Furaha za watu wengine zinasogezwa mbele kila siku, nikiwa mkubwa nitafurahi, nikimaliza la saba nitafurahi, nikimaliza sekondari nitafurahi, nikimaliza chuo nitafurahi, nikipata kazi nitafurahi, nikioa au kuolewa nitafurahi, nikizaa mtoto nitafurahi, nkistaafu nitafurahi, mwisho nikifa nitafurahi, furaha zenu mnazisogeza mbele tu kila siku, acheni mambo hayo, mwenye furaha upata mambo ya kumfurahisha usijalibu kusogeza furaha zako mbele, inaanza furaha ndio yanafuata mambo ya kukufurahisha, kuwaangalia vimbwengo wanaotuzunguka tu kunaleta furaha ya nini, usogeze furaha yako mbele, furahi tu na hayo ya kukufurahisha yatakufuata.