa jirani yangu. Sina haja ya kufanya uchochezi, na ndio maana nikatoa wito kwa watu wenye sauti zaidi yangu waipaze huko juu, maana kwa hali ie, mtu anaenda kutibiwa lakini ajiandae pia kuambukizwa!
Mkuu nimekuelewa sana.....tatizo siku hizi mkweli ni mmoja tu nchi hii.
 
Ukifikiria kuhusu afya ukija elimu kama ni mzalendo unaweza ukachoka.tuweke siasa kando kwa sababu kichwa kinagonga tz bado kuna kazi kubwa sana
 
Na ndiyo maana ili uonekane umefanikiwa Tz ni kwenda kugombea ubunge. Ila kusoma ni sawa na kujinyea kinyesi kichwani. Hakuna anayewajali ma dr, hakuna anayejua chnagamoto za wauguzi mahospitali. Wanasiasa wanaleta siasa kwenye afya za watu. Ila la wito lipo pale pale!
Hapo kwenye wito ndo Penye kosa hapo, wanasiasa wanafuja mahana ya wito!. Kwanini basi wito usiwe universal kwa kila mmoja?. Usifanye siasa kama huna wito wa siasa, nirudie tena hicho unacho kiita wito ni uhuni wa wana siasa dhidi ya wana taaluma. Kumbuka dr, nurses, mwalimu hapeleki wito dukani na kupewa sukari!
 
Na mimi wala sijaelekeza jumba bovu kwa madaktari pekee, bali kwa yeyote anayewajibika katika eneo linalomuhusu
mkuu una hoja, lakini ungeenda kumuuliza afisa uhusiano wa MOI ungepata majibu sahihi, badala ya hao wamama.

tayari kuna jengo jipya pale kuna nafasi ya watoto watahamia huko hivi karibuni.. (kama umeingia utaona namba zimeanzia 2A) Wadi ya watoto itakuwa wadi 1A na 1B pale floor ya kwanza..
kutibu mifupa siyo sawa na magonjwa.. matibabu huwa yalisha kuwa planned tangu siku ya kwanza mgonjwa anafika, anachofanya daktari ni sawa kabisa. kuniniginiza mawe ( inatwa Traction) pia ni aina ya matibabu.
 
Back
Top Bottom