ukweli husimama wenyewe, ZZK ni mshindi hilo halina ubishi! utambeza tu ila ukweli mchungu unabaki pale pale bilioni elfu moja na mia tano majasho ya wanyonge na walala hoi bongo zimeliwa mchana kweupe! Mungu atuangazie nuru yake na upande wetu manake hatuna pa kukimbilia sasa! ripoti ya CAG iko wazi kwa public na inasambaa kwa whatsapp kwa kila mtu, kila kitu kiko sebuleni sasa! ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni, hili ni janga la kitaifa! hizo ni pesa zimevunja rekodi kuwahi kuibwa bongo! Eee mwanamama mwanasheria shupavu uliekalia kiti kikubwa umesikia hili? mbona uko kimya sasa? ni utawala upi wa sheria unaoupigania? anza na hili sasa tuone kweli unapigania uhuru wetu wa binafsi, ila kumbuka mfupa huu ni mgumu mno kuutafuna unatakiwa kujitoa mhanga!.
nadhani wa kupingana na kulumbana nae si ZZK ni kupangua hoja na tuhuma zilizoko kwenye ripoti yenyewe! yani wahusika kusema tu hizo 1.5T ziko wapi na kuweka risiti ya matumizi yake mezani , basi kama hilo haliwezekani basi jibu rahisi ni kuwa zimepigwa na serikali hii ya awamu ya tano na ni wazi kwa wabongo wachache wenye akili kuwa ZZK ni mshindi na Mungu atamlinda hakuna binadamu anaweza kumfanya chochote , binadamu ni viumbe dhaifu kabisa, akifika home jioni yuko hoi hutupa kule masuti aliyovaa mchana kutwa masuti ambayo yametokana na kodi , kodi iliyotokana na kuvuja jasho kwa watu wanyonge basi mabosi hawa kama walivyo mafukara wakulima "hufa" kila siku giza liingiapo (kulala) na siku moja hulala kimya na kuwa baridiiiiiiiii na kulazwa ndani ya udongo na juu yake huwekwa mifuniko ya zege ili hata wakifufuka kwa bahati mbaya wasitoke wasubiri tu huko huko mavumbini SIKU YA KIAMA watakapokamuliwa majasho ya wanyonge na JAJI wa MAHAKAMA KUU ya Mbinguni Allah SW!! kwanza siku zenyewe si nyingi ni miaka sabini ikizidi sana themanini nyimbo mapambio magwaride na mafataki lazima yakuhusu marehemu mtarajiwa, duniani tunapita tu wizi wa nini ndugu zetu wenye vyeo vya kidunia hata Mungu hawajui?
ili tuendelee mbele ni vizuri tujenge utamaduni wa kukubali kukosolewa na kushindwa! katika hili Mwami ameshinda kwa kishindo laivu bila chenga, na hakuna awezae kumfanya chochote kwakuwa ametanguliza kinga ya Muumba wake. nadhani nia ya Mkulu ndio dira ya maendeleo thabiti na sasa ripoti inataja wizi wote ofisi zote na wote waliohusika , mkulu ajifungie ndani aisome ripoti taratibu na atumbue tu wezi na wazembe wote idara zote, ngazi zote na ofisi zote bila ajizi na kwa reason ya CAG report tu otherwise juhudi zake kuipaisha bongo ni kazi bure mkulu anatumia nguvu kubwa kujaza maji kwenye pipa huku watendaji wake wengine wanamchora wanamcheka na wanamng'ong'a tu kwa kutoboa pipa kwa chini na kufaidi majasho ya wanyonge, kamwe maji hayatajaa kwenye pipa la mkulu!asiangalie ukoo, level, cheo, jina wala sura!mkulu tupa kule majizi na wazembe wote!CCM oyeee!