Hakuna malipo ya NSSF, PPF hadi umri wa kustaafu ufike!

Hawa jamaa wana akili za ajabu sana, they know life expectancy ya Mtanzania ni around mid 40's, nani atafika huko besides if it's my money why not let me have it when I need it????? Mbona kodi zao wanachukua mapema???
 
Kwanini wasirekebishe muswada wa kiinua mgogo cha wabunge ambao kila miaka mitano wanapewa, yani mbunge achukue kiinua mgongo anapo malizana kabisa na siasa na endapo atarudi tena anatakiwa akirudishe hicho kiinua mgongo na atakapo maliza tena anapewa nusu yake kama mtu anaye resit mithiani naomba kuwasilisha
 
Hii ndiyo CCM.Chama kilichoamua kuangamiza vijana wa kitanzania.Salama yetu tu ni kuungana kwa umoja wetu na kuwakataa hawa madhalimu.
 
Wastani wa umri wa kuishi mtanzania ni miaka 50, unataka kulazimisha haki ya mtu hadi miaka 60 hiyo si ni sawa na kumyima hiyo haki yake. Marekebisho ya hiyo yangeangalia zaidi hali halisi ya mtanzania. Tumeshindwa kuendelea na billions of money kutoka kwa wafadhili je leo maendeleo yatakuja kwa kumnyima mtanzania haki yake.

Matarajio yetu sasa ili tanzania iweze kwenda mbele ni kuwajengea uwezo mtu mmoja mmoja ili kuwa na strong middle income people, sasa kwa kuwanyima haki yao ya msingi kwa kisingizio cha kupata fedha za maendeleo hii ni sawa na kuchimba kaburi la maendeleo ya Tanzania katika siku za usoni.

Tahadhari ni kuwa tunaweza kufanya mzaha na likawa kweli, hasa kwa kuwa wtz hatuna umoja katika masuala ya msingi kama hili. Tuendelee kuelimishana. Hata kama Bunge litapitisha basi wafanyakazi wote tuandamane.
 
Kwa sie wajasiriamali hilo halitugusi sana kwa kuwa hatupeleki fungu huko. ila hii itasababisha ukwepaji mkubwa wa uchangiaji maana watu watatafuta kila namna mishahara iwe understated hivyo PAYE itashuka as well hiyo changizo kwa hiyo mifuko.

Hadi kufikia 2015 tutashuhudia mengi. Ila hayana budi kuja ili Gamba litoke Mjengoni na UDHAIFU wake
 
naona sasa wanataka tuwashkishe ukuta.

anywayz nimechukuwa cheki yangu jusi baada ya kusungushwa karibu miezi miwili.
ukweli ndio uo wanataka tuwashikishe ukuta mikazi yenyewe migumu kuna mtu atafikisha miaka 50 nasikia wanataka kufanya hivyo hili kupunguza pressure ya deni lao nssf tuakikishe mpango wao haufanikiwi na tusiwaruhusu hata kujadili wakipeleka tu mswada tuvamie ukumbi wa bunge tuwaswage viboko p u .........vu zaoo shiiitt shame on them yaani nimekesirika sana
 
Na kama ktk hiyo miaka 65 nilifanya kazi mwaka mmoja tu, labda nilipokuwa na miaka 30 ndio niliweka nssf. Itabidi nisubiri miaka 35 ili nilipwe?je hiyo pesa itakuwa na thamani baada ya 35yrs?wafikirie tena, hiyo gumu banaa!
 
Asante kwa ufafanuzi.

Shida ni kuwa likishafika BUNGENI watasema NDIOOOOOOOOO wale wabunge wa CCM na kwa kweli hali haitakuwa nzuri hasa kwa sekta binafsi.

Wafanyakazi tulio PRIVATE toeni michango yenu ya mawazo nini kifanyike kuzuia udhalimu huu unaotaka kufanyika.
yaani mwana akuna kusubiri mpaka waseme nyookoooo dawa ni kuvamia ukumbi wa bunge na kuwacharaza bakora peoplez power inaweza mkiwaacha tu tumekwisha tusiwaruhusu hata kujadili yanasema hivyo kwa kuwa yenyewe yameshatimiza umri huo
 
Jamani humu JF hakuna wabunge kama akina Zitto, Mnyika, January watujulishe nini mkakati wa serikali juu ya hili?

TAHADHALI: kama tumezoea kuchukulia mambo ya kitaifa kirahisirahisi naomba TUAMKE na kusema NO katika hili.
 
Werema naye ni mwanachama humu, na yule mzinzi Chemba! Wafikishe ujumbe. Wakipitisha hawamalizi 2015
 
Jamani humu JF hakuna
wabunge kama akina Zitto, Mnyika, January watujulishe nini mkakati wa
serikali juu ya hili?

TAHADHALI: kama tumezoea kuchukulia mambo ya kitaifa kirahisirahisi
naomba TUAMKE na kusema NO katika hili.

kweli mkuu! hapa sasa wanatushika kubaya....
 
Ndo tabu ya kuwekeza na kukopwa na serikali maela ya kutisha!
Wakiipeleka bungeni lazima ipite bse kuna wabunge vichwa nazi!
Magonjwa yote haya hasa lifestyle diseases nani atafika 55-60 years?
 
Wana JF,

Hivi hii mifuko iko chini ya wizara gani?

Waandishi wa habari tusaidieni kuuliza undani wa jambo hili.

MUHIMU: Mwajiliwa USILALE katika kufuatilia juu ya hatima ya fedha yako, hawa CCM wanaweza wakaleta balaa kwa familia nyingi sana za wafanyakazi wengi ambao wamekua wakikatwa hela yao kwa muda. Kumbuka pia PAYE iko juu, hivyo Netpay anayopata mfanyakazi inamsaidia kugharamia mahitaji tu ya kawaida. Wengi wakiamini kuwa baada ya miaka michache aache kazi ili ajiajiri kwa mtaji wa NSSF. SASA ITAKUWAJE MTAJI UKIOTA MBAWA?
 
...mwonja asali haonji mara moja. Baada ya kuwakamua PAYE kiulaiiiini sasa mtakamuliwa PENSHENI. Yaani mtakamuliwa kotekote. Endeleeni kuimba solidarity forever kwenye majukwaa, huku kivitendo mkiwa kila mtu kivyake.
 
Sasahivi hatuna muda na hawa wapiga kelele bungeni kwani wao wanakuwa wameandaliwa mafao yao tayari.Tunatakiwa kuamka wafanyakazi muda wakujifanya wapole umeshakwisha wakipitisha tu inabidi tuandamane nchi zima bila kuingia makazini si sekta binafsi wala serikali kuu.
Hivi wanafikiria nini wakati mtu ukiacha kazi unabidi uchukue hela zako.Hawa watu wamefirisika kimawazo kbs.
 
Back
Top Bottom