Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

hata Mimi SIKUBALIANI naye huyu haiwezekani watoto wasipowaangalia wazee alitaka Nani awatizame hapa ndio utaona tofauti ya dini ya kweli Na dini batili


Mkuu hapa atuzungumzii ishu ya dini. Lakini kwa muktadha huo dini husika inaendekeza uvivu eti kisa watoto watakulea. Ndio maana waamini katika dini husika hujiolea tuu na kuzaa hovyo bila akili kama wanyama
 
Kama upo vizuri kichwani naomba unipe maudhui makubwa matatu ya maandiko haya:
Luka 15
11 Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;
12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.
13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.
15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu.
17 Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.
18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;
19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.
20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.
25 Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.
26 Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?
27 Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima.
28 Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi.
29 Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;
Baki na laana zako mzee...
 
Mkuu hapa atuzungumzii ishu ya dini. Lakini kwa muktadha huo dini husika inaendekeza uvivu eti kisa watoto watakulea. Ndio maana waamini katika dini husika hujiolea tuu na kuzaa hovyo bila akili kama wanyama
Labda Kuna mtu unakusudia kumtukana hapa vinginevyo umejibu kichuki zaidi kwa hiyo naomba uelewe kuwa kuoa ni ibada Na kuzaa ni majaaliwa ya mungu wangapi wana wake lkn hawajazaa Yaani wagumba Na wangapi wanabaka. Na wamejaza watoto
 
Hahahahaaaa... Wazee marijali siyo?
Ni balaa kuna watu sijui huwa wanawaza nini, huna investment yoyote unazaa mtoto katika umri wa miaka 60
Nazani siyo Tanga tu bali mwambao wa Pwani Kwa ujumla kuna hiyo kasumba!
Unakuta Mtu umri umeenda lakini anatotoa tu kisha akiondoka anaachia wenzie wigazi!
Mkuu hii ipo maeneo mengi tu, kwingine unakuta migogoro ya kifamilia inapelekea kutengana mzee anatafuta mke mwingine anaendelea kuzaa hata kama ana watoto wakubwa tayari
 
Labda Kuna mtu unakusudia kumtukana hapa vinginevyo umejibu kichuki zaidi kwa hiyo naomba uelewe kuwa kuoa ni ibada Na kuzaa ni majaaliwa ya mungu wangapi wana wake lkn hawajazaa Yaani wagumba Na wangapi wanabaka. Na wamejaza watoto


kuoa bila utaratibu ni upumbavu. Haina tofauti na wanyama. Kila kitu kwenye maisha ni ibada ila usipofuata utaratibu ni upumbavu
 
Mkuu inauma sana kuona tabia hii ikiendekezwa katika jamii. Amini nakuambia ukifanya kazi vizuri ujanani na kuwekeza uzeeni utakuwa msaada mkubwa kwa watoto na wajukuu zako wasio wepesi wa kuchangamkia fursa
Nadhani hapo nimekuelewa kwamba kila mtu(mwanaume) apambane kwa nafasi yake kujiwekea akiba ya uzeeni,kwa hiyo hata watoto wa kiume hakuna kuwawekea utajiri uliopambana kupata,na wao wapambane watengeneze za kwao (si ndiyo uanaume!???)

Sasa ukipambana ukawaachia wao watapambanaje wakati wewe umeshapambana kwa niaba yao???

Vijana wa leo,pambaneni kujiandalia uzee wenu,watoto wenu nao watapambana kupata vyao,miradi yako komaa nayo mwenyewe,na watoto wako watapambana kutafuta miradi yao!!!!
 
Back
Top Bottom