Yani natamani Sana ndoa sijui kwanini ,Yani natamani niwe na mwanaume wangu nimdekeze nisumbue sumbue kumnyoshea nguo kumpikia akipendacho [emoji39][emoji39][emoji39][emoji39][emoji39] yaniiia
Ila naona wakati bado niliambiwa jf ntapata nimejaribu naona hakuna mwenye uhitaji wa kuoa
NgojA niendeleee kusubiri [emoji41]
Ndoa jambo la staha, kukutoa kwa karaha
Doa kando kwa furaha, kukuoa si jeraha
Ukenda tambo kulala, hutopoa kifukara
Japo umekuwa peke, hutopigwa kwa mateke
Japo umekuwa peke, hutopigwa kwa mateke
Epuka wenye makeke, na kuiga kula kete
Wajivuni walo tete, wenye kusiliba pete
Japo ndoa waitaka, sijitie takataka
Japo ndoa waitaka, sijitie takataka
Fungu la kukosa pata, sijiweke kwa chakacha
Nadhiri iweke hata, usichekwe kwa kuachwa
Penye nia pana njia, takuja wa kuchumbia
Penye nia pana njia, takuja wa kuchumbia
Tena asije kwa gia, na nia kukuibia
Weka makini pazia, kutenga warubunia
Baada ya dhiki faraja, kwa mwanamke wa haja
Baada ya dhiki faraja, kwa mwanamke wa haja
Mume ajenge daraja, na kulea waje waja
Harusi tafana yaja , midomoni kuitaja
Siku moja itafika, kamwe hutanung'unika
Siku moja itafika, kamwe hutanung'unika
Tapata wa kukushika, nawe pia utafika
Kwa cheko la uhakika, si la kimbio za nyika
Mapenzi yakikutaka, huna budi kuyapata
Mapenzi yakikutaka, huna budi kuyapata
Na kama hayajakata, utaringa tayvotaka
Ila kuyafatafata, bila salamu tadata
Kiangazi kinakwisha, maisha yatamasika.