CONTROLA
JF-Expert Member
- Sep 15, 2019
- 6,939
- 22,989
Mwaka unaisha leo ndio tunafunga Nov kesho ndio 1st Dec zinabaki siku tu sio mwezi tena wala miezi tufunge 2022 and if God wish ikimpendeza tuingie 2023 tukiwa na Mipango na mikakati mipya ya nguvu mno.
Nadhani hii itakuwa Funga mwaka yangu ya 2022, tangu huu mwaka uanze tumepiga story za biashara nyingi tofauti tofauti, wapo waliofanikiwa anzisha na wapo ambao bado idea zao zipo kwenye diary zao na notebook za simu zao.
Tunaendelea kushauriana biashara za kufanya kama vijana,lakini leo sichambui wala kupoint biashara yoyote ile bali nataka kufungua uwezo wa kufikiria kwa mtu ambae ameganda haelewi afanye nini.
Watu wengi wana mitaji,nina ushuhuda PM kila anaenifata anasema ana mtaji ila haelewi afanyie nini,watu wana mitaji mizuri ya kushangaza lakini ndio hivyo hawaelewi nini cha kufanya,....
Ngoja niwambie ndugu zangu,katika uwanja wa biashara hadi leo hii hapa tulipo Hakuna biashara mpya (hilo weka akilini mwako) yani liweke na ulitambue hilo tena kwa herufi kubwa.
Watu wengi wanaonifata PM anakwambia anataka umshauri chakufanya,ukimshauri anakwambia hicho kitu Kipo jirani yangu kuna mtu anakifanya.
Huwa mtu akishaniambia hivyo namtoa kwenye kundi la wafanyabiashara halafu nampotezea na ndio haoni tena nikiendelea jibu Msg zake...
kwann? biashara tunafanya ili tupate hela hatufanyi ili tuonekane sisi ni tofauti na wao,sasa kama nakushauri namna ya kupata pesa halafu unasema "jirani yangu yeye tayari anapiga pesa" maana yake wewe hutaki zile pesa umeridhika kwa moyo mmoja aendelee kuzipiga peke ake... (huo ni uduanzi)
Ok tuendelee... ninachosema ni kwamba biashara zinafanywa na kila mtu,leo hii ukishika mtaji wako usianze waza sijui nani anafanya nini au nani hafanyi nini,angalia moyo wako unataka nini kisha shirikisha ubongo wako,malizia na ushauri kidogo toka kwa wafanyabiashara walio ktk game unaowaamini the Do it.
Biashara nyingi zilizopo zina kasoro,nyingi mno mno, Mimi ni mfanyabiashara lakini pia ni mteja kwenye biashara za wengine,Jamani nawambia hiviii kasoro ni nyingi sana sana sana ktk kila biashara ninayoenda au ninayoiona around me.
Huwa mimi sio mtu wa kuanZisha jambo jipya,sijafikia level za kina Coca Cola mimi wao ndio wanaweza toa soda ina ladha ya Binzari na wakakomaa hadi watu wakaizoea, NOT ME.
Mimi ni mtu ninae angalia wapi pana udhaifu na kupita na huo huo udhaifu wa mwenzangu,biashara ni hizi hizi wapendwa unapotaka fungua biashara leo ukagundua unahitaji fungua duka la mangi, eneo A nenda eneo hilo hilo kwenye maduka ya mangi maeneo hayo Fanya Shopping ukweli..
utagundua nini wanacho nini hawana na kwanini hawana,ukishagundua list ya vitu ambavyo hawana una uwezo wakufungua duka mitaa hiyo hiyo na kuweka vitu ambavyo hawana na kuongezea maradufu ya vingine wasivyo navyo.
Watu wengi wanafanya biashara kwa mazoea,wengi sana hawafanyi biashara kuondoa changamoto za watu wa eneo husika ila wanafanya biashara ili wapate pesa.
Mtu anafungua duka la mangi, malengo lazima yawe mawili
1.Upate Pesa na
2.usaidie na kuondoa changamoto zote za wa majumbani.
Watu wengi hukomaa na point no 1 wanaangalia zaidi Pesa na sio kusaidia wananchi wa eneo husika ndio maana unaweza kwenda duka la mangi akakwambia hana unga wa lishe, ni rahisi kukwambia hana mafuta ya alizeti,ni rahisi kukwambia hana sabuni za chooni,nk nk
kwanini hana? kwasababu ni vitu vina wateja wachache na yeye yupo kimaslahi zaidi hataki pesa yake ikae tu. amekomaaa na (kupata pesa zaidi) na sio kuondoa changamoto za watu wa eneo lile.
Huo ni udhaifu wake na ndio point kwako mwenye mtaji wako mkononi, wafanyabiashara 90% wa sasa hivi wanafanya biashara ili wapate pesa na sio ili kusaidia wananchi.
Ndio mana unaweza tafuta kitu flani maduka ya mtaani ukakikosa kila unae enda anakwambia "hicho mpaka kariakoo" au hicho "mpaka sokoni" na hcho unachokiuliza ni 1 ya vitu vilivyo katika kundi la vitu anavyouza lakini yeye Hauzi.
Haya ni madhaifu ya wafanyabiashara wengi sana sana,usihangaike kuwaza jambo jipya Fanya kwa ubora biashara hizo hizo wanazozifanya wao kimazoea waonyeshe namna biashara inatakiwa kufanywa.
Mtu ni WAKALA wa E.Money ukienda kwake unamuuliza Una TTCL PESA (sina) una Z-PESA zantel (sina) una HALO PESA (sina) sasa kila kitu huna yeye ana tigo,voda na airtel, kwani hyo mitandao mingine ina shda gani hata kama haina wateja kuna shida gani ukiwa nayo? madhaifu ya namna hiii ndio Point kwako wewe mwenye Mtaji.
Kuna mtu ana BUCHA la nyama,unafika buchani una utumbo,(sina) una nyama ya kusaga (sina) khaa sasa shida nini? halafu kuna mtu ana mtaji hataki kufungua bucha kisa kuna mtu kafungua,angejua huyo aliefungua anaboa sema ndio hvyo wateja hawana pa kwenda asinge hata jifikiria mara mbili.
Wapendwa hakuna biashara mpya nasema tena biashara zote ni yebo yebo labda kuuza karanga kwenye ndege ndio inaweza kuwa mpya,ila zilizo salia zote zishafanywa na zinaendelea kufanywa.
Unapowaza chakufanya hebu angalia madhaifu ya mwenzako kisha jipange fungua biashara hiyo hiyo kwa ubora na kuzingatia 1 na 2 (pesa na kuondoa changamoto) usiangalie pesa tu kama wengine.
Binafsi mimi sio mtu mzuri sanaaaaa ktk biashara,maana ni dk 0 tu utanichukia ukinialika ofisini kwako nikija kukutembelea nikakuta unafanya vitu mvurundo my dear sitomaliza mwezi utaona mtu kafungua biashara kama yako eneo hilo hilo ulipo.
Siku zote napenda challenge hakuna raha ndugu zangu kama kufanya biashara ya ushindani,yani raha sanaaaa and i like it mno hivyo napenda sana kufungua biashara sehemu ambazo watu wanafanya biashara kimazoea.
Usiwaze chakufanya na huo mtaji ulio nao, pita hapo mtaani kwako angalia eneo kisha angalia nani kalegea legea halafu jisachi mfukoni unajiona una cash ya kufungua biashara kama yake? kama jibu ni NDIO hiyo hiyo ndio biashara ya kufungua.
Acha kutafuta biashara mpya utapasuka kichwa UFE uanze sema biashara sio fungu lako wakati wenzako kila siku wanafungua maduka kila mtaa.
Kazi kwetu, Happy 2022>
Nadhani hii itakuwa Funga mwaka yangu ya 2022, tangu huu mwaka uanze tumepiga story za biashara nyingi tofauti tofauti, wapo waliofanikiwa anzisha na wapo ambao bado idea zao zipo kwenye diary zao na notebook za simu zao.
Tunaendelea kushauriana biashara za kufanya kama vijana,lakini leo sichambui wala kupoint biashara yoyote ile bali nataka kufungua uwezo wa kufikiria kwa mtu ambae ameganda haelewi afanye nini.
Watu wengi wana mitaji,nina ushuhuda PM kila anaenifata anasema ana mtaji ila haelewi afanyie nini,watu wana mitaji mizuri ya kushangaza lakini ndio hivyo hawaelewi nini cha kufanya,....
Ngoja niwambie ndugu zangu,katika uwanja wa biashara hadi leo hii hapa tulipo Hakuna biashara mpya (hilo weka akilini mwako) yani liweke na ulitambue hilo tena kwa herufi kubwa.
Watu wengi wanaonifata PM anakwambia anataka umshauri chakufanya,ukimshauri anakwambia hicho kitu Kipo jirani yangu kuna mtu anakifanya.
Huwa mtu akishaniambia hivyo namtoa kwenye kundi la wafanyabiashara halafu nampotezea na ndio haoni tena nikiendelea jibu Msg zake...
kwann? biashara tunafanya ili tupate hela hatufanyi ili tuonekane sisi ni tofauti na wao,sasa kama nakushauri namna ya kupata pesa halafu unasema "jirani yangu yeye tayari anapiga pesa" maana yake wewe hutaki zile pesa umeridhika kwa moyo mmoja aendelee kuzipiga peke ake... (huo ni uduanzi)
Ok tuendelee... ninachosema ni kwamba biashara zinafanywa na kila mtu,leo hii ukishika mtaji wako usianze waza sijui nani anafanya nini au nani hafanyi nini,angalia moyo wako unataka nini kisha shirikisha ubongo wako,malizia na ushauri kidogo toka kwa wafanyabiashara walio ktk game unaowaamini the Do it.
Biashara nyingi zilizopo zina kasoro,nyingi mno mno, Mimi ni mfanyabiashara lakini pia ni mteja kwenye biashara za wengine,Jamani nawambia hiviii kasoro ni nyingi sana sana sana ktk kila biashara ninayoenda au ninayoiona around me.
Huwa mimi sio mtu wa kuanZisha jambo jipya,sijafikia level za kina Coca Cola mimi wao ndio wanaweza toa soda ina ladha ya Binzari na wakakomaa hadi watu wakaizoea, NOT ME.
Mimi ni mtu ninae angalia wapi pana udhaifu na kupita na huo huo udhaifu wa mwenzangu,biashara ni hizi hizi wapendwa unapotaka fungua biashara leo ukagundua unahitaji fungua duka la mangi, eneo A nenda eneo hilo hilo kwenye maduka ya mangi maeneo hayo Fanya Shopping ukweli..
utagundua nini wanacho nini hawana na kwanini hawana,ukishagundua list ya vitu ambavyo hawana una uwezo wakufungua duka mitaa hiyo hiyo na kuweka vitu ambavyo hawana na kuongezea maradufu ya vingine wasivyo navyo.
Watu wengi wanafanya biashara kwa mazoea,wengi sana hawafanyi biashara kuondoa changamoto za watu wa eneo husika ila wanafanya biashara ili wapate pesa.
Mtu anafungua duka la mangi, malengo lazima yawe mawili
1.Upate Pesa na
2.usaidie na kuondoa changamoto zote za wa majumbani.
Watu wengi hukomaa na point no 1 wanaangalia zaidi Pesa na sio kusaidia wananchi wa eneo husika ndio maana unaweza kwenda duka la mangi akakwambia hana unga wa lishe, ni rahisi kukwambia hana mafuta ya alizeti,ni rahisi kukwambia hana sabuni za chooni,nk nk
kwanini hana? kwasababu ni vitu vina wateja wachache na yeye yupo kimaslahi zaidi hataki pesa yake ikae tu. amekomaaa na (kupata pesa zaidi) na sio kuondoa changamoto za watu wa eneo lile.
Huo ni udhaifu wake na ndio point kwako mwenye mtaji wako mkononi, wafanyabiashara 90% wa sasa hivi wanafanya biashara ili wapate pesa na sio ili kusaidia wananchi.
Ndio mana unaweza tafuta kitu flani maduka ya mtaani ukakikosa kila unae enda anakwambia "hicho mpaka kariakoo" au hicho "mpaka sokoni" na hcho unachokiuliza ni 1 ya vitu vilivyo katika kundi la vitu anavyouza lakini yeye Hauzi.
Haya ni madhaifu ya wafanyabiashara wengi sana sana,usihangaike kuwaza jambo jipya Fanya kwa ubora biashara hizo hizo wanazozifanya wao kimazoea waonyeshe namna biashara inatakiwa kufanywa.
Mtu ni WAKALA wa E.Money ukienda kwake unamuuliza Una TTCL PESA (sina) una Z-PESA zantel (sina) una HALO PESA (sina) sasa kila kitu huna yeye ana tigo,voda na airtel, kwani hyo mitandao mingine ina shda gani hata kama haina wateja kuna shida gani ukiwa nayo? madhaifu ya namna hiii ndio Point kwako wewe mwenye Mtaji.
Kuna mtu ana BUCHA la nyama,unafika buchani una utumbo,(sina) una nyama ya kusaga (sina) khaa sasa shida nini? halafu kuna mtu ana mtaji hataki kufungua bucha kisa kuna mtu kafungua,angejua huyo aliefungua anaboa sema ndio hvyo wateja hawana pa kwenda asinge hata jifikiria mara mbili.
Wapendwa hakuna biashara mpya nasema tena biashara zote ni yebo yebo labda kuuza karanga kwenye ndege ndio inaweza kuwa mpya,ila zilizo salia zote zishafanywa na zinaendelea kufanywa.
Unapowaza chakufanya hebu angalia madhaifu ya mwenzako kisha jipange fungua biashara hiyo hiyo kwa ubora na kuzingatia 1 na 2 (pesa na kuondoa changamoto) usiangalie pesa tu kama wengine.
Binafsi mimi sio mtu mzuri sanaaaaa ktk biashara,maana ni dk 0 tu utanichukia ukinialika ofisini kwako nikija kukutembelea nikakuta unafanya vitu mvurundo my dear sitomaliza mwezi utaona mtu kafungua biashara kama yako eneo hilo hilo ulipo.
Siku zote napenda challenge hakuna raha ndugu zangu kama kufanya biashara ya ushindani,yani raha sanaaaa and i like it mno hivyo napenda sana kufungua biashara sehemu ambazo watu wanafanya biashara kimazoea.
Usiwaze chakufanya na huo mtaji ulio nao, pita hapo mtaani kwako angalia eneo kisha angalia nani kalegea legea halafu jisachi mfukoni unajiona una cash ya kufungua biashara kama yake? kama jibu ni NDIO hiyo hiyo ndio biashara ya kufungua.
Acha kutafuta biashara mpya utapasuka kichwa UFE uanze sema biashara sio fungu lako wakati wenzako kila siku wanafungua maduka kila mtaa.
Kazi kwetu, Happy 2022>