dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,126
- 49,385
... irabu ndizo herufi za sauti; bila irabu sauti haitoki katika lugha ya Kiswahili. Wakati irabu inaweza kutamkika yenyewe, herufi nyingine zote lazima ziambatane na irabu ili zitamkike; mf. (Bb) ba, be, bi, bo, bu; n.k. Hivyo, kwa usahihi zaidi mada yako ilitakiwa isomeke, "Hakuna neno la Kiswahili linalotamkika bila kuwa na irabu".Hakuna neno la kiswahili linaloweza kuwa na maana bila ya kuwa na irabu (a, e, i, o, u). Katika Lugha ya Kiswahili irabu ni moja ya vitu ambayo vinahitajika katika neno/maneno ya Kiswahili ili kuleta maana, hivyo hakuna neno la Kiswahili lenye maana pasipo kuwa na irabu
Lakini kwenye lugha nyingine neno linaweza kuwa na Maana hata pasipokuwa na irabu. Rejea Lugha ya kingereza ina maneno Kama vile shy, why, try, myth, n.k maneno hayo yanaleta maana sahihi pasipokuwa na irabu katika maneno hayo.
Japo inasemekana herufi Y katika Lugha ya kingereza ndio herufi muhimu na ambayo maneno mengi yasiyo tumia irabu hujumuisha herufi Y ili kuleta maana ya neno.
Ni ngumu neno la kingereza kuleta maana endapo likikosa irabu pamoja na herufi Y.
Hivyo herufi Y katika Lugha ya kingereza ni muhimu kama zilivyo irabu katika Lugha ya Kiswahili Herufi Y hutumika ili kuleta maana endapo zikikosekana irabu katika Lugha ya kingereza