Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,336
- 10,896
- Thread starter
- #261
Ni kweli wazazi wengine wameiishi kwa kima cha chini wengine kwa biashara ndogondogo. Unspokua wanafurahi sasa mtt kakuwa mzigo utapungua. Ukibaharika kurithi mali kwa wazazi mshukuru tu Mungu. Kikubwa ni elimu iwe ya shule au ya msisha. Wazee wa zamani waliwarithisha watt wao ujuzi kama kuwinda, uvuvi ususi, ujenzi, uhunzi nk.
Mungu hukulipa hapa hapa duniani. Tena wakati mwingine huweza kumtumia hata mkeo au wanao kukuadhibu ikiwa ulimuasi ukiwa kijana.
Mhubiri 12
1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;
5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
