Hakuna malipo ya NSSF, PPF hadi umri wa kustaafu ufike!

Huo ndo utaratibu ulivyo sasa nadhani, kuna exceptions lakini kwa ujumla hautakiwi kuchukua hadi umri wa kustaafu, ndo nilivyoielewa sheria nilipoiangalia, kuna thread humu tulijadiili hilo.
 
Kama itapita hakika itakuwa kilio kwa wafanyakazi wengi;
Kwa maisha ya sasa yalivyo na ugumu wa kila hali; magonjwa ya kila aina , BP, kisukari, HIV/AIDS , TB , malaria etc. Bado wanategemea watu tufike 55- 60yrs old. ..............Eeh Mungu tusaidie waja wako.

Na shilingi yetu inavyoshuka samani assume una miaka 35 mpaka ufikishe miaka 60 ni kasheshe na kazi hujapata sijui itakuaje
 
Hi wana JF,

Nimesikia kuwa kuna sheria imepitishwa kuwa HAKUNA TENA kuchukua hela za NSSF ukiacha kazi HADI UMRI wa kustaafu
ufike.

Mwenye kujua UKWELI atuhabarishe zaidi (NSSF au watunga sheria wetu).

Wafanyakazi wa sekta binafsi mnalijua hili?

Ndugu yangu bagain,

Kama kumbukumbu zangu zipo sawasawa, hii hoja imeshajadiliwa na kupitishwa na bunge letu, kwenye kikao chake cha April, 2012. Labda kwa vile kwenye bunge la April, kulikua na mjadala mkali zaidi wa ripoti ya CAG, na tishio la kumuangusha Waziri Mkuu, ndio maana wengi wetu tulipitwa na huu mjadala nyeti na muhimu sana kwa wafanyakazi.

Na nafikiri hata Mkuu wa nchi ameshamwaga wino kuifanya sheria kamili. Kinachosubiriwa ni Wizara ya kazi na Ajira, kumaliza mchakato wa kuandaa regulations za Sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ( na hapa inajumuisha mifuko yote yani NSSF, PPF, PSPF, LAPF na GEPF). Na kwa sheria hiyo mpya, mifuko yote itaruhusiwa kuandikisha wanachama kutoka sekta yeyote provided mfanyakazi husika amechagua huo mfuko.

Nimesikia wataweka clause ya kuruhusu mwanachama kukopa nusu ya balance ya michango yako kwa shughuli za maendeleo ambazo zitakua defined, nahela zinazobaki ni mpaka ufike umri wa kustaafu au uwaachie warithi wako kama ukifa kabla.

Nafkiri nimekuongezea mwanga kidogo kwenye Sheria ambayo IMESHAPITISHWA na BUNGE letu, labda la kujiuliza ni je maslahi ya mfanyakazi yatalindwaje?
 
Sijashangazwa na michango yenu humu kwa sababu nafikiri Watanzania bado hatujaelewa maana ya pensheni ni nini, lakini huu ni utaratibu wa watu angalau kuweka akiba, ili unapofikisha umri mkubwa huna uwezo wa kufanyakazi upate maisha yenye hadhi kwa kutumia ile akiba yako ambayo sasa inaweza kufidia kiasi cha fedha kwa kukosa mshahara, maana wakati huo hujiwezi. Humu ndani kutokana na hulka ya kupenda kutumia bila kuweka akiba mnaona kama huo mpango eti utafifisha ndoto zenu wakati ile ni just 5% ya mshahara ama 10% kwa sekta binafsi, 90% unaachiwa na hufiki popote na ndoto zako, najua hii hamtaipenda, hebu jiulizeni hapo mlipo mna akiba kiasi gani mmeweka wenyewe benki voluntarily, wengi ni kutumia tu, bia na kiti moto! mimi ningeona kweli hiyo ni sawa kabisa, let u guys be forced to save because hamwezi wenyewe, eti mtu atasema anataka ajenge nyumba, tumia hiyo 90% yako. Labda sasa tungesema kwamba okay, hatuchukui fedha lakini tutunze akaunti zetu huko na tukipata pesa kwa namna yeyote basi we can conribute ila mafao labdayaongezeke zaidi. lakini siyo kuzitumbua tu hizo fedha, nchi haina savings kabisa watu wanakula bata tu. hiyo sheria na ipite ili tulazimishwe kuweka akiba. Naunga mkono hoja.
 
nd. Kibai. Tatizo kubwa la social security zetu ni LOW INTEREST RATES. Haiwezekani nikatwe 1,000 leo halafu nipewe 1,001 baada ya miaka 30. Ndio maana watu wanataka wapewe chao. Vinginevyo viwango vikaribiane na COMMERCIAL & COMPOUNDED RATES. Kwa mfumo wa sasa mfanyakazi anapoteza kwa 'kuwekewa' akiba. Na hapo ndipo mrija ulipo.
 
wafanyakazi msijaribu kufumbwa macho juu ya hili. There will be many distractions.
 
hii Nchi bana ni sawa na mbwa anayekosa chakula halafu anakula watoto wake. Kama ni kweli, hata kufikiri tu kufanya hivo ni upuuzi. Serikali inayokula na kunyonya watu wake. Hell
 
Si kweli. Mimi nina miaka 30, nimechukua hela yangu Nssf Ijumaa Juni 22, 2012, na hadi leo Jumapili hakuna sheria yoyote iliyotungwa na bunge. Kinachosubiri umri huo ni pensheni, yaani malipo ya kila mwezi kwa waliochangia miaka 15 mfululizo na kufikia umri wa kustaafu i.e. Miaka 55 ya hiyari au 60 ya lazima
 
life expectancy ya Mtanzania in average ni miaka 47 sasa unapowaambia wangojee miaka 55 maana wangojee wakiwa kaburini??
Halafu kuna watu wengine wanapata vikazi vya muda tu kama mwaka mmoja kazi ikiisha unaweza kukaa hata miaka 4 hujapata nyingine so hicho kijisent walichokata usubirie miaka 55 wakati ukiwa umeshakufa??
 
Si kweli. Mimi nina miaka 30, nimechukua hela yangu Nssf Ijumaa Juni 22, 2012, na hadi leo Jumapili hakuna sheria yoyote iliyotungwa na bunge. Kinachosubiri umri huo ni pensheni, yaani malipo ya kila mwezi kwa waliochangia miaka 15 mfululizo na kufikia umri wa kustaafu i.e. Miaka 55 ya hiyari au 60 ya lazima
hujaelewa tuu kwa sasa hakuna sheria ila ndio muswaada unaenda bungeni!
 
Bargain,
Hii sio tetesi maana haijawa kama hivyo. Lakini umefanya vizuri kuleta hii habari katika kipindi hiki na kuwafanya waajiriwa wote Tanzania wakae mkao wa kula.
Ukweli ni kwamba serikali ina mpango wa kupeleka bungeni marekebisho ya muswada wa sheria wa mafao ya wafanyakazi kama ulivyopitisha ba bunge ili sasa kufanya wafanyakazi wote wanaokatwa akiba ya mafao (PPF,NNSF, PSPF,LAPF,GEPF n.k) kulazimika kutopata mafao yao kama hawajatimiza umri wa kustaafu(55-60).Mpango huu unaletwa kwa sababu serikali yenu haina namna ya kufanya na ingependa kupata boost ya mapato toka mifuko hii ili kuleta pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Mpango huu wa aibu na kandamizi utawaathiri wafanyakazi zaidi ya 700000 serikalini lakini kwa kipekee utaathiri na kuua ndoto za wafanyakazi zaidi ya 3000000 walio katika sekta binafsi kama vile makampuni, NGOs na wale waliojiajiri wenyewe na ambao wanatumia mifuko hii.
(Una imani kubwa kwamba wabunge wetu hasa wa upinzani wataupigia ngumu mpango huu nyonyaji ambao ni wa aina yake katika nchi zote za Afrika. Hii pia inatoa fursa kwa wafanyakazi wote nchini (hasa vijana) kutafakari na kuona jinsi serikali yenu inavyopanga kufifisha mipango yenu ya muda mfupi na ile ya kati. Kazi kwenu simameni na Chukueni Hatua Sasa.
HABARI NDO HIYO

One thing is for sure, they succeed and that will be the nail that seals their coffin!!
 
Kutokana ugumu wa maisha na kukosa ajira wanachama wengi tunateseka kwa kukosa jinsi ya kuishi. Makampuni yanatupunguza, NGO zinakufa na kadhalika sasa tunachotaka ni kushinikiza kutoa hela ndani ya mwezi mmoja hivi technologia kwenu inamaanisha nini? Kama wakati wa mwalimu miezi sita na leo wakati wa dhaifu miezi sita? Hamna computer, internet au nini tatizo lenu wiziwizi tu, hizi ni taarifa za awali kabla ya sheria yenu kandamizi tunaingia barabarani
 
Hi wana JF,

Nimesikia kuwa kuna sheria imepitishwa kuwa HAKUNA TENA kuchukua hela za NSSF ukiacha kazi HADI UMRI wa kustaafu
ufike.

Mwenye kujua UKWELI atuhabarishe zaidi (NSSF au watunga sheria wetu).

Wafanyakazi wa sekta binafsi mnalijua hili?

Hii kitu ya kuja kuwapa hela nikafe nikiwa tajiri wakati niliishi maisha ya kimasikani kamwe sitoweza kufanya hicho kitu!
 
Sijashangazwa na michango yenu humu kwa sababu nafikiri Watanzania bado hatujaelewa maana ya pensheni ni nini, lakini huu ni utaratibu wa watu angalau kuweka akiba, ili unapofikisha umri mkubwa huna uwezo wa kufanyakazi upate maisha yenye hadhi kwa kutumia ile akiba yako ambayo sasa inaweza kufidia kiasi cha fedha kwa kukosa mshahara, maana wakati huo hujiwezi. Humu ndani kutokana na hulka ya kupenda kutumia bila kuweka akiba mnaona kama huo mpango eti utafifisha ndoto zenu wakati ile ni just 5% ya mshahara ama 10% kwa sekta binafsi, 90% unaachiwa na hufiki popote na ndoto zako, najua hii hamtaipenda, hebu jiulizeni hapo mlipo mna akiba kiasi gani mmeweka wenyewe benki voluntarily, wengi ni kutumia tu, bia na kiti moto! mimi ningeona kweli hiyo ni sawa kabisa, let u guys be forced to save because hamwezi wenyewe, eti mtu atasema anataka ajenge nyumba, tumia hiyo 90% yako. Labda sasa tungesema kwamba okay, hatuchukui fedha lakini tutunze akaunti zetu huko na tukipata pesa kwa namna yeyote basi we can conribute ila mafao labdayaongezeke zaidi. lakini siyo kuzitumbua tu hizo fedha, nchi haina savings kabisa watu wanakula bata tu. hiyo sheria na ipite ili tulazimishwe kuweka akiba. Naunga mkono hoja.

Kabai tatizo sio kuweka akiba, tatizo la watu hapa ni kuwa, kuna watu wanataka kuastaafu kabla ya umri wa kisheria wa kustaafu ili wapate muda mzuri wa kufanya mambo binafsi na kufurahia maisha yao kabla hazijaja zile siku mbaya za uzeeni (ni mbaya kwa sababu kwa life style ya TZ, vichomi vinaanza mapema miaka ya 45 na unapofikia miaka 60, umeisha na unakuwa na uwezo mdogo sana wa kufurahiya maisha)/ Kumbuka kuwa maisha yako huyafurahii uzeeni! unayafurahiya ujananani!!

Baadhi yetu tumataka kuondokana na utegemezi wa kutufanya watumwa wa waajiriwa wetu, kwa sheria hii inafanya watu sasa kama ataweka akiba yake ana kuamua kuwekeza akiwa na miaka 35 na akaacha kazi atalazimika kuziacha fedha zake kwa miaka 25!! this is not fair kwa inflation rate ya NCHI YETU!! lakini kwa wale walio na ndoto za kustaafia kazini hapa wamefika na hawana tatizo na hili.

Nilitegemea kabla ya kuandaa sheria hii waataalam wetu wangekuja na Data (takwimu) za ni watu wangapi na kwa namna gani waliochukua fedha yao mapema wameathirika kwa kushindwa kuzimanage, na wale walio staafu katika umri wa 55-60 wamefanya vizuri then wauconvise umma kuwa kuna umuhimu wa kuweka fedha yao mpaka ustaafu au vinginevyo. LKn hii mambo ya kutusaidia kufikiri na kutuamulia na kutupeleka kama mabwege haufai hata kidogo.
Ninaona kuwa mashirika haya ya kijamii wanataka kukamata hela ya watu wainvest walinde maslahi na mafao yao, waiushawishi umma kuwa hatujui kulinda future yetu!

Hivi mwenye kujua kuhusu PPF, maana ninavyo jua ili iningie kwenye pension scheme ni mpaka ucontribute kwa miezi 120 ambayo ni sawa na miaka 10. JE hii ina maama kuwa kwa sheria hii imeoverule hiki kigezo cha awali? na hata mashirika mengine kulikuwa na criteria ya kuingizwa kwenye pension scheme ambazo ndio unasubiri mpaka umri wa kustaafu!

Binafsi Hili ni pigo kwangu!
 
Back
Top Bottom